Kama unaingiza faida ya Tsh. 30,000 na kuendelea kwa siku pita hapa

salute[emoji41]
 


Hhaha dili chafu na zenye risk kubwa ndo zinalipa...duh ..wameshafika huko wasukuma kwenye mbao??ahaha..!ila naona mbao kwa miaka hii hazilip vzr km miaka ya 2000!..au 🤔!
 
Maelezo mkuu tafadhali
 
Unaenda kutapeliwa.. kuwa makini [emoji23][emoji23]
Wewe unajiita lazy, and a boy, not a man, utanishauri nini? What can a lazy boy advice me what to do...embu nenda shule kaondoe ujinga.
 
Kuna gharama za uendeshaji na mtaji.
Kwanza kabisa msimamizi ni bora uwe wewe mwenyewe
Gharama za uendeshaji ni kwenye manunuzi ya umeme tu
Mtaji wake inategemea wewe unataka kuanza na console ngapi na za aina ipi?
Ps 2 dukani unapata kwa sh 170,000/= full ukitafuta used bei inazungumzika
Ps 3 dukani inapatikana kwa sh 500,000/= ukitafuta used bei inazungumzika
Ps 4 dukani inapatikana kwa sh 1,000,000/= mpaka 700,000/= ukitafuta used bei inazungumzika
Utanunua na tv inapendeza kuanzia inch 24 kwa kila console moja
 
Mwakajana kuna mzee mmoja alikamatwa huko Tabora alikuwa na gunia hamsini na tisa (59).
 
Kuna mtu namjua , heheehe .. N kasheshe, ana zaid ya mwaka, hana mpango wa kuacha leo wala kesho
 
ASANTE SANA MKUU KWA IDEA NYINGI ZA BIASHARA ULIZOTOA HUMU NDANI, KWANGU MIMI FULL TIME EMPLOYED NAONA HII YA MATOROLI ITANIFAA, SAMAHANI UNAFAHAMU KWA DAR WAPI WANATENGENEZA HIZO TOROLI? CHANGAMOTO YA PILI NI KUMPATA KIJANA WA KUMKODISHA
mafundi wa kuchomelea wote wanaweza kutengeneza matoroli.
Pili mtu wa kumkodisha ni ww kuangalia mazingira hata nyumbani unaweza kuyaweka kikubwa je ni kuna huo uhitaji? Au vijiweni maeneno ya hard ware, sokoni, center kwenye muingiliano wa shughuli mbali mbali za mizigo n.k
 
Nafanya stationery....inalipa sana.
hv stationery inarudishaje faida et, mana copy shiling 50 afu printing 100 but ile machne ya copy inauzwa zaid ya 1milion.....naonaga kama ina return ndogo et
 
hv stationery inarudishaje faida et, mana copy shiling 50 afu printing 100 but ile machne ya copy inauzwa zaid ya 1milion.....naonaga kama ina return ndogo et
inategemeana na location mf. Jamaa angu ana stationary copy sh 100. Kuprint @sh500. Bado makorokoro kibao kama madaftari,kalamu,penseli,vitabu,bible,maua,manila card,lamination,tape,hapo hapo anauza vitu vya urembo vidgvidgo.
Yaani kiufupi stationary yake amesheheni vitu vingi sana. Vichezeo vya watoto ndio usiseme na ndo anauza kuliko hata kupiga copy ila kama endapo wewe kazi yako ji kupiga tu copy na kuchapa utachelewa sana kuona faida.
 
n kweli asee pia naona akiongezea mpesa hapo itakua poa
 

Make money online now
hawa wahuni achana nao utapoteza tu mda wako
ukitaka kutoa hela wanataka uwe na referral 40,kama huna referal wanasema ulipe ili wakupe referal(tangu lini boss akahtaji pesa kutoka kwa mfanyakazi wake?) , ukishalipa yanaaza mambo ya "server down" mara paap ur accout is blocked daaaaaah wahuni sio watu[emoji41]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…