Kama una mpango wa kuja South, zingatia mambo haya sita kabla ya kuanza safari yako

Kama una mpango wa kuja South, zingatia mambo haya sita kabla ya kuanza safari yako

Jamaa ni mshamba sana. Kuna wabongo hatari wapo hadi kwenye systems za nchi jirani wanakula na wakuu wa huko. Wengine hadi NIDA za huko wanazo hawasumbuliwi.
Tuelekezane tu wazee mtufumbue macho msituite washamba bhana ingawaje hatujui kitu...
RPC wa Hwange hapo Zimbabwe ni Mtanzania na anajivunia utanzania wake na anajulikana kama Mtanzania mdogo wake yupo SA jeshini...
 
Sio kweli ulichoongea mtu yeyote mwepesi kujua lugha atajua tu hata akijua lugha ingine..
Kweli mkuu, kujua lugha nyingine ni kichwa tu na kujituma. Kuna mtu anajua lugha zaidi ya nne. Na zote amejifunzia ugenini. Kuna wabongo wanaongea kiganda, kirundi, lingala, shangani, shona nk.

Nina mwana wa kitaa bongo, tena mzaramo pure lkn anachapa kichewa mpaka Passport ya Malawi alipata.
 
Habari zenu wanaJF wenzangu, ama baada ya salam ningependa kuendelea na mada yangu hapo chini.

Nianze kwa kusema kuwa dunia ina mengi, na kamwe hauwezi kuyajua kama haujaambiwa au kuyaona. Ndio maana waswahili wanamsemo wao unaosema "tembea uyaone". Hii haimaanishi kwamba utembee uyaone magorofa, magari au barabara, bali uone mambo mapya ambayo hapo kabla ya kutembea ulikuwa haujawahi kuyaona au kuyasikia popote.

Sasa leo ningependa nije na mada inayowatahadharisha ndugu zangu wabongo, ili kuwafungua macho na akili ya kujua yale ambayo hapo kabla walikuwa hawajayajua kuhusu South Africa, Dzonga, Afrika borwa, Afrika kusini, bondeni, Kaburu na kila jina linalotambulisha taifa hili.

Ni mambo sita tu ambayo ningependa kukutahadharisha nayo, uyazingatie kabla ya safari. Ila kama kuna mengine ya kuongezea basi wenzangu ambao wako humu pia wataongezea mengine katika comment. Na uzi wangu wa leo unajikita katika mambo yaliopo ndani ya mipaka ya South tu. Kuhusu changamoto zingine za njiani kabla ya kufika South nk, hizo sintozizungumzia kwa sasa. Maana thread za changamoto hizo zipo nyingi na mimi nishawahi kuandika moja.

Tuendelee hapo chini na yale unayotakiwa kuzingatia.

1. Hakikisha una document zote muhimu zinazohitajika safarini. Na kama uliambiwa kuwa gharama ya safari ni laki tatu, basi uandae angalau laki nne, ili moja uiweke pembeni itakusadia mbele ya safari. Kumbuka kuna dharura njiani, dola au rand kupanda nk.

2. Wakati unapanga safari, jitahidi kwanza ujue kingereza. Na kama una kichwa kizito cha kujifunza ngeli, basi upambane ujue hata salam, kuomba kitu au kuaga. South ni nchi inayoongea lugha 11. Ambapo lugha 9 ni za wenyeji na 2 za wazungu. Lakini lugha ya taifa na ambayo inapewa kipaumbele zaidi ni English.

Sasa ukijua English, hata kama hauna elimu ya maaana, uwezekano wa kupata kazi ni mkubwa ukilinganisha na wale ambao hawajui English. Ndomaana wazimbabwe wamedhibiti kazi nyingi na haswa zinazomilikiwa na wazungu, maana wao English kwao ni kama maji na mtungi, halafu wanaongea British safi kuliko waafrika wengine. Kutokujua English kumewanyima watu wengi (haswa kutoka bongo) fursa za kazi, hivyo kusababisha wengine kuamua kufanya deal hatari, halali na zisizo halali ili mradi mtu aishi.

3. Kabla ya kuanza safari hakikisha una address au contacts za wenyeji wako zaidi ya mmoja. Nchi hii kuna watu wengi wameuwawa, wameibiwa, wamekamatwa na kurudishwa nyumbani kwa sababu ya kukimbiwa au kuzimiwa simu na wenyeji wao kabla ya kuingia au baada ya kuingia South. Na hii sio kwa wabongo tu, bali ni nchi zote za East Africa watu wana tabia za kuwaingiza maboya ndugu, jamaa na marafiki zao kwamba waje tu watawapokea na kuwafanyia mpango wa kuishi, lakini ndugu, jamaa au marafiki hao wanapoingia tu mwenyeji huzima simu, hubadili namba nk. Hivyo ukiwa na address au namba za sim zaidi ya 3, itakusaidia ku deal na mwingine baada ya mmoja au wawili wa mwanzo kukuzimia simu.

4. Usiwaze kwamba utafanya kazi fulani tu, bali wewe ujiandae kufanya kazi yoyote (ya halali) kujiingizia kipato. Hili swala la watu kuja huku wakiandaa akili, na saikolojia zao za kichwa kwamba anakuja kufanya kazi fulani tu. Ndio limesababisha baadhi ya wabongo kupoteza mwelekeo wa maisha, na kujikuta wanajitupa katika biashara hatari na zisizokuwa halali.

5. Usilete usela mavi usiokuwa na maana. Vijana wengi waliotaka kuleta usela wa Mbagala, Mburahati, Manzese, Temeke, Tandika nk tumewazika wakiwa bado wadogo. Hii ni kwa sababu huku watu hawana muda wa kukimbizana na mwizi wajichoshe. Ukileta usela mavi, watu wanakutafutia target, wanafumua ubongo, kazi imekwisha. yumbani watu wanarudisha nguo au maiti na kesi hamna. Pia usije kwa lengo la kutafuta na kufanya starehe kupitiliza mpaka ukasahau kilichokuleta. Maana kama starehe hata bongo zipo na umeziacha, kama mademu bongo wapo na umewaacha, kama tungi pia bongo lipo umeliacha. So focus kwa kile kilichokufanya utafute nauli uje. Sio kuendekeza kulewa na chupi za Kaburu utapotea mazima na hakuna mtu atakaekurudisha katika chanel yako tena.

6. Ukifika hapa kama wewe ni mpya usikimbilie kukaa kiti cha mbele katika daladala (tax), hata kama imejaa na imebaki siti moja ya mbele, ni bora usubiri nyingine alafu ndio upande. Hii ni kwa sababu huku majimbo mengi daladala zao hakuna kondakta anaezunguka ndani ya daladala kuomba nauli. So ukisema unakimbilia mbele kukaa na dereva, utashangaa watu wanakusanya hela zote huko nyuma, alaf wanakutupia wewe ndio uhesabu na kama kuna mtu ametoa hela kubwa umrudishie chenji, na ikiwa pungufu uhakikishe waliokupa wanazieneza. Dereva yeye hupokea nauli ambayo imeshahesabiwa tayari na iwe imetimia. Ikipungua hata sh hamsini basi ataanza na wewe uliepokea hela kabla ya kuendelea na waliopo ndani ya gari. Pia asilimia kubwa ya madereva wa hapa wana silaha mbali mbali ndani ya gari zao, kama sio bunduki basi fimbo inayofanana na mkia wa taa. So hela yake isipoenea na wewe ndo New comer (mpya) haujui lugha, basi imekula kwako. Hata ujitetee kwa English yako ya kuunga unga hatokuelewa. Naomba niishie hapa.
Uko SA kwa miaka mingap? Labda nikutahadharishe ukirud bongo pia Kuna mambo kadhaa yamebadilika
 
We ni mshamba alafu unaona kuishi sauzi ni ujanja sana
Konda msafi amesema kuna kazi formal kuzipata ni ngumu kama udoktar kwenye hospital za serekali, uhasibu achana na hizo huko hotelini
Naona umeamua kutumia ID nyingine kutetea ulichoandika. Tatizo unakurupuka bila kujua unachoandika.

Mimi kule juu niliandika kwamba ukijua English itakusaidia kupata kazi kiurahisi, ila sikuandika aina ya kazi kama ni ya serikali au ya private. Kikubwa nilichomaanisha ni kupata kazi maana huku mtu anakuja kwa lengo la kutafuta kazi haijalishi hiyo kazi ni ya aina gani. Kama ulitumia akili kusoma utakuta nimefafanua vizuri kuwa ukija hautakiwi uweke akilini kuwa ni kazi ya aina gani utakayofanya. Yani yoyote utakayopata ndio riziki yako hiyo.

Sasa mtu anakuja tena kudai ooh hauwezi kupata kazi serikalini sijui wazimbabwe wanafanya kazi za hovyo. Sasa ni wapi nilipoandika kuwa utapata kazi serikalini? Au wapi nilipoandika kuwa wazimbabwe wanafanya kazi serikali? Muwe mnasoma kwanza vizuri na muelewe kabla ya kukimbilia ku comment upuuzi.
 
Naona umeamua kutumia ID nyingine kutetea ulichoandika. Tatizo unakurupuka bila kujua unachoandika.

Mimi kule juu niliandika kwamba ukijua English itakusaidia kupata kazi kiurahisi, ila sikuandika aina ya kazi kama ni ya serikali au ya private. Kikubwa nilichomaanisha ni kupata kazi maana huku mtu anakuja kwa lengo la kutafuta kazi haijalishi hiyo kazi ni ya aina gani. Kama ulitumia akili kusoma utakuta nimefafanua vizuri kuwa ukija hautakiwi uweke akilini kuwa ni kazi ya aina gani utakayofanya. Yani yoyote utakayopata ndio riziki yako hiyo.

Sasa mtu anakuja tena kudai ooh hauwezi kupata kazi serikalini sijui wazimbabwe wanafanya kazi za hovyo. Sasa ni wapi nilipoandika kuwa utapata kazi serikalini? Au wapi nilipoandika kuwa wazimbabwe wanafanya kazi serikali? Muwe mnasoma kwanza vizuri na muelewe kabla ya kukimbilia ku comment upuuzi.
Id nyingine ipi angalia nyuzi zangu na zake kama zinaendana acha ushamba wewe sio wakwanza kuishi south africa na sio ujanja
 
Uko SA kwa miaka mingap? Labda nikutahadharishe ukirud bongo pia Kuna mambo kadhaa yamebadilika
Mimi nina miaka zaidi ya 20. Nilikuja nikiwa kijana mdogo, ila kwa sasa umri umesogea. Bongo nilikuwa nakuja sana. Tofauti na baadhi ya wabongo wengine ambao toka wafika hapa hawajawahi kurudi bongo.

Mara ya mwisho kuja bongo ilikuwa ni 2019 kabla ya corona. Toka kipindi hicho mpaka leo sijakanyaga bongo, japo nina mpango wa kuja mwisho wa mwaka.
 
Mkuu usitumie nguvu sana kwenye kuelezana kupata kazi SA ni connection wapo Watanzania wanafanya kazi kwenye Bunge la SA na wengine wapo Jeshini, Bank ndio wamejaa sasa ukiwa umetoka life tofauti na wao hauwezi kuwajua mpaka unarudi Tanzania hata hapo hapo Tanzania yapo maisha utayasikia tu kama hauna connection yeyote Watanzania sio kama mataifa mengine akiwa na fursa anaweka ukuta msikutane labda uwe ndugu yake...
Huyo kijana anaonekana hajui chochote kinachoendelea nje ya Tanzania achilia mbali SA. Ni kijana anaeonekana hajatoka. Hawa ni wale vijana wa Tunduma pale mpakani ambao wengi wao hupewa story mbili tatu na watu wanaotoka SA, kisha wao huichukua hiyo story na kuwasimulia wenzao kama hivi bila kujua kwamba katika wasimuliwaji kuna wale ambao wanafahamu kindaki ndaki kile wanachosimulia pengine zaidi yao wao. So mtu kama huyo ni wa kumuelewa na kumpuuza tu.
 
Id nyingine ipi angalia nyuzi zangu na zake kama zinaendana acha ushamba wewe sio wakwanza kuishi south africa na sio ujanja
Vijana wa tunduma mpakani mkisha hadisiwa story mbili tatu na watoka SA tayari na nyinyi mnakuja jukwaani kujifanya mnajua. Nimekuuliza maswali ni wapi niliposema kuwa mtu ukifika South utafanya kazi za maana wanazofanya wasouth afrika umeshindwa kunijibu na kuishi kulalamika tu.
 
Vijana wa tunduma mpakani mkisha hadisiwa story mbili tatu na watoka SA tayari na nyinyi mnakuja jukwaani kujifanya mnajua. Nimekuuliza maswali ni wapi niliposema kuwa mtu ukifika South utafanya kazi za maana wanazofanya wasouth afrika umeshindwa kunijibu na kuishi kulalamika tu.
Kila kazi ya maana ilimradi umelizika nayo haya maswala color job na physical hayana maaana kabisa, mbona mwanvita alikuwa sa anafanya kazi voda na alikuwa anavuta kibunda kwani hakuna wsa wanaoweza kufanya?
 
Mimi nina miaka zaidi ya 20. Nilikuja nikiwa kijana mdogo, ila kwa sasa umri umesogea. Bongo nilikuwa nakuja sana. Tofauti na baadhi yam wabongo wengine ambao toka wafika hapa hawajawahi kurudi bongo.

Mara ya mwisho kuja bongo ilikuwa ni 2019 kabla ya corona. Toka kipindi hicho mpaka leo sijakanyaga bongo, japo nina mpango wa kuja mwisho wa mwaka.
Mkuu me nataka kujua hivi uki over stay si ndo inabidi uishi kwa kujificha ili uepuke kamata kamata ya askari wa migration mitaani? Au hii imekaaje kwa uelewa wako
 
Mimi nina miaka zaidi ya 20. Nilikuja nikiwa kijana mdogo, ila kwa sasa umri umesogea. Bongo nilikuwa nakuja sana. Tofauti na baadhi ya wabongo wengine ambao toka wafika hapa hawajawahi kurudi bongo.

Mara ya mwisho kuja bongo ilikuwa ni 2019 kabla ya corona. Toka kipindi hicho mpaka leo sijakanyaga bongo, japo nina mpango wa kuja mwisho wa mwaka.
Tupe michongo nasisi tuje kaka huku maisha magumu na kuna watu wasiojulikana wanapoteza watu
 
Dah aisee hongera sana bingwa. Ni kama vile umejitoa katika tanuri la moto mkuu.
Sana aisee siku napanda basi kutoka cape kuja Pretoria ku clear mambo ya passport nilisema Asante Mungu maana mikononi mwa patrol ya police nimenusurika mara tatu
Mikononi mwa gangs mara mbili mbaya Moja haikuwa mbaya sana
Usiku mbaya Woodstock kwa walioko Cape town wanapajua
Pretoria yenyewe amanusura nizichange vibaya aliniokoa jamaa mmoja m colored kwa kunipa info late sana nikala bus kwenda Joz kulala park station three days
Park station penyewe ilibidi nipigane na wamalawi vibaya sana wao wakijua mi mmalawi na watz wanajua mi mrundi basi tafrani kwa kweli kurudi tz nilishukuru na yes lilikuwa tanuru la moto
 
Tuelekezane tu wazee mtufumbue macho msituite washamba bhana ingawaje hatujui kitu...
RPC wa Hwange hapo Zimbabwe ni Mtanzania na anajivunia utanzania wake na anajulikana kama Mtanzania mdogo wake yupo SA jeshini...
Hata mwanza border ya Malawi na Mozambique Kuna migration officer nilimkuta ni mtz jamaa ni alikarim sana
 
Back
Top Bottom