Kama umewahi kushuhudia live nguvu za giza pita hapa uweke ushuhuda wako

Kama umewahi kushuhudia live nguvu za giza pita hapa uweke ushuhuda wako

Hatari sana
FB_IMG_1577214597861.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yuko dogo mmoja alikua anasoma B sekondary. Alikua anamchukua mke wa mtu. Mtu mwenyewe alikua nje ya nchi kimasomo. Ndugu zake msomi hawakupendezewa shemeji Yao aliwe na student. Kuna siku dogo wakapanga na bibie wakapeane penzi kwenye minazi. Enzi hizo gesti wanaingia wenye pesa zao.

Dogo alikua dent hana pesa. Basi kweli muda kufika mke akafika na mechi ikaanza bila refa. Dogo akapakua mzigo kufika kileleni utamu Ulipozidi ni kawaida mtu kufunga macho. Basi dogo wakati anafyatua risasi alimkumbatia mke wa mtu kisawasawa huku amefunga macho. Ile kumaliza na kufumbua macho akajikuta alikua anafanya mapenzi na kisiki cha mnazi na sio mtu. Dogo kutoka pale hakurudi shuleni. Alipanda basi la Dar na kuacha shule. Sidhani kama alisharudi wilaya ya B.
 
Uzi una wakongwe huu..

Kuna vijana wawili walipiga paka wa ostadhi mmoja hivi..mwenye paka akapata taarifa akawaambia waombe msamaha..kijana mmoja alikubali mmoja akagoma..yule aliyegoma alianza kutokwa na majipu mwilini wazazi wake wakamsihi akaombe msamaha lakini bado aligoma..kilichomkuta ni kupoteza maisha...yule mzee ni mchawi akikutaka uwe mpenzi wake ni dk 0 tu..

Tukio lingine Kuna kijana alijisaidia kubwa nyuma ya nyumba ya huyo mzee ostadhi alivyofika kwake akakuta ile kubwa ipo kitandani kwake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Miaka 6 iliyopita Kuna rafiki alikwenda kijijini kwa Bibi yake kusalimia..alivyofika kijijini akatembea na Mume wa mtu...mke wa mwenye Mume akamlogezea ukimwi.

Rafiki alianza kuumwa ilibidi aletwe dar kwa vipimo zaidi ..kila akipimwa hakuna kitu na hali inazidi kuwa mbaya..na uumwaji wake ni ule ule wa wagonjwa wa ukimwi..hali ikazidi kuwa mbaya hadi kufikia kuwa mtu wa kitandani tu..Mama yake mdogo akajiongeza akamleta mtaalam akaweka kambi nyumbani kwao week mbili..week ya tatu rafiki mzima hakuwa na hata dalili Kama alitoka kuumwa ule ugonjwa...uchawi upo jamani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom