Kama umewahi kushuhudia live nguvu za giza pita hapa uweke ushuhuda wako

B sekondary, wilaya E, mkoa wa K.... Ni woga au?
 
Uwiii lazima ningelipiza tu, liwe jua iwe mvua...
 
Mchawi kawazawadia kila mtu kitunguu akamwonyeshe mkewe...
 
Toa full story
 
Ulikosea nn
 
Mambo ya giza yanaikumba jamii kwa kasi kikubwa ni kushikia imani za dini zetu kwa nguvu.
 
Da
 
Supu ilibadilika Radha baada ya mbibi kuinyooshea kidole,
Aisee uchawi upo ndg zangu nilinunua supu ikiwa na Radha yake nzuri kabisa lakini baada ya kuja bb ambaye yeye mwenyewe alikuwa anauza supu jirani na pale niliponunua, akanikuta nakunywa Ile supu ghafla nikamuona kama kanyoosha kakidore kwenye Ile bakuri ya supu ghafla Radha ilipotea nikawa nakunywa kama maji, jamani nani asiyeamini uchawi.
 
Miaka ya nyuma nilienda Mafia Island kwa Babu yangu.
Basi nilienda na Redio ya kuchaji kwa kuzungusha kama unapandisha Kioo ktk Gali kubwa.yaani unapo zungusha ndio linajichaji nazani ushapata picha.
Basi ikawa nikilala Usiku naliwasha kwa sauti kubwa mwenyewe nalala.
Kumbe kuna wazee majilani walikua nawakera Usiku, Wakamwambia Babu asubuhi.
Babu akanielezea alichoambiwa na Wazee wenzake,nikaacha kuweka sauti kubwa nikapunguza sauti.
Ikapita siku kama tatu hivi nikakutana na Bibi mmoja njiani nilivyo msalimia akaitikia alafu akaniuliza wewe ndie unatupigia kelele usiku na Redio yako eee?.
Mzee nikauchuna kimya basi nikaacha kabisa kuwasha Usiku.
Ikapita siku kazaa Mzee nikajisahau nikarudia tena ujinga wangu wa kuwasha Redio tena kwa sauti kubwa nakula zangu ladha za Bongo.
Nilivyo kuja kustuka saa 9 usiku Redio imepunguzwa sauti yaani ule mziki unapigwa lakini mwimbaji kama sauti imemkauka,nikapotezea nikazima nikilala zangu.
Asubuhi nikachaji Redio yangu basi kila nikibadili Station Mtangazaji sauti imemkauka,nikaweka Kanda za kaseti vilevile .
Ikabidi niipeleke kwa fundi, fundi akaniambia Spika mbovu akaibadilisha ngoma vilevile .
Nikamfuata Babu nikamuelezea yaliyo tokea akasema wale wazee washafanya yao. Basi nikarudi zangu Dar na redio yangu na haikupona tena. Licha ya kufanya juhudi ya kuangaika kwa mafundi
 
hapo ni hata sijakusoma mkuu!!

yaan mwaka 1992 ndio ushuhuda wako wa kwanza ukiwa unafundisha shule X

halafu ushuhuda wako wa mwisho ni mwaka 2009 ukiwa field liwale wakati huo inasoma chuo cha sauti mtwara

hoja yangu sasa, yaani ulianza kufundisha kabla haujawa mwl?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…