Kuna mwandishi wa kitabu kiitwacho RICH DAD POOR DAD, aliwahi kuandika title ya kitabu kingine alicho ongelea CASHFLOW QUADRANTS. Ukisoma ndani inaonesha kuwa kila mtu huwa anachagua kukaa kwenye quadrant yake kutokana na kuchagua RISK au kukwepa RISK.
Quadrant ya kwanza anaongelea EMPLOYEES, yaani waajiriwa. Kundi hili la watu hawataki RISK kabisa. Ukikutana nao mshahara ni kila kitu kwao, hawashauriki kuhusu kufanya biashara, kumiliki biashara au kuwekeza. Nadhani uzi unawahusu zaidi. Lakini kwa dunia ya leo ukitegemea tu kuajiriwa hakika hauwezi kuwa tajiri na generation yako lazima ipambane.
Quadrant ya pili inaongelea SELF EMPLOYED, hawa ni watu wa kujiajiri, watu hawa huchagua kuangalia fursa kwenye jamii na kuzivalia njuga. Hawa ni kama mama lishe, wauza matunda, wauza maua n.k , Hawa huanzisha biashara zao na kuzisimamia wenyewe 24/7, Hawa wamechagua RISK ndogo. Na mapato yao huwa size ya kati. Mara nyingi hufanikiwa na kuwa na maisha ya kawaida sana.
Quadrant ya tatu ni BUSINESS OWNERS hawa ni watu wanao miliki biashara. Wao huangalia fursa kwenye jamii na kuzifanyia kazi kwa kuajiri rasilimali watu. Mfano wamiliki wa hotel, restaurant, guest house, bar, mabasi ya mikoa, dala dala. Hawa wanachukua risk kubwa na huwekeza pesa nyingi na hawaogopi kufilisika, japo hufanya risk management ili kujua ni biashara gani aimiliki na ni kwa wakati gani muafaka.
Quadrant ya nne ni INVESTORS, hawa ni wawekezaji kama ulikuwa unawasikia, hununua shares kwenye makampuni makubwa. Hununua majengo na kuuza, Huwekeza kwenye mabenki, huingia ubia na serikali au taasisi n.k Mara nyingi hawa hutokea Quadrant ya pili au ya tatu. Ki ufupi wanajua nini maana ya biashara na mara nyingi ni professionals wa biashara au wameajiri watu ambao ni professionals. Hawaogopi risk hata kidogo.
Kwa hiyo nakubaliana na moderator. Ila arudishe heading ya kwanza kama unaogopa risk usi wekeze. Kimbilia kwenye Quadrant ya kwanza.