Kama tuna haki tudai lakini tuepuke mihemko! Refa wa kati tunamuangushia jumba bovu!

Kama tuna haki tudai lakini tuepuke mihemko! Refa wa kati tunamuangushia jumba bovu!

Kwa hiyo tuelewe kwamba kuidhinisha hili ni goli au siyo goli si kazi ya refa?
Kwa uelewa wako,uwanjani Kuna marefa wangapi?Hao wengine wako kwa ajili gani?je,kila tukio tatanishi,refa wa Kati anapaswa kwenda kuamua mwenyewe?Je,uamuzi wa refa mmoja na uamuzi wa marefa watatu kwenye tukio moja,ni upi more likely to be correct?
Je,referee angeambiwa ni goli na wasaidizi wake na akaweka mpira Kati,angepata hizi lawama kwanini hajaenda yeye binafsi kuangalia?
Uwanjani majukumu yamegawanywa,wasaidizi wake wakimwambia kuwa mpira umevuka mstari wa goli basi hiyo inatosha kwa refa kuweka mpira Kati!
 
Tatizo hatuwaungi mkono DSTV,we VAR gani ni upande mmoja tu ina maana DSTV walishindwa kuweka kamera tatu golini tuone na video za upande mwengine.azam angepewa hiyo tenda mbona makamera yanamwagika tu.
 
Wanakaza mafuvu tuu

Tukio la offside au mpira kuvuka line, huamuliwa na teknolojia moja kwa moja refa yeye hupewa taarifa tuu na chumba cha VAR kuwa ni goli au sio goli

Matukio kama penati, faulu, mtu kunawa mpira, hayo yanahitaji utashi wa refa kuamua hivo kujiridhisha

Nimewashangaa sana Yanga na wachambuzi kulinganisha tukio la lomalisa na hilo la goli
 
Kosa labda ni kutooneshwa ni namna gani mpira ulionekana baada ya kuchora line kama tunavooneshwa kwenye offside,

Sio kulaumu eti kwanini refa hakwenda kuangalia wakati haamui yeye tukio kama hilo
 
Wanakaza mafuvu tuu

Tukio la offside au mpira kuvuka line, huamuliwa na teknolojia moja kwa moja refa yeye hupewa taarifa tuu na chumba cha VAR kuwa ni goli au sio goli

Matukio kama penati, faulu, mtu kunawa mpira, hayo yanahitaji utashi wa refa kuamua hivo kujiridhisha

Nimewashangaa sana Yanga na wachambuzi kulinganisha tukio la lomalisa na hilo la goli
Hatimaye nimekutana na comment ya mtu anayeelewa mpira!
 
Kosa labda ni kutooneshwa ni namna gani mpira ulionekana baada ya kuchora line kama tunavooneshwa kwenye offside,

Sio kulaumu eti kwanini refa hakwenda kuangalia wakati haamui yeye tukio kama hilo
Exactly
 
Wakuu,kuna suala nimeliona kuanzia kwa mashabiki,wachambuzi na hata viongozi mbalimbali juu ya mechi ya Yanga vs Mamelods!
Lawama nimeona zikienda kwa refa wa kati kwa kuacha kwenda kuangalia VAR kuhusu mpira wa Aziz Ki lakini akaenda kuangalia foul ya Lomalisa kwenye VAR ili aangalie kama ilistahili kadi nyekundu au la!
Ndio hapo naona watu wanachanganya,wanashindwa kuelewa majukumu ya refa wa kati!Nitaeleza kwa ufupi na mwenye kuelewa ataelewa cha msingi usitangulize mihemko!

*Refa wa kati huwajibika kwenda kuangalia VAR pale ambako kuna tukio la utata ambapo ataenda kujiridhisha!Matukio haya ni yale ambayo yeye kama refa wa kati ana uwezo wa kuamua kwa utashi wake!Mfano matukio ya penalty na foul,mambo hayo hutegemea utashi wa refa!Refa anaweza kuamua iwe penalty au isiwe penalty,anaweza akaamua iwe kadi ya njano au nyekundu!Hapo VAR haimwambii kuwa atoe kadi ya njano au nyekundu bali anatumia utashi wake kwa kuzingatia kanuni za mpira wa miguu!VAR haimwambii refa wa kati atoe penalty au asitoe,ni utashi wake kulingana na kile anachokiona!

*Sehemu ya pili ni matukio ya utata ambayo refa wa kati hana utashi nayo!Matukio haya ni kama Offside na mpira kuvuka mstari wa goli!Matukio haya huamuliwa na VAR moja kwa moja!Kwa mantiki hiyo,kama refa wa kati hana utashi kwenye maamuzi basi ndio maana wasaidizi wake humpa taarifa tu kuwa hiyo ni offside au goli limeingia au halijaingia!
Ulishawahi kuona refa wa kati anaenda kwenye VAR kuangalia kama ni offside,hicho kitakuwa kichekesho!

Kwa wanaomlalamikia refa wa kati eti kwanini hakwenda kujiridhisha kwenye VAR kama mpira wa Azizi ki nadhani sasa mmeelewa!
Nimeshangaa viongozi wa Yanga katika barua yao ya malalamiko,wamemlalamikia refa wa kati kuacha kwenda kuangalia VAR kwenye mpira wa azizi Ki lakini refa huyo huyo akaenda kuangalia VAR kwenye tukio la Lomalisa la foul ili kujua ni kadi ya njano au nyekundu!

Ukisoma taratibu bila jazba utanielewa!

NB: Penalty;Hata kwa kutumia VAR,tukio moja linaweza kuamuliwa tofauti na marefa wawili tofauti!Kuna refa anaweza kusema hii ni penalty na refa mwingine akasema hiyo sio penalty,hiyo ndio maana ya utashi!

Offside:Kwa kutumia VAR,refa hana choice!Ikishachorwa ile mistari miwili ndio basi,refa hana choice!
Ndio maana Offside na goal,refa hupewa tu taarifa kupitia microphone!
Tumeelewana wakuu au nieleze zaidi?

Refa wa kati apewe maua yake,alichezesha ile mechi vizuri sana!View attachment 2957945
Kama siyo goli yanga walitakiwa wapewe kona
 
Umeelewa mada lakini?Umekurupuka,mimi sijazungumzia kama ni goli au sio goli!
Tuliza mihemko utaelewa nilichoandika!
W endio utulize mihemko, kama hujazungumzia kuwa goli ama sio goli huoni kama hujielewi.
 
Refa ameshaeleza kwanini alienda kuangalia faulu ya lomalisa kwenye var na kwanini hakuangalia marudio ya goli kwenye var Ila kwa sababu ile timu wenye akili ni wawili ndio maana unaona hayo malalamiko.
Kwanini haikuwa kona..!!???
 
Ilikuwa nini baada ya hapo?
Baada ya lile goli kwa mpira kudunda golini, mchezaji wa masandawana aliutoa mpira nje na kipa wao akaenda kuuchukua nje ya goal line. Baada ya mpira kusimama kwa muda, kwenye kuuanzisha, refa alimpa kipa apige kama vile aliudaka. Hili lilikuwa kosa jingine..!! Ndo hapo nakuuliza wewe bwana Bome-e, kwa vile mpira ulivuka goal nje ya goli, kwanini haikuwa kona?
 
Baada ya lile goli kwa mpira kudunda golini, mchezaji wa masandawana aliutoa mpira nje na kipa wao akaenda kuuchukua nje ya goal line. Baada ya mpira kusimama kwa muda, kwenye kuuanzisha, refa alimpa kipa apige kama vile aliudaka. Hili lilikuwa kosa jingine..!! Ndo hapo nakuuliza wewe bwana Bome-e, kwa vile mpira ulivuka goal nje ya goli, kwanini haikuwa kona?
Ingepigwa kona,moyo wako ungeridhika?Tuache hizi lialia,tujipange kwa michuano ijayo!
 
Ingepigwa kona,moyo wako ungeridhika?Tuache hizi lialia,tujipange kwa michuano ijayo!
Unatoka nje ya hoja sasa, au umeishiwa hoja..!!?? Suala si kuridhika au kutorishika kwangu, maana hata kama sijaridhika na nisichoridhika nacho ndiyo haki, hamna namna. Hii nimeiweka kukuonyesha kwamba refa alikuwa na lake moyoni ambalo linakinzana na haki..!!

BTW, kama umeishiwa hoja, kubaliana na wenye hoja..!! usilete habari za kuridhika au la..!! Hata mwizi akishindwa kuiba huwa haridhiki, lakini wizi si jambo la haki..!! Suala ni haki.
 
Unatoka nje ya hoja sasa, au umeishiwa hoja..!!?? Suala si kuridhika au kutorishika kwangu, maana hata kama sijaridhika na nisichoridhika nacho ndiyo haki, hamna namna. Hii nimeiweka kukuonyesha kwamba refa alikuwa na lake moyoni ambalo linakinzana na haki..!!

BTW, kama umeishiwa hoja, kubaliana na wenye hoja..!! usilete habari za kuridhika au la..!! Hata mwizi akishindwa kuiba huwa haridhiki, lakini wizi si jambo la haki..!! Suala ni haki.
Yaani unajaribu kuaminisha kwamba refa alikuwa na jambo lake na Yanga!Ingekuwa hivyo,angeweza kutoa red card kwa Lomalisa!Halafu aliyesema mpira haukuvuka mstari sio refa wa kati bali ni wasaidizi wake 3 ambao wako vyumba vya VAR!
Mechi ya Simba na Alahyl,kuna mchezaji wa simba alipiga mpira ukamgonga kichwani mpinzani na ukarudi kwenye possession ya Simba,refa akasimamisha mpira na akaenda kumuangalia mchezaji aliyeumia!Baada ya hapo refa akawapa mpira Alahyl waanzishe mpira!Hapo napo utasema refa alikula njama?
Tuache hizi lialia
 
Back
Top Bottom