Kama unatafuta nyumba ya kupanga DSM, kuna vitu vya kuzingatia usivichukulie poa!

Kama unatafuta nyumba ya kupanga DSM, kuna vitu vya kuzingatia usivichukulie poa!

Huyo jamaa yako mkumbushe kwamba ana miaka 50 mbele sasa asione hivyo alivyo ndivyo itakavyokuwa lawama hatutaki mwambie nimekwambia mimi lawama hatutaki na kama hataki mwache ainjoi ujinga.
MImi sioni shida yake, ni lazima kila mtu ajenge nyumba? Biashara ya kupangisha itakufa. Duniani kote hii biashara ni kongwe, ana miradi yake mikubwa anajimudu kukaa popote. Unafikiri kuwa na nyumba ndiyo kuwa na maisha mazuri?
 
MImi sioni shida yake, ni lazima kila mtu ajenge nyumba? Biashara ya kupangisha itakufa. Duniani kote hii biashara ni kongwe, ana miradi yake mikubwa anajimudu kukaa popote. Unafikiri kuwa na nyumba ndiyo kuwa na maisha mazuri?
Inaonekana we ndo mshauri wake au unamjaza ujinga nitajie listi ya matajiri waliopanga anza tanzania maliza na duniani.
 
Inaonekana we ndo mshauri wake au unamjaza ujinga nitajie listi ya matajiri waliopanga anza tanzania maliza na duniani.
Kupanga ni kuchagua. Ni maamuzi yake, wahindi wale miaka 30,50 wako bongo kwenye nyumba za NHC Upanga, kariakoo. Wanaishi mbona maisha yanaenda. Tuna ndugu toka anaanza maisha, kaanzia Upanga NHC mpaka leo mtu mzima, kaachia watoto. Nakuuliza kila mtu akijenga hii biashara itakufa na ni kongwe.
 
Kupanga ni kuchagua. Ni maamuzi yake, wahindi wale miaka 30,50 wako bongo kwenye nyumba za NHC Upanga, kariakoo. Wanaishi mbona maisha yanaenda. Tuna ndugu toka anaanza maisha, kaanzia Upanga NHC mpaka leo mtu mzima, kaachia watoto. Nakuuliza kila mtu akijenga hii biashara itakufa na ni kongwe.
Waindi ushawaita waindi kama kuna mswahili mwenye hiyo mentaliti ni hana akili ni sawa na kuacha kununua gari wakati uwezo upo una panda uber na daladala kisa tu umeamua maisha ya binadamu ni vitu 3 vya msingi Mke/Mume (2)nyumba yako (3)usafiri wako huyo jamaa yako ni chokoraa mwenye hela ni hana akili.
 
Kupanga ni kuchagua. Ni maamuzi yake, wahindi wale miaka 30,50 wako bongo kwenye nyumba za NHC Upanga, kariakoo. Wanaishi mbona maisha yanaenda. Tuna ndugu toka anaanza maisha, kaanzia Upanga NHC mpaka leo mtu mzima, kaachia watoto. Nakuuliza kila mtu akijenga hii biashara itakufa na ni kongwe.
Ila kwa maisha yetu ya kibongobongo kama uchumi wako ni wa kawaida ni bora ukajenga.
 
Nilikua kwenye nyumba ya kupanga, nzuri tu. Tatizo mwenye nyumba akapandisha bei kwa asilimia zaidi ya 25, bila taarifa mapema.

Nikaona sio shida, nikahama mkataba ulivyoisha. Sasa katika harakati za kutafuta nyumba, kuna vitu nimejifunza na vingine nimeshachelewa nimejikuta najuta tayari niko ndani.

Baadhi yake:

1. Usikae na mwenye nyumba.

Nilipokua zamani nilikua sikai na mwenye nyumba. Anakuja mara chache sana. Ila sahivi nimeyatimba.

Hafu mwenye nyumba ana shughuli kila siku, mazingira yapo ovyo wala sio masafi kwasababu yeye tu ana ndugu zaidi ya 8 na watoto, ukijumlisha mnashare uwanja, aisee.

2. Jitahidi msiwe mna-share bili/matumizi ya maji au umeme.

Iwe na wapangaji wenzako au mwenye nyumba, jitahidi sana ulipie bili mwenyewe.

Ikitokea umebanwa sana bdsi angalau muwe wawili mwisho. Sub-meater hazitasaidia kitu. Mtatoa kila mtu 20,000/= ya umeme kwa mwezi wewe unashinda kazini ukirudi unawasha feni tu, kuna sista duu anachemsha maharage kwa presha cooker.

Lazima mtagombana tu.

3. Hakikisha nyumba imekamilika ujenzi, asikudanganye lipia tu namalizia wiki ili kuweka madirisha sijui.

Unavyoenda kukagua eti nyumba haijakamilika choo au dirisha, akasema lipia namalizia mtego huo.

Ukishalipia tu imeisha. Utakuta jikoni hakuna sink, feni ya sebuleni haweki, na ata maji unaweza kuta akachelewa kuyaingiza.

Jitahidi uende nyumba iliokamilika kila kitu.


4. Kama una gari, angalia upatikanaji wa funguo za geti.

Otherwise utajikuta unawahi kurudi kuogopa kufungiwa geti kama mtoto. Zamani nilikua ata saa 8 usiku naweza kutoka sahivi nawahi home saa 4 wasije funga geti. Nishalalamika ila ndio ivo, kila siku ahadi hewa.

5. Zingatia idadi ya wapangaji wenzako.
Kama unaweza, jitahidi wapangaji muwe wachache. Mkiwa kikosi kuna faida na challenge zake. Faida moja wapo unaweza pata mke hapo hapo. Ila hasara unakuta challenge hadi kwenye kamba za kuanika mfano weekend mkifua wengi kwa pamoja, makelele kila mtu akiweka singeli nk.


6. Uliza kuhusu utaratibu wa bili za maji taka, takataka/usafi na ulinzi shirikishi.

Hii michango haiwagi mikubwa ila nayo ni kero.
Kuna hii ya maji taka kuyatoa kwasababu shimo limejaa, michango ya wale wazoa takataka na ulinxi shirikishi.

7. Zingatia msimu wa mvua kunapitika? Mafuriko na nyumba kuvuja?

Kuna nyumba msimu wa mvua hazifikiki sio kwa gari wala kutembea, pia kuna uwezekano mvua ikinyesha nyumba ikawa inavuja.

8. Kelele/mishemishe za majirani.

Unaweza ukawa umeenda kucheki nyumba ukakuta pako cool, kumbe jioni kuna bar uchwara inapiga music usiku kucha.

Au ukakuta weekend au jioni ni nyumba za ibada wanatumia maspika ww unasema unapumzika wao wakakiwasha.

Edit:

9. Uchumi ukiruhusu tafuta chumba chenye choo ndani.

Kama uchumia na mazingira yanaruhusu, epuka nyumba zenye vyoo vya kushare. Kuna watu ustaarabu mdogo sana .

Kwa sasa nimeyatimba, ila kutaka kuforce kukaa Makongo Juu kumeniponza. Nikimaliza Kodi yangu naamsha.
Bill ya maji ni shida, mpaka leo tuna mgomo wa kulipa maji kisa kijana wa mwenye nyumba anaedit sms za dawasco kisha analazimisha tulipe… 😅
 
Back
Top Bottom