Kuna jamaa yangu nilikuwa nae Chuoni yeye kazi yake kubwa ilikuwa kuiba Glass za wine na bia Bar/Pub na hii tabia hajaiacha mpaka leo japokuwa kashaoa na watoto anao. Pia alikuwa na tabia ya kuwasafisha mikoba,hereni,cheni,hela na saa mademu aliolala nao Guest.
Hivi karibuni tuu kuna demu alimpata akaenda kulala nae Hotelini yule demu akapanda dau kubwa akampa elfu themanini kabla hawajafanya lolote,demu kazitia kwenye mkoba wake jamaa alichofanya akavizia mida ya saa10 usiku demu kalala fofofo jamaa akazama kwenye handbag akachukua hela zote alizozikuta pamoja na za yule demu akasepa zake. Demu anaamka hakuti mtu kucheki pochi haina hata mia,demu akapiga sana simu jamaa hakupokea.