Kama unakasirika sababu ya jambo moja kati ya haya fahamu wewe ni Mpumbavu kabisa

Kama unakasirika sababu ya jambo moja kati ya haya fahamu wewe ni Mpumbavu kabisa

Huu ni mfano(mwongozo tu) wa jinsi unavyoweza kuomba asubuhi, mchana au usiku:

"Baba wa Mbinguni, kwanza nakushukuru kwa kuniokoa na kuniahidi kuwa nikiomba lolote utanipa. Nakuja mbele zako sasa kwa unyenyekevu nikiwa na hitaji langu hili(taja hitaji lako). Ninaamini kuwa Wewe Mungu una uwezo wa kunisaidia au kuniongoza katika njia sahihi. Naamini utanipa kama ulivyoahidi. Napokea kwa imani majibu ya hitaji hili.

Katika jina la Yesu Kristo, Amina."
Amina, Mama Mtumishi barikiwa kwa maombi hakika
 
Kabla ya maisha yangu kufichwa ndani ya Kristo katika Mungu nalikuwa mtu wa namna zaidi ya hiyo hasira,chuki,kukataa maonyo,kutokukubali kukosolewa na Mambo mengi ya namna hiyo.

Lakini kwa sasa ni historia uniseme,unitukane,unidhihaki,unisingizie uongo,unionye hainiumi na hainisumbui Kama zamani kwasababu mimi siyo tena mtu wa ulimwengu huu,na Kama siyo mtu wa ulimwengu huu kwanini niingie kwenye migogoro na watu wa huu ulimwengu?
 
Kabla ya maisha yangu kufichwa ndani ya Kristo katika Mungu nalikuwa mtu wa namna zaidi ya hiyo hasira,chuki,kukataa maonyo,kutokukubali kukosolewa na Mambo mengi ya namna hiyo.

Lakini kwa sasa ni historia uniseme,unitukane,unidhihaki,unisingizie uongo,unionye hainiumi na hainisumbui Kama zamani kwasababu mimi siyo tena mtu wa ulimwengu huu,na Kama siyo mtu wa ulimwengu huu kwanini niingie kwenye migogoro na watu wa huu ulimwengu?
Asante kwa ushuhuda mzuri. Ubarikiwe sana
 
Hakuna binadamu asiye kasirika ,mm nadhani mada yako ingekuwa na mantiki iwapo ungesema mtu asiye weza kudhibiti hasira zake ni mpumbavu.
Hasira haitaji ruhusa yako kuingia ndani ya kifua chako huwa inakuja automatically baada ya kufanyiwa kitu usicho kipenda au cha kuudhi ila kitendo utakacho fanya baada ya hiyo hasira ndo kitakuhukumu iwapo ni mpumbavu au ni mwenye busara.

Huwezi kuniambia eti mwizi aniibie alafu nisiwe na hasira naye, au mke wangu nimfumanie anafanya uzinzi eti nisikasirike ww utakuwa sio binadamu bali utakuwa ni robot.
Ni kweli kila binadamu anaweza kukasirika, na hasira mara nyingi huja bila ruhusa. Hata hivyo, Biblia haituhimizi kukasirika, bali inatufundisha kuitawala ili tusitende dhambi.

📖 Waefeso 4:26-27 BHN
Kama mkikasirika, msikubali hasira yenu iwafanye mtende dhambi, na wala msikae na hasira kutwa nzima. Msimpe Ibilisi nafasi.

👉 Hasira isipodhibitiwa inaweza kusababisha madhara makubwa, kama vile kulipiza kisasi, kuua, kupiga, kutukana nk.

📖 Mithali 14:29"Asiye mwepesi wa hasira ana akili nyingi; bali mtu mwenye moyo wa hamaki huinua upumbavu."
👉Hii inamaanisha kuwa mwenye hekima nyingi ni mtu anayeweza kudhibiti hasira yake badala ya kuiruhusu itawale matendo yake.

📖 Mhubiri 7:9"Usiwe na haraka rohoni mwako kukasirika, maana hasira hukaa kifuani mwa wapumbavu."
👉Andiko hilo ndio msingi wa uzi wangu – si kwamba mtu hawezi kukasirika, bali asiwe mwepesi kukasirika anapofanyiwa mambo madogo yanayoweza kuepukika. Sehemu ya pili ya mstari huo inasema: hasira hukaa kifuani mwa wapumbavu. Wapumbavu ndio wanaoacha hasira ikae(iwe sehemu ya maisha yao).

Yakobo ana-discourage kabisa hasira.

"Kwa maana hasira ya mwanadamu haitendi haki ya Mungu(Yak 1:20)


Tusisahau pia hasira sio tunda la Roho. "Tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu..." (Wagalatia 5:22-23).
 
Sasa unawezaje kuchukizwa, kukasirishwa na usiemjua wala yeye hakujui, nj kweli ni mpumbavu
 
Kabla ya maisha yangu kufichwa ndani ya Kristo katika Mungu nalikuwa mtu wa namna zaidi ya hiyo hasira,chuki,kukataa maonyo,kutokukubali kukosolewa na Mambo mengi ya namna hiyo.

Lakini kwa sasa ni historia uniseme,unitukane,unidhihaki,unisingizie uongo,unionye hainiumi na hainisumbui Kama zamani kwasababu mimi siyo tena mtu wa ulimwengu huu,na Kama siyo mtu wa ulimwengu huu kwanini niingie kwenye migogoro na watu wa huu ulimwengu?
Wanaotafuta kujua siri ya kushinda hasira, Siasa mbaya sana amefichua siri hiyo
 
Kukasirika mbona ni hulka ya binadamu yoyote, kuna mtu hakasiriki??Kikubwa ni kuweza kucontrol hasira na kufanya kitu cha kipumbavu.
Kukasirika ni automatic, ni unvoluntary action, kujizuia usifanye ujinga na kutulia, kucool down, ndani ya muda mfupi na kuchukulia maisha kwa kawaida ndo fadhila tunayoomba.
UKIONA NA WEWE UNAFANYIWA CHOCHOTE KATI YA HIVYO, NA HUHISI CHOCHOTE UPO TU KAMA JIWE, UJUE UNAELEKEA KWENYE KUPOTEA
 
Kukasirika mbona ni hulka ya binadamu yoyote, kuna mtu hakasiriki??
Waefeso 4:26 BHN
"Kama mkikasirika, msikubali hasira yenu iwafanye mtende dhambi, na wala msikae na hasira kutwa nzima."
 
Back
Top Bottom