Kama umeajiriwa sehemu yoyote shika sana kazi yako hakikisha huipotezi, ukiipoteza utajuta

Kama umeajiriwa sehemu yoyote shika sana kazi yako hakikisha huipotezi, ukiipoteza utajuta

OMOYOGWANE

JF-Expert Member
Joined
Dec 30, 2016
Posts
4,701
Reaction score
11,920
Habari wakuu!!

Huu ni ushauri kwa watu wote waliopo kwenye ajira sehemu mbali mbali serikalini au makampuni binafsi n.k,

Haiijarishi wewe ni polisi, mwanajeshi, Mwalimu, daktari, mhasibu, sekretari, mwandishi wa habari, kiongozi wa kisiasa, Modetator JF n.k hata kama unalipwa elfu moja kwa siku, heshimu sana kazi yako na ipende kama unavyompenda mke wako au watoto wako.

Siku ukipoteza hiyo kazi sio ajabu kujikuta unapoteza na vitu vingine vya muhimu kama vile mke, heshima, marafiki ndugu hata biashara uliyoamua kuianzisha nayo ikafa kifo cha mende,

Hakuna watu wanafiki kama walio maofisini, hakikisha hupotezi kazi baki huko huko na wanafiki wenzio maana siku utakapopoteza kazi hakuna atakayehangaika na wewe hapo ofisini kwako ulipo sasa ama huko utakakokuwa unapereka vyeti na CV zako narudia tena hakuna atakayehangaika na wewe,

Siku ukitaka kujitolea watapokea CV zako ulizotype na kuprint kwa pesa ya msaada kama umezipeleka private watakuambia watakupigia simu na hiyo ndio bye bye, kama ni serikalini hayupo Mkurugenzi, au mkuu yeyote atakayehangaika na makaratasi yako yatawekwa kwenye faili yaungane na barua za wenzako za mwaka juzi ambazo hazijajibiwa,

Haijarishi unalipwa laki moja au mbili kwa mwezi, haijarishi unalipwa mamilioni, haijarishi unatembea kwenye gari zuri la serikali au kampuni, nguvu uliyonayo sasa ndiyo inayokufanya uheshimike na kuchangamkiwa unapokwenda kikazi kwenye taasisi zingine,


Wasio na kazi au ajira hawajapenda au kutaka wawe hivo bali ni competition kali iliyopo mitaani

Kijana kama wewe ni boda boda umeoa unawatoto na unarisha familia heshimu sana hiyo kazi

Mwenye macho na asome kisha atafakari

Nawasilisha.
 
Kazi nyingi za kuajiriwa siku ukiipoteza haupotezi kazi peke yake ila inapoteza na marafiki wote uliokutana nao kazini
Waheshimu sana marafiki uliokua nao kabla hujapata kazi usiwatenge hata baada ya kupata kazi kwakua wale ndio marafiki wa kweli siku ukiipoteza kazi utarudi kuwatafuta tu , na wale marafiki uliokutana nao kazini watakua wanakukwepa hata ukikutana nao njian na ukiwapigia simu hawatapokea au wakipokea stori inakua na mkatomkato anajua utampiga kizinga hata cha 10k au kumlilia njaa
 
Natarajia kuacha kazi ninayolipwa wastani wa 3300 kwa siku huku nikitegemea hiyo ndio Pesa ya kula, kodi, familia n.k.. Unanishaurije mkuu?
Pata kazi kwingine kwanza na hakikisha mmesainishana mikataba ndio uache hiyo kazi vinginevyo utapeleka watoto wakaishi kwa bibi yao kijijini
 
Ukweli mtupu,
Hawa walioajiriwa, ujanja na kutembea mbele ni kutokana na ajira walizo nazo, wakizipoteza, wanakuwa kama vichaa Bora hata sie ambao hatujawahi kuzipata hizo ajira, tumeishazoea maisha yetu ya kitaa, shahada na vyeti kapuni, tunapiga boda boda tu
 
Kazi nyingi za kuajiriwa siku ukiipoteza haupotezi kazi peke yake ila inapoteza na marafiki wote uliokutana nao kazini
Waheshimu sana marafiki uliokua nao kabla hujapata kazi usiwatenge hata baada ya kupata kazi kwakua wale ndo marafiki wa kweli siku ukiipoteza kaz utarud kuwatafuta tu , na wale marafik uliokutana nao kazin watakua wanakukwepa hata ukikutana nao njian na ukiwapigia sim hawatapokea au wakipokea stori inakua na mkatomkato anajua utampiga kizinga hata cha 10k au kumlilia njaa
kazini hakunaga marafiki, kuna wanafiki

put it in your mind
 
Kazi nzuri. Nikiona watu wa Dar wanaamka saa 10 za usiku kwenda kazini. Wanarudi nyumbani saa 4 za usiku. Mshahara laki 210,00 net pay. Kodi, ada za watoto, matibabu, chakula, wazazi wa mke wanaumwa wote wamekuja kutibiwa hapo kwako.
Unajiuliza nilimkosea nini Mungu, hupati jibu.
 
Back
Top Bottom