Ikiwa yapata nusu saa tokea kupaa kwake ndege moja iliyobeba abiria zaidi ya 200
..ikasikika sauti tokea kwa rubani ikisema "injini moja haifanyi kazi na iliyobaki haina nguvu kabisa ni wakati wa kufanya maombi kwani muda sio mrefu ndege hii inaanguka,tumieni nafasi hii kuombana msamaha ili mfike mbinguni salama."
Abiria wakaogopa sana na ukimya na hofu vikatawala.
David na Grace walikuwa miongoni mwa abiria wa ndege ile..
Grace: mume wangu nisamehe Aidan sio mwanao ni mtoto wa yule mlinzi,na hata kipindi umetekwa wakati umefuata pesa benki ilikuwa ni mpango wangu ili nipate pesa ya ada ya boyfriend wangu chuo kikuu.
David:wala usijali mamy,unisamehe pia kwa kuwa nishatembea na wadogo zako karibia wote kibaya zaidi yule mtoto wa mwisho wa mdogo wako Angel ni wangu japo mume wa Angel huwa anadhani anafanana na mwanenu Anita kwa sababu ni watoto wa Mama mkubwa na mdogo.
Basi watu wakawa bize kwelikweli kuombana msamaha na kusali. Ghafla ikasikika sauti ikisema
"Asante kwa maombi yenu hali ya ndege imetengamaa na tutafika salama"[emoji2][emoji2]
Watu wote "aaaaahhhh we rubani mjinga nini usitutanie sisi, we si umesema hii ndege inaanguka sasa iweje unageuza kauli ghafla?? tunasema ndege lazima ianguke hiii haiwezekani,kama imekushinda tunaiangusha wenyeweee[emoji35][emoji35][emoji35]
"Ideas are easy but Implementation is hard."