Kwa uelewa wako,uwanjani Kuna marefa wangapi?Hao wengine wako kwa ajili gani?je,kila tukio tatanishi,refa wa Kati anapaswa kwenda kuamua mwenyewe?Je,uamuzi wa refa mmoja na uamuzi wa marefa watatu kwenye tukio moja,ni upi more likely to be correct?Kwa hiyo tuelewe kwamba kuidhinisha hili ni goli au siyo goli si kazi ya refa?
Hatimaye nimekutana na comment ya mtu anayeelewa mpira!Wanakaza mafuvu tuu
Tukio la offside au mpira kuvuka line, huamuliwa na teknolojia moja kwa moja refa yeye hupewa taarifa tuu na chumba cha VAR kuwa ni goli au sio goli
Matukio kama penati, faulu, mtu kunawa mpira, hayo yanahitaji utashi wa refa kuamua hivo kujiridhisha
Nimewashangaa sana Yanga na wachambuzi kulinganisha tukio la lomalisa na hilo la goli
Kama siyo goli yanga walitakiwa wapewe konaWakuu,kuna suala nimeliona kuanzia kwa mashabiki,wachambuzi na hata viongozi mbalimbali juu ya mechi ya Yanga vs Mamelods!
Lawama nimeona zikienda kwa refa wa kati kwa kuacha kwenda kuangalia VAR kuhusu mpira wa Aziz Ki lakini akaenda kuangalia foul ya Lomalisa kwenye VAR ili aangalie kama ilistahili kadi nyekundu au la!
Ndio hapo naona watu wanachanganya,wanashindwa kuelewa majukumu ya refa wa kati!Nitaeleza kwa ufupi na mwenye kuelewa ataelewa cha msingi usitangulize mihemko!
*Refa wa kati huwajibika kwenda kuangalia VAR pale ambako kuna tukio la utata ambapo ataenda kujiridhisha!Matukio haya ni yale ambayo yeye kama refa wa kati ana uwezo wa kuamua kwa utashi wake!Mfano matukio ya penalty na foul,mambo hayo hutegemea utashi wa refa!Refa anaweza kuamua iwe penalty au isiwe penalty,anaweza akaamua iwe kadi ya njano au nyekundu!Hapo VAR haimwambii kuwa atoe kadi ya njano au nyekundu bali anatumia utashi wake kwa kuzingatia kanuni za mpira wa miguu!VAR haimwambii refa wa kati atoe penalty au asitoe,ni utashi wake kulingana na kile anachokiona!
*Sehemu ya pili ni matukio ya utata ambayo refa wa kati hana utashi nayo!Matukio haya ni kama Offside na mpira kuvuka mstari wa goli!Matukio haya huamuliwa na VAR moja kwa moja!Kwa mantiki hiyo,kama refa wa kati hana utashi kwenye maamuzi basi ndio maana wasaidizi wake humpa taarifa tu kuwa hiyo ni offside au goli limeingia au halijaingia!
Ulishawahi kuona refa wa kati anaenda kwenye VAR kuangalia kama ni offside,hicho kitakuwa kichekesho!
Kwa wanaomlalamikia refa wa kati eti kwanini hakwenda kujiridhisha kwenye VAR kama mpira wa Azizi ki nadhani sasa mmeelewa!
Nimeshangaa viongozi wa Yanga katika barua yao ya malalamiko,wamemlalamikia refa wa kati kuacha kwenda kuangalia VAR kwenye mpira wa azizi Ki lakini refa huyo huyo akaenda kuangalia VAR kwenye tukio la Lomalisa la foul ili kujua ni kadi ya njano au nyekundu!
Ukisoma taratibu bila jazba utanielewa!
NB: Penalty;Hata kwa kutumia VAR,tukio moja linaweza kuamuliwa tofauti na marefa wawili tofauti!Kuna refa anaweza kusema hii ni penalty na refa mwingine akasema hiyo sio penalty,hiyo ndio maana ya utashi!
Offside:Kwa kutumia VAR,refa hana choice!Ikishachorwa ile mistari miwili ndio basi,refa hana choice!
Ndio maana Offside na goal,refa hupewa tu taarifa kupitia microphone!
Tumeelewana wakuu au nieleze zaidi?
Refa wa kati apewe maua yake,alichezesha ile mechi vizuri sana!View attachment 2957945
W endio utulize mihemko, kama hujazungumzia kuwa goli ama sio goli huoni kama hujielewi.Umeelewa mada lakini?Umekurupuka,mimi sijazungumzia kama ni goli au sio goli!
Tuliza mihemko utaelewa nilichoandika!
Kwanini haikuwa kona..!!???Refa ameshaeleza kwanini alienda kuangalia faulu ya lomalisa kwenye var na kwanini hakuangalia marudio ya goli kwenye var Ila kwa sababu ile timu wenye akili ni wawili ndio maana unaona hayo malalamiko.
Baada ya lile goli kwa mpira kudunda golini, mchezaji wa masandawana aliutoa mpira nje na kipa wao akaenda kuuchukua nje ya goal line. Baada ya mpira kusimama kwa muda, kwenye kuuanzisha, refa alimpa kipa apige kama vile aliudaka. Hili lilikuwa kosa jingine..!! Ndo hapo nakuuliza wewe bwana Bome-e, kwa vile mpira ulivuka goal nje ya goli, kwanini haikuwa kona?Ilikuwa nini baada ya hapo?
Ingepigwa kona,moyo wako ungeridhika?Tuache hizi lialia,tujipange kwa michuano ijayo!Baada ya lile goli kwa mpira kudunda golini, mchezaji wa masandawana aliutoa mpira nje na kipa wao akaenda kuuchukua nje ya goal line. Baada ya mpira kusimama kwa muda, kwenye kuuanzisha, refa alimpa kipa apige kama vile aliudaka. Hili lilikuwa kosa jingine..!! Ndo hapo nakuuliza wewe bwana Bome-e, kwa vile mpira ulivuka goal nje ya goli, kwanini haikuwa kona?
Unatoka nje ya hoja sasa, au umeishiwa hoja..!!?? Suala si kuridhika au kutorishika kwangu, maana hata kama sijaridhika na nisichoridhika nacho ndiyo haki, hamna namna. Hii nimeiweka kukuonyesha kwamba refa alikuwa na lake moyoni ambalo linakinzana na haki..!!Ingepigwa kona,moyo wako ungeridhika?Tuache hizi lialia,tujipange kwa michuano ijayo!
Yaani unajaribu kuaminisha kwamba refa alikuwa na jambo lake na Yanga!Ingekuwa hivyo,angeweza kutoa red card kwa Lomalisa!Halafu aliyesema mpira haukuvuka mstari sio refa wa kati bali ni wasaidizi wake 3 ambao wako vyumba vya VAR!Unatoka nje ya hoja sasa, au umeishiwa hoja..!!?? Suala si kuridhika au kutorishika kwangu, maana hata kama sijaridhika na nisichoridhika nacho ndiyo haki, hamna namna. Hii nimeiweka kukuonyesha kwamba refa alikuwa na lake moyoni ambalo linakinzana na haki..!!
BTW, kama umeishiwa hoja, kubaliana na wenye hoja..!! usilete habari za kuridhika au la..!! Hata mwizi akishindwa kuiba huwa haridhiki, lakini wizi si jambo la haki..!! Suala ni haki.
Tunajaribu kuangalia tukio halisi na yaliyojiri baadae ya tukio, scenario and possible argumentsIngewekwa kona,malalamiko yako yangeisha?
Nani atakayetoa suluhu baadae ya mjadalaTukubaliane na jambo moja kwanza kabla ya kurukia jambo lingine!