Kama umeweza kupunguza stress zako bila kilevi tusaidie mbinu uliyoitumia

Kama umeweza kupunguza stress zako bila kilevi tusaidie mbinu uliyoitumia

gearbox

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2024
Posts
563
Reaction score
1,768
  • Umeshindwa kulipa deni, benki wanakuja kuchukua nyumba
  • Magonjwa yasiyo na tiba unasubiri kifo
  • Kufilisika na huna ujuzi wala mtaji
  • Kugundua watoto sio wako
  • kuingia 18 za vyombo vya dola,
  • N.k.

Wengi kimbilio la kupunguza stress huwa ni pombe, ngono, bangi, madawa, n.k. na mwishowe huwa waraibu

Kama umeweza kudeal na stress bila kilevi weka hapa mbinu
 
Stress za kawaida unaweza kusikiliza muziki, kucheki series, n.k. lakini hizi stress nzito zimefanya wengi kutumia vilevi

Wengi kimbilio la kupunguza stress huwa ni pombe, nyapu, bangi, madawa, n.k. na mwishowe tunapata tatizo la ziada "addiction"

kama umeweza kudeal na stress bila kilevi weka hapa mbinu
Weka mziki, hardcore hip hop. Alaf kwenye screen cheza FIFA.
 
Music unatatua matatizo yangu mengi ya stress
Kuna Muda inakuwa down sana kwa stress, nikisikiliza amapiano zangu kadhaa ninazozipenda, nakaa sawa!
 
Muwe mnawakumbuka wazazi kama wapo hai
Safari za mara kwa mara au kuongea nao na kupata Baraka zao ni tiba tosha
Hapo kama ni stress sio mbaya sana
Ila depression ndio mbaya zaidi na omba isiwapate

Hiyo ndio mbaya sana na kama unaongelea hiyo basi ni kuwa karibu na ndugu au hata holiday na rafiki inasaidia sana
Ila ulevi hautibu msongo wa mawazo bali unaongeza tu
 
Stress za kawaida unaweza kuzikandamiza kwa kusikiliza muziki, kucheki series, n.k. lakini stress nzito ni ishu nyingine

Wengi kimbilio la kupunguza stress huwa ni pombe, nyapu, bangi, madawa, n.k. na mwishowe tunapata tatizo la ziada "addiction"

kama umeweza kudeal na stress bila kilevi weka hapa mbinu
nilishawahi kupitia kipindi kigumu sana maishani mwangu, chenye stress hadi nilikuwa naongea peke yangu, wengi walijua nataka kuchanganyikiwa. shida nyingi kila kona na unachekwa hakuna wa kukusaidia. hii ilikuwa kati ya 2007 hadi 2011. Niliamua kumgeukia Mungu, hapo ndipo nilipoamini Neno la Mungu linavyosema kwamba Yesu Kristo ni mfalme wa amani, nilipata amani ya ajabu, isiyoelezeka, amani yenye furaha, amani isiyo ya kipimo hata kueleza hapa siwezi, ataiujua tu yule atakayeipata.

amani ambayo hata kama nilikuwa sina pesa, nilikua na amani na ninabubujiko la Mungu moyoni, kumbe baada ya kugeukia kwa Mungu kwa kuokoka kwa kweli ndipo Mungu akaanza kunitengeneza polepole, kunipa fadhila polepole, hadi nikasimama, nikajijenga, nimebaki tu namtukuza Mungu maishani.

hiyo ni amani ambayo ulimwengu huu hauwezi kuitoa. pome haiwezi kutoa amani kama ile, pesa haziwezi kutoa amani kama ile, mwanamke hawezi kukupa amani kama ile, nayo ndiyo ninayoipambania mara kwa mara, ikipotea huwa namtafuta Mungu hadi inarudi.

YOHANA 14:27 INASEMA: Amani nawaachieni; amani yangu nawapa; niwapavyo mimi sivyo kama ulimwengu utoavyo. Msifadhaike mioyoni mwenu, wala msiwe na woga

ISAYA 9:6 INASEMA;
Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume;
Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake,
Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani.

USHAURI; ukipita kipindi kigumu, chenye stress na depression, labda kwasababu ya uhaba wa kipato, magonjwa, ugomvi mbalimbali, kuachwa au chochote, TAFUTA AMANI KWA YESU. mpe Yesu maisha yako kwa kuokoka na ujiunge na waliookoka kama wewe. usikatishwe tamaa na wale wanaosema wameokoka ila wanatenda dhambi, hayo ni madhaifu ya dunia, ambatana na wenye nia moja na wewe. Yesu atakupa amani ya kweli. usitafute amani kwa waganga, pombe au wanawake, utapotea mazima. na ukienda kwa Yesu, hatakutupa nje kamwe.

Yohana 6:35 - 37 inasema: Yesu akawaambia, Mimi ndimi chakula cha uzima; yeye ajaye kwangu hataona njaa kabisa, naye aniaminiye hataona kiu kamwe. 36 Lakini naliwaambia ya kwamba mmeniona wala hamwamini. 37 Wote anipao Baba watakuja kwangu; wala ye yote ajaye kwangu sitamtupa nje kamwe.
 
  • madeni makubwa kuzidi uwezo wako,
  • magonjwa yasiyo na tiba unasubiri kifo
  • kufilisika
  • kugundua watoto sio wako
  • kuingia 18 za vyombo vya dola,
  • n.k.

Wengi kimbilio la kupunguza stress huwa ni pombe, ngono, bangi, madawa, n.k. na mwishowe tunapata tatizo la ziada "addiction"

kama umeweza kudeal na stress bila kilevi weka hapa mbinu
Huwa nasali naongea na Mungu sijawahi kutumia kilevi chochote.
 
Back
Top Bottom