Kama una mtaji fanya biashara ya Mbuzi, utakuja kunishukuru


Kijana una upeo mkubwa, nimefurahishwa sana na comment yako hii. Ni ufafanuzi unaothibitisha Uwezo wako mkubwa wa kufikiri na kupambanua mambo kwa weledi.
 
Huu uzi kwanini usihamiishiwe kule kwenye "Stories of change "?
 
That friend of "ours" aliwahi nidokezea hii na mzee wake wa kiyemen, unakumbuka? sema yeye info zake zilikuwa na manyokanyoka mengi kama kawaida yake...
 
That friend of "ours" aliwahi nidokezea hii na mzee wake wa kiyemen, unakumbuka? sema yeye info zake zilikuwa na manyokanyoka mengi kama kawaida yake...

Mambo mengi, version tofauti sana na hii.
 
Daah!kaka jebel ahsante sana!!kama yupo MTU anahitaji hyo business na yuko busy hana mda snipe dili hill mi antume tunaingia mkataba hata was miezi sita mi namfanyia kila kitu mradi maelewano tu
Uko wap mkuu
 
Ulitumia usafiri gani kuwasalimisha kiongozi?
 
Ulitumia usafiri gani kuwasalimisha kiongozi?
Nilikuwa natumia gari ndogo mkuu, sana sana kirikuu
Nawakusanya kwa siku kama mbili au tatu halafu napiga simu Mwanza wanaleta gari

Changamoto unaweza ukanunua nguruwe kwenye nyumba kumi maeneo tofauti gari ikija mnaanza kupita nyumba moja mpaka ya mwisho tunapakia tunaondoka
Pia ukishawalipia wakati unasubiri usafiri
mwenye mji anakwambia gharama za kuwalisha ni zako mpaka utakapokuja kuwachukua.

Kirikuu inakaa wastani wa nguruwe 12 wodogo na 9 wakubwa

Kibali ilikua tunakata Buselesele
kila nguruwe Tsh1000

Kila nguruwe nilikuwa naweza kupata faida ya Tsh 50,000 ila sehemu kubwa ya faida inaliwa na usafiri.
 

Mkuu cheki PM tafadhali
 
Umenikumbisha miaka fulani huko tumefika gairo kununua kuku vijijini Dogo wa kimara akawa kuku akikimbia tunasema mkimbize au chukua huyo kuku umfunge miguu anasema hawa hawang’ati kweli mbona wakali mwanaume huyo
😅😅😅😅
 
Hii biashara ni nzuri hata Arusha maana Kikatiti, na kule namanga kuna wanunuzi wa kenya wanakuja kununua mbuzi na wamaasai wanadai wanafunguka pesa nzuri sana, japo sikuwa kuingia front kwenye hili, lakini kikatiti huwa kuna mnada wa mbuzi na ng'ombe kwa hapa Arusha, nadhani Kikatiti bei za mbuzi huanzia 60,000 huwa bei zao mnadani ndiyo hizi hazishukagi. Kondoa ndiyo ninasikia wapo mbuzi mpaka wa 30000 na wana weight ya kuridhisha

Nitafuatilia pia updates cha kiwanda cha nyama Arusha.
 
Alisema amepata mchongo nje ya nchi nadhani😅 we sahizi upate line ya Marekani utakataa uendelee kuswaga mbuzi bongo?
Yeye ametoa mapendekezo kuwa ile ilikuwa ni biashara yenye afadhali hukosi pesa kabisa yaani sio sawa na kukaa bure au kufanya mavitu pasua kichwa.
 
Asante kwa taarifa zenye kujitosheleza..umeeleza vizuri Sana.
Naomba nikuulize swali..lingine..wateja uliwapataje wa kununua nguruwe wengi kwa wakati mmoja..?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…