Kama una mtaji fanya biashara ya Mbuzi, utakuja kunishukuru

Kama una mtaji fanya biashara ya Mbuzi, utakuja kunishukuru

Hii mada nzuri sana. Lakini ili angalau upate faida inakubidi angalau uwe una uwezo wa kuuza mbuzi hata 100
Yaaah ni kweli kwa nia ya kupata faida kubwa! Kitu cha kuangalia kwenye biashara yoyote ni kile kiitwacho "BREAK EVEN POINT". Wafanyabiashara mnajua ninachosema yaani angalia POINT au SEHEMU unapopatia FAIDA. Ukipafahamu then idadi siyo hoja kwani utakuwa umeshajua break even point yako na faida yako itakuwaje!
 
Tatizo wanachinja usiku na huwa mbuzi ni wengi sana labda zaidi ya elfu 5 na wanakuwa wamechanganywa kutoka sehemu mbali mbali ni ngumu kuingia kiwandani kusubiria mbuzi wako wachinjwe na in short utaratibu wao uko hivyo, lakini they are reliable.
Hakuna kitu hapo. Watakuwa wanawapiga watu Sana
 
[emoji911][emoji911]RAMANI RAMANI RAMANI[emoji911][emoji911]

■TUNACHORA RAMANI KWA BEI NAFUU SANA
■TUNAKADILIA GHARAMA ZA UJENZI
■TUNA SHAURI AINA YA UJENZI

◇HATUA(STEPS)
● Andaa hitaji lako la idadi ya vyumba
● Tunakuandalia sketch y mpangilio,mpk utapo ridhika
● Tupe size ya kiwanja chako
● Lipia advance ya kazi
● Tutachora kwa uaminifu na kuipiga mihuri tayar kwa kibali cha unenzi
● Tunakufanyia delivery ya kazi yako kwa dsm ,mikoani tuna tuma pia ,

utamalizia gharam wakati wa makabithiano wa kazi

Mawasiliano whats up cont#0768160754 au #0776590555
KARIBU TUKUHUDUMIE
Kwa nn usingefungua uzi wenye hili tangazo lako? Mpk udandie kwenye uzi wa watu?
Huoni inaleta mashaka hata kwa ss wateja kujua km kweli wewe ndo mtoa huduma au umedandia kazi za watu....
 
Mm niliwai kufanya hii biadhara ya mbuzi lkn nilikuwa nakwenda kuuza pugu. Ukiwa umezoea kufanya buashara ya nyanya ,vitunguu, mchele ,ukija kwenye buashara hii unakuta kuna changamoto nyingi sana , changamoto kuuubwa kumsafilisha mbuzi afike akiwa salama. Utakuta dari ina mbuzi 180 yaani wamebanana itabidi awepo mtu wa kuwainulia, kuna jamaaa aliuwa kondoo 5 kwa safali moja. Changamoto nyingine pale pungu vijana wa kikurya ni wezi sana wa mbuzi usipokuwa makini wakati wa kushusha unapigwa mbuzi hata 2 , ukinunua mbuzi ktk kijiji chochote kuna kibali unakata inategemea na sehemu kuna sehemu wanalipia sh 1000 kwa kila mbuzi na unapewa lisiti ya mashine. Sasa hapo unaweza ukajiongeza yule jamaa asikuandikie idadi ya mbuzi kwa hiyo kama umenunua mbuzi 50 unampa 40 eflu yeye anauandikia risiti ya 30 elfu ukiwa baada ya hapo kuna kibali kingine ambacho miaka ile tulikuwa tunalipa 1500 kwa kila mbuzi hiki ndio muhimu sana ambacho kinakufanya upite popote bila kupingwa,lkn hiki kibali cha pili huwa kinalipwa kwa gali nzima yaani anakata dalali wa gali na mara nyingi malipo hujumlishwa kwenye nauli.

Ukitaka biashara hii upate faida usinunue mnadani mm nilikuwa afikia kwa jamaa aafu tunaenda nyumba hadi nyumba pale unazungumza na muuzaji mpaka mwisho ,mnadani wateja wengi hupanda bei hii itakuganya nawe upande bei
Kutokununua mzigo mnadani kuna muda inakua na changamoto nakumbuka kuna kipindi nafanya biashara ya kuku nikawa naenda mlango kwa mlango. Niliingia hasara sana kwanza ilichukua mda mrefu kujaza mzigo, pili nilinunua kwa bei kubwa sababu siku ya mnada kuku walikua wengi bei ikashuka maradufu zaidi ya ile nilinunua door to door
 
Mleta mada hongera Sana kwakutufumbua

Na tumaswali tuchache mkuu

Mnappsafirisha mbuzi malipo yapoje mnalipa kwa idadi ya mbuzi au makadirio tu?

Naomba kujua idadi ya vibali ambavyo unatakiwa kuwa navyo kwa ujumla ili usisumbuliwe toka kununua had kufikisha mzgo sokoni

Je katika mwezi unaweza kufanya mizunguko mingapi yaan tripu ngapi kupeleka mbuzi kiwandani?

Asante mkuu tumaini langu nitapata majibu mkuu





Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Mleta mada hongera Sana kwakutufumbua

Na tumaswali tuchache mkuu

Mnappsafirisha mbuzi malipo yapoje mnalipa kwa idadi ya mbuzi au makadirio tu?

Naomba kujua idadi ya vibali ambavyo unatakiwa kuwa navyo kwa ujumla ili usisumbuliwe toka kununua had kufikisha mzgo sokoni

Je katika mwezi unaweza kufanya mizunguko mingapi yaan tripu ngapi kupeleka mbuzi kiwandani?

Asante mkuu tumaini langu nitapata majibu mkuu





Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app

Maswali mazuri ndugu.

Kila mbuzi unamlipia ushuru 1000Tsh kwa kila mbuzi halafu kibali kinakuwa ni kimoja ambacho ili kupunguza gharama mbuzi wote wanakuwa chini ya kibali kimoja kama vile mwenye mzigo ni mtu mmoja, kama mzigo ni mkubwa basi sisi tulikuwa tunakata vibali viwili basi.

Kuhusu mara ngapi unaweza kupeleka mzigo itategemeana na mtaji wako na uchakarikaji wako katika kutafuta mzigo. Upande wa mtaji Nina maana kwamba unaweza kuagiza mzigo kiwandani labda wa 3M halafu kama una balance ukabakia unakusanya mzigo mwingine wakati unasubiria mzigo ufike kiwandani, mbuzi wachinjwe na pesa utumiwe. Kuna wakati inaweza kuchukua hadi siku 3 au 4 kutoka mchakato wa kusafirisha mbuzi kutoka vijijini hadi kiwandani hadi kupata pesa kwa hiyo ndani ya siku hizo unajikuta una andaa mzigo mwingine, unafanya rotation. Wenye mitaji mikubwa walikuwa walifanya hivi.

Sijui kama kuna swali nimesahau kujibu mkuu
 
Mleta mada hongera Sana kwakutufumbua

Na tumaswali tuchache mkuu

Mnappsafirisha mbuzi malipo yapoje mnalipa kwa idadi ya mbuzi au makadirio tu?

Naomba kujua idadi ya vibali ambavyo unatakiwa kuwa navyo kwa ujumla ili usisumbuliwe toka kununua had kufikisha mzgo sokoni

Je katika mwezi unaweza kufanya mizunguko mingapi yaan tripu ngapi kupeleka mbuzi kiwandani?

Asante mkuu tumaini langu nitapata majibu mkuu





Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app

Nauli ya mbuzi mnalipa kwa idadi ya mbuzi lakini hao madreva kutoka Kondoa kwenda Dodoma mjini kama gari ni la kuungaunga huwa hawahesabu idadi ya kila mbuzi mnamkadiria tu.

Kama wewe ni mwepesi na unajua kuongea vema na watu utapata mzigo kiurahisi sana kuliko wale watoto wa mama
 
Kwa mwezi kiongozi ulikuwa na uwezo wa kufanya mizunguko mingapi, yani ununuzi na uuzaji wa mzigo

Aise mimi mtaji wangu haukuwa mkubwa kwa hiyo nilikuwa nasubiria malipo kwanza kwa hiyo kwa week nilikuwa nafanya trip moja au mbili. Lakini niseme ukweli nilikuwa sikosi faida nzuri kabisa kwa sababu nilikuwa napigania maisha siyo ukwasi kama wa MO
 
je kiwanda ni kimoja tu kwa dar na huko Arusha

na wanapokea Mbuzi siku gani au ni kila siku?

kiwanda kiko wapi kwa hapa dar,

kuna utaratibu gani wa kupeleka mbuzi wako.. unaandikishwa in advance ili kuwa supplier wao au unaweza tu ukaja na mbuz wakapokea..

na hizo alama mnaowaweka mbuzi mlikuwa unawaandika na nini au ndo kuwa piga chata na vyuma vya moto

Je wanapokea Aina nyingine za nyama kama vile ng'ombr au ni mbuzi tu

Ndugu yangu yangu sijui nia yako ya kuuliza maswali haya kwa sababu nimetoa maelezo yote haya kweli uzi, kiwanda kilipo nimetaja kijiji, wilaya hadi mkoa, nimesema mbuzi unaweka alama kwa kukata manyonya kwa kutumia mkasi na mzigo nimeshasema kila siku wanapokea. Upande wa order ukishapeleka mara ya kwanza basi unasajiliwa na alama yako inatunzwa kwa hiyo siku nyingine hata huhitaji kwenda na gari kiwandani wewe unapakia mzigo unaenda kiwandani halafu unasubiria notification ya idadi ya kilo na mtonyo wako.
 
Habarini Waungwana!

Leo nimeona nitoe mchongo wa biashara ambayo binafsi nimewahifanya kabla sijapata ajira na natarajia kuendelea kufanya baada ya ajira kuisha.

Uzuri wa biashara hii, pamoja na kuwa na faida nzuri, soko lake ni la uhakika sana na changamoto zake ni chache sana na zinakabilika kwa mtu ambaye ameamua kwa dhati kutafuta.

BIASHARA YENYEWE NI KUNUNUA MBUZI NA KWENDA KUUZA KIWANDANI.

A. Upatikanaji wake

Upatikanaji wa mbuzi. Pamoja na mambo mengine ambayo Tanzania tumejaliwa ni mifugo hasa mbuzi. Kuna upatikanaji wa uhakika wa mbuzi na kondoo katika mikoa ya Dodoma (Urangini), Singida, Tanga na Tabora. Kwa kule KONDOA kuna Warangi wazuri sana madalali ambao ni waaminifu sana tofauti na madalali ambao tumewazoea katika jiji la Dar.

Kwa ushauri wangu, sehemu nzuri zaidi ya kununua mbuzi kwa bei nzuri, wenye ubora (Uzito) na faida nzuri, urahisi wa upatikanaji wake na hata urahisi wa usafirishaji ni KONDOA (Urangini). Huku kuna minada ya mbuzi kila siku na hivyo kwa siku unaweza kununua hadi mbuzi 50 na zaidi kama una mwenyeji mzuri.

B. Soko lake
Binafsi ningependekeza kupeleka kiwandani hasa kiwanda cha TanChoice kilichopo Soga, wilani Kibaha mkoa wa Pwani. Hapa utaweza kuuza idadi yoyote ya mbuzi japo huwa wanapenda walau uwe na mbuzi kuanzia 20 (hii ni idadi wakati mimi napeleka inawezekana kukawa na mabadiliko kwa sasa).
Sehemu nyingine ni Longido-Arusha katika kiwanda cha Eliya Food Ltd japo kwa Arusha kuna wanunuzi wengi hasa Wakenya wanatoa bei nzuri sana.

C. Bei ya mbuzi

Kwa kuwa mbuzi hununuliwa vijijini bei yake siyo kubwa kwani ina range kati ya 30-70 elfu. Mbuzi wa 30 elfu anaweza kukadiriwa kuwa na uzito wa kilo 7 au 6.5. Mbuzi wa 70 elfu anaweza kufikisha hadi 12Kg au 13Kg. Kiwandani hawapendelei sana mbuzi wakubwa sana kwa hiyo ni vema kuwa makini katika selection ya mbuzi wa size ya kati ili upate faida nzuri na soko la uhakika.

D. Bei ya nyama kiwandani
Wakati mimi napeleka mbuzi katika kiwanda cha TanChoice, walikuwa wakinunu kwa Tsh 7000/Kg kwa mbuzi na Tsh6800/Kg. Kwa Arusha inasemekana bei iko juu kidogo ila Arusha niseme ukweli sana information za kutosheleza kwani nilienda trip moja tu.

E. Kadirio la faida
Kama mbuzi amenunuliwa kwa kwa Tsh 50,000/= halafu akatoa Kg 9 za nyama ambazo ni sawa na Tsh 63,000/= faida yake itakuwa karibu 6,000Tsh hadi 7,000Tsh kwa mbuzi mmoja. Hapa unakuwa umetoa Gharama zote kuanzia usafiri kutoka Dar nimetumia kwa wakazi wa Dar hadi Kondoa, kulala guest, usafiri kwenda minadani, kuwasafirisha kutoka minadani hadi Kondoa mjini, ushuru wake na vibali, usafiri kwenda Dar kiwandani, chakula na mengineyo.

F. Changamoto zake

Kusema ukweli kila kazi ina changamoto zake na hasa inapokuja suala la biashara, basi changamoto haziepukiki. Biashara hii kama zilivyo biashara nyingine ina makandokando yake kama ifuatavyo;
  • Kuna wakati kunakuwa na wanunuzi wengi wa mbuzi kwa hiyo competition inakuwa kubwa sana na kupelekea wauzaji kupandisha bei na hivyo faida kukuachia kidogo sana
  • Usipokuwa makini madalali ambao wameshawahi kufika Dar basi lazima watakulalia katika ununuzi wa mbuzi. Binafsi kwa mara ya kwanza nilijikuta kwa kila mbuzi mmoja napigwa 2000-3000Tsh. Yaani mbuzi anamununua 40,000Tsh halafu ananiambia amemchukulia 43,000Tsh.
  • Kuna wakati upatikanaji unakuwa mgumu hata kama wanunuzi siyo wengi. Baadhi ya siku unakuta wanaoleta mbuzi minadani ni wachache sana na hivyo unaweza kutumia siku nyingi kupata mzigo mzuri.
  • Uwezekano wa kuibiwa mbuzi. Kumbuka munapowanunua mbuzi kutoka mnadani basi munawahesabu na kila mnunuaji anaweza label ya kwake kwenye mbuzi kwa kutumia mkazi. Mimi ilikuwa nachora herufi K ambayo ni herufi ya kwanza ya jina la wife. I love her and she knows that. Baada ya hapo munawaweka mbuzi pamoja na kumkabidhi kijana anayewaswaga kutoka mnadani(minada ipo maporini sijui kwanini) hadi kuwafikisha mjini. Baada ya hapo mbuzi wote wanawekwa kwenye gari na kupelekwa kiwandani. Wakati mwingine mnaweza kupata gari linaloishia Dodoma na kulazimika kuunganisha na wanunuzi wengine wanaofikishia mzigo wao Dom mjini na kisha kutumia gari moja kupeleka kiwandani. Sasa inaweza kutokea au kijana anayewaswaga kutoka mnadani akapiga pande mbuzi mmoja au vijana wanaowaangalia na kuwapeleka malishoni kama unanunua mzigo mkubwa kwa siku kama tatu au zaidi.
-Mbuzi kukosa uzito wa kutosha. Hapa ndo sehemu ya kuwa makini sana. Mbuzi wanaotoka Tabora kwa mfano, uzito wake ni mdogo sana wanapochinjwa tofauti na mbuzi wa Kondoa. Kwa hiyo ukinunua mzigo Tabora kwa bei kubwa kuna uwezekano ukaingia loss na kurudi hapa kunitukana na kunilaumu. Naomba kwa atakayekuwa interested aulize maswali ya kutosha na ikiwezekana afike Kondoa kufanya preliminary investigation and research. I do recommend Kondoa kwa warangi.
G. Malipo

Unapofikisha mzigo kiwandani unaandikisha idadi ya mbuzi, na label uliyowawekea. Kisha unawaachia bank account au namba ya simu kama utapenda malipo yafanyike kwa njia ya simubank. Baada ya siku moja au mbili maximum unatumiwa kiasi cha uzito uliopatikana baada ya kuchinja mzigo wako na kisha account yako inasoma. Hapa kwenye malipo mara nyingi hakuna usumbufu japo binafsi nilifikiria sana reliability yake yaani wanakwambia umepata KG 500, kwa mfano, inakuwa ni hiyo hiyo au inawekana ilikuwa zaidi?

Hitimisho
Kila biashara ina changamoto kama nilivyosema mwanzoni lakini biashara ambayo soko lake ni la uhakika na mzunguko wake ni wa uhakika basi daima huwa ni biashara nzuri. Kwa yeyote anayependa kujaribu biashara hii, nashauri afanye utafiti wa kutosha na kisha aanze na mzigo kidogo hata wa 1M kwanza aone faida yake, changamoto zake n.k.

ASANTENI KWA MDA WAKO NAKUTAKIENI MAFANIKIO KWA KAZI UFANYAYO.

Soga kipo kibaha upande upi mkuu kibaha pana kidgo
 
Mm niliwai kufanya hii biadhara ya mbuzi lkn nilikuwa nakwenda kuuza pugu. Ukiwa umezoea kufanya buashara ya nyanya ,vitunguu, mchele ,ukija kwenye buashara hii unakuta kuna changamoto nyingi sana , changamoto kuuubwa kumsafilisha mbuzi afike akiwa salama. Utakuta dari ina mbuzi 180 yaani wamebanana itabidi awepo mtu wa kuwainulia, kuna jamaaa aliuwa kondoo 5 kwa safali moja. Changamoto nyingine pale pungu vijana wa kikurya ni wezi sana wa mbuzi usipokuwa makini wakati wa kushusha unapigwa mbuzi hata 2 , ukinunua mbuzi ktk kijiji chochote kuna kibali unakata inategemea na sehemu kuna sehemu wanalipia sh 1000 kwa kila mbuzi na unapewa lisiti ya mashine. Sasa hapo unaweza ukajiongeza yule jamaa asikuandikie idadi ya mbuzi kwa hiyo kama umenunua mbuzi 50 unampa 40 eflu yeye anauandikia risiti ya 30 elfu ukiwa baada ya hapo kuna kibali kingine ambacho miaka ile tulikuwa tunalipa 1500 kwa kila mbuzi hiki ndio muhimu sana ambacho kinakufanya upite popote bila kupingwa,lkn hiki kibali cha pili huwa kinalipwa kwa gali nzima yaani anakata dalali wa gali na mara nyingi malipo hujumlishwa kwenye nauli.

Ukitaka biashara hii upate faida usinunue mnadani mm nilikuwa afikia kwa jamaa aafu tunaenda nyumba hadi nyumba pale unazungumza na muuzaji mpaka mwisho ,mnadani wateja wengi hupanda bei hii itakuganya nawe upande bei

Kweli mkuu kwa maelezo yako ni dhahiri umewahi fanya biashara hii, lakini sasa hiyo sehemu ya mwisho ya kwenda nyumba kwa nyumba ni ngumu sana, utapata taabu sana kufikisha mzigo na bei itakuwa kubwa sana. Ukibahatika mnadani wanunuzi wakawa wachache na mbuzi wakawa wengi, unapata mbuzi wa kuchagua wewe mwenyewe, bei ndogo na faida inakuwa nzuri.

Halafu kingine kwa sasa iko hivi; kuna wenyeji kule ambao ni Warangi wenzao, wanaojua kila kichaka na kila nyumba, kwa hiyo huwa wananunua mbuzi kutoka kwenye nyumba za watu kisha kuwapeleka minadani kuwauuza, hawa jamaa wanapiga faida nzuri pia kwa sababu unaweza kukuta kwa kila mbuzi anapiga zaidi ya 5000/= akiwa na mbuzi 50 anaondoka zake na 250,000/= kwa siku. Kwa hiyo hawa wenyeji huwezi kushindana nao kwani wao wanaongea lugha moja.
 
Maswali mazuri ndugu.

Kila mbuzi unamlipia ushuru 1000Tsh kwa kila mbuzi halafu kibali kinakuwa ni kimoja ambacho ili kupunguza gharama mbuzi wote wanakuwa chini ya kibali kimoja kama vile mwenye mzigo ni mtu mmoja, kama mzigo ni mkubwa basi sisi tulikuwa tunakata vibali viwili basi.

Kuhusu mara ngapi unaweza kupeleka mzigo itategemeana na mtaji wako na uchakarikaji wako katika kutafuta mzigo. Upande wa mtaji Nina maana kwamba unaweza kuagiza mzigo kiwandani labda wa 3M halafu kama una balance ukabakia unakusanya mzigo mwingine wakati unasubiria mzigo ufike kiwandani, mbuzi wachinjwe na pesa utumiwe. Kuna wakati inaweza kuchukua hadi siku 3 au 4 kutoka mchakato wa kusafirisha mbuzi kutoka vijijini hadi kiwandani hadi kupata pesa kwa hiyo ndani ya siku hizo unajikuta una andaa mzigo mwingine, unafanya rotation. Wenye mitaji mikubwa walikuwa walifanya hivi.

Sijui kama kuna swali nimesahau kujibu mkuu
Umejibu vizuri Sana mkuu shukrani Sana

Ngoja nijichange angalau nipate mtaji wa mbuzi 100 kwa makadirio yangu naona hapo ndyo faida kidogo naweza iona

Kwa ushauri Zaid nitakuwa nazama pm mkuu ili uwe MENTOR WANGU kwenye hii bizness

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Umejibu vizuri Sana mkuu shukrani Sana

Ngoja nijichange angalau nipate mtaji wa mbuzi 100 kwa makadirio yangu naona hapo ndyo faida kidogo naweza iona

Kwa ushauri Zaid nitakuwa nazama pm mkuu ili uwe MENTOR WANGU kwenye hii bizness

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app

Karibu sana mkuu. Ni katika kutoa nasi tunapokea. Binafsi mawazo ya watu yamenisaidia sana kufika sehemu nilipo kwa sasa.
 
Back
Top Bottom