Kama umeajiriwa sehemu yoyote shika sana kazi yako hakikisha huipotezi, ukiipoteza utajuta

Very very true mkuu....kwa mwenye Akili sahv Maisha yanazidi kuwa marahisi ....
 
Hakuna Kitu huwa nachukia kwenye ajira Kama kunyenyekea, kujipendekeza na unafiki.


Mpo kwenye weekly au monthly meetings mbaba au mmama mzima anajipendekeza kwa bosi utadhani litoto
Hahaaahaa[emoji16][emoji16][emoji16]
 
Huwezi kuwa mfanyakazi bila kuwa mtumwa
inategemea ndugu acha watu wafikie malengo kwa kupitia magumu! kuacha kazi na kuangaika kutafuta nyingne ni moja ya mapitio ya ugumu au mafanikio ya moja kwa moja! ukufanya kazi na utumwa vinashabiana japo si maana halisi..
 
Kwan mnakuaga hamuweki akiba
Swali zuri sana hili, nimefukuzwa kazi tangu may lakini mke wangu na watoto wangu wanakula vizuri tuu, hata kama mshahara ni 350k still unaweza ukaweka 75k kila mwezi kazi yako ukifanya miaka miwili minimum, trust me utakula, utakunywa na hela ya sadaka kila jumapili utakuwa nayo hata kama ukose kazi mwaka mzima, ni maamuzi tuu
 
Ticha sijaelewa asee
 
Sahihi mkuu
 
Huo Ni uoga mkubwa na kushindwa kuwaza nje ya box.

Huu ni ushauri kwa watu wote waliopo kwenye ajira sehemu mbali mbali serikalini au makampuni binafsi n.k,

Haiijarishi wewe ni polisi, mwanajeshi, Mwalimu, daktari, mhasibu, sekretari, mwandishi wa habari, kiongozi wa kisiasa, Modetator JF n.k hata kama unalipwa elfu moja kwa siku, heshimu sana kazi yako na ipende kama unavyompenda mke wako au watoto wako.

Siku ukipoteza hiyo kazi sio ajabu kujikuta unapoteza na vitu vingine vya muhimu kama vile mke, heshima, marafiki ndugu hata biashara uliyoamua kuianzisha nayo ikafa kifo cha mende,

Hakuna watu wanafiki kama walio maofisini, hakikisha hupotezi kazi baki huko huko na wanafiki wenzio maana siku utakapopoteza kazi hakuna atakayehangaika na wewe hapo ofisini kwako ulipo sasa ama huko utakakokuwa unapereka vyeti na CV zako narudia tena hakuna atakayehangaika na wewe,

Siku ukitaka kujitolea watapokea CV zako ulizotype na kuprint kwa pesa ya msaada kama umezipeleka private watakuambia watakupigia simu na hiyo ndio bye bye, kama ni serikalini hayupo Mkurugenzi, au mkuu yeyote atakayehangaika na makaratasi yako yatawekwa kwenye faili yaungane na barua za wenzako za mwaka juzi ambazo hazijajibiwa,

Haijarishi unalipwa laki moja au mbili kwa mwezi, haijarishi unalipwa mamilioni, haijarishi unatembea kwenye gari zuri la serikali au kampuni, nguvu uliyonayo sasa ndiyo inayokufanya uheshimike na kuchangamkiwa unapokwenda kikazi kwenye taasisi zingine,


Wasio na kazi au ajira hawajapenda au kutaka wawe hivo bali ni competition kali iliyopo mitaani

Kijana kama wewe ni boda boda umeoa unawatoto na unarisha familia heshimu sana hiyo kazi

Mwenye macho na asome kisha atafakari

Nawasilisha.

[/QUOTE]
 
.
Mkuu inaonesha wazi wazi unayaogopa sana maisha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…