Kama umewahi kuiba Guest house /Hotelini karibu utuambie uliiba nini na ulitumia mbinu gani?

Nakumbuka wakati nafanya kazi hotel flani (sihitaji jina kuna watu watanichomea humu), nilianzisha uhusiano na mmojawapo wa store keeper wa hapo hotelini.
Ilikuwa ni mwendo wa kubeba vilotion, vimswaki, vitaulo, vile vindala vya manyonya, sabuni, cable za umeme na vingine vinavyoingia kwenye pochi.

Kumbe hawa wafanyakazi wa muda mrefu katika maeneo yenye ulinzi wa kutumia camera, huwa wanajua muda ambao waangalizi wa camera wanakuwa wamesinzia, hivyo kupelekea kudokoa vitu kiurahisi.
Alikuwa akiniambia, muda flani tutaenda store ya hotel maana muhindi yule atakuwa anasinzia mbele ya screen muda huo.
Na hatukuwahi kushikwa.

Tulikuwa tunabeba sana vyakula vibichi au vilivyopikwa ndani ya kofia zetu za jikoni pale hotelini, keki, nyama, kuku, sambusa, sauce ndogondogo za chupa, chillies, tomato, samaki, toothpicks, pastes, tambi, vikopo vya masala, kahawa na vimaziwa vya pakti n.k
Sema ma-Chef wakuu wanakuwa wanoko hivyo akitoka tu, tumebeba.
Wapishi tunaiba sana vyakula na vidude vidogovidogo.
Nimefanya kazi hotel 3, nimekutana na tabia hizohizo.

Baadae nahisi walishtuka na kuanzisha utaratibu wa kuvua kofia na kuziacha jikoni wakati wa kuondoka nyumbani.
Ila nilikuwa najaza kifriji changu pasu kwa pasu na hotel ile.

Naenda bar naagiza glasi 3, moja ya bia ninayokunywa, moja ya maji na moja ya pombe kali.
Nabeba mbili naacha moja.
Nafanya hivi endapo muhudumu akinizingua.

Nilikuwa najiuliza, laiti ningekuwa nafanya kazi benki, sijui muda huu ningekuwa selo ipi!!!
Maisha yale sijui yalikuwaje.
ILA NOW NIMEACHA JAMANI, MSINIOGOPE!!!!!
 
Mi zaman sana kabla sijajitambua vizur nkiwa o level nlikuwa naiba sana vikopo vya kuwekea chumvi na opener pia zile sabuni za maji zilizopo chooni
 
Ha ha
 
nimecheka mno hii mada,mimi lazima sabuni.lotions,shampoo niondoke nazo!! looo huu sio uungwana
 
s
siku moja nililala hoteli moja Songea.. Asub nikaws nahitaji pasi ili ninyooshe nguo zangu.. nikaambiwa kuna mteja aliiba jana yake.. kwa hiyo hawanunua nyingine..
siku nyingine nikiwa Dar hotel fulan zilizopo nyuma ya Ubungo.. kufika muda wa kulala nashangaa chumba hakina neti.. nilivyowaambia reception wakaw hawaamini..
baadae walivyokuja chumban wakawa wanasema itakuw yule dada alielala hapa ameiiba..
haya mambo yapo sana
 
mhh roho za kimaskini ndio zinafanya watu waibe vitu vidogo visivyo na tija...... Ibeni vitu vya maana kama umeamua kuwa mwizi
 
Yaani ni hali tu unajikuta unayo.
Mpaka leo nikienda kunywa pale 4Ways opposite na Governor hawanipi glass za udongo.
Nikiagiza beer napewa glasi za plastic za Castle.

Ndani nina full set ya vyombo vya 'Mchanga mweupe wa hotel"
Kuanzia uma, vijiko, visu, sahani, vibakuli mpaka glass na serving bowls.
Sema ubaya wake vina chata za hotel.
Huwa walikuwa wakiagiza, zinawekwa chata za hotel kabisa, kisha maboksi yanahifadhiwa stoo ya vyombo.
Sema kwa kuwa niliwahi kufanya kazi pale, nikiulizwa huwa nawajibu kuwa walinipa zawadi.....kumbe siri naijua mimi na malaika wangu anayenilinda....!!!!
 
Kuna siku nilicheka sana, nipo guest nikaenda uwani kufika nakutana na jamaa anang'ang'ania kutoa vile vioo vya chooni eti akipasue, nikamuuliza broo vip ? Akasema kalipia guest demu kagoma kuja kwaio kupunguza ni kuwatia hasara wenye guest.
 
ha haha vizuri kwa kuacha
 
Kuna siku nilicheka sana, nipo guest nikaenda uwani kufika nakutana na jamaa anang'ang'ania kutoa vile vioo vya chooni eti akipasue, nikamuuliza broo vip ? Akasema kalipia guest demu kagoma kuja kwaio kupunguza ni kuwatia hasara wenye guest.
ha hahaha si angelala tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…