Nawasilisha kama ilivyosimuliwa :
Kuna mwalimu Shule X, huko kanda ya ziwa, aliamka saa tisa usiku kuwahi usafiri asubiri gari kwenda mjini, kijiji cha ndani huko mkoa mpya uliopo ziwani.
Akasubiri gari na baada ya mda likaja, akasimamisha na kuingia. Gari ikaondoka, kakaa baada ya mda kumcheki abiria mwenzake kainama, akahisi labda ni usingz, lakini alipocheki waliopo nyuma pia dizaini kila mtu kainama. Akaona isiwe shida akamsemesha jamaa kainama tu kwa siti yake.
Sasa na yeye akatulia, gari imeenda lakini ghfla kama kausingz kakamwingia, akshtuka ghafla ni saa kumi na mbili asubuh na amesimama pale pale alipokuwa saa tisa kituoni.
Akapanic, kachukua baiskeli hadi wilayani hakurudi tena, ikabidi afisa elimu aende kule na timu yake kuongea na waalimu na wananchi ila jamaa hakuweza kukubali kurudi kituoni. In short walimpa uhamisho.
Nyingine mwalimu kapangiwa kituo Shule X huko kanda ya nyonyo. Kama ujuavyo vita ya kugombea mwalim binti mpya kati ya wanakijiji na wafanyakazi wenzake. Kumbe akawa kawakatalia, ikawa nongwa!
Siku moja anaosha ndizi kamaliza vizuri kwa sufuria, ghafla kikashuka kinyesi kingi kika replace ndizi zote, kinyesi fresh kinatoa hadi Moshi. Madam yule alikimbia kwenda kwa Bro nae ni mwalimu jirani Yake. Hakurudi tena kwa ile nyumba anaogopa.
Nina visa kama 10 kidogo ila mzembe kuhadithia.
Haya Mambo yapo kanda ya Nyonyo hasa kwa tuliokulia Bush huwa hata hatutetereki.
Sent using
Jamii Forums mobile app