Kama uzinzi huleta umasikini, mbona kuna watu ni wazinzi wana maisha mazuri kiuchumi?

Kama uzinzi huleta umasikini, mbona kuna watu ni wazinzi wana maisha mazuri kiuchumi?

Wanasema ukiwa mtu wa kutembea na kila mwanamke unajiletea mabalaa/mikosi wakimaanisha unakaribisha umaskini kwenye maisha yako, mbona kuna watu nawafahamu ni wanabadilisha wanawake kila kukicha, miaka nenda rudi, ila bado kipesa wako vizuri, na navowafahamu pesa zao si za kishirikina.

Hio stereotype imetoka wapi
Kitu chochote kikisemwa sana jua kinaukweli, jambo lolote lina kanuni ya muda kuleta matokeo hivyo hao unaowajua wanafanya uzinzi na Bado wapo vizuri kiuchumi wape muda utapata majibu baada ya kuanza kushuka kiuchumi.
nakubaliana na wewe mkuu


Sex is overrated,zinaa sio nzur mbali na kupoteza fedha na muda…inavutia majanga pia kwenye maisha na kizazi chako…moja kat ya kaz kubwa tunapaswa kuifanya binadamu n kujizuia,kujitawala,kujithibiti na kujiweza….
Kuna muda,jipe muda kama siyo yeye hata kizazi chake hakitakuwa salama.
Kufanikiwa au kutofanikiwa kwa mtu haina mahusiano yeyote na dhambi zake na sio uzinzi tuu, ni haina mahusiano na dhambi yeyote ile.

Dhambi au matendo mema ni kwa ajili ya kuonesha utii kwa Mungu, upendo kwa Mungu, binadamu na jirani na mwisho ni kwa ajili ya mbio za uzima wa milele pekee, HAKUNA CHA ZAIDI YA HAYO.

Mungu sio mjinga namna hiyo, hata kwa logic ya kawaida tuu, ingekuwa kufanikiwa kwa mtu kuna mahusiano na dhambi zake (mf uzinzi), basi binadamu tungekuwa wanafiki sana na tungempenda Mungu kinafiki tuu, yaani tungetii maagizo ya Mungu na kuacha dhambi ili tufanikiwe kwenye mambo yetu, NA SIO KWA SABABU YA UPENDO WA DHATI KWA MUNGU, kiifupi utii wa amri za Mungu ingekuwa ni kwa ajili ya kufukuzia mafanikio ya kidunia tu basi, kwani ni nani asiyetaka maisha mazuri ya mafanikio hapa duniani ?, hivuo formular ya hayo mafanikio ingekuwa ni kutofanya dhambi basi.

Binafsi nawakubali sana na kuwaamini matajiri wacha Mungu, wacha Mungu wa kweli walio-masikini ni wachache sana, wengi wao ucha Mungu wao ni kwa ajili ya mafanikio kwenye mambo fulani fulani ya kidunia sasa Mungu sio mjinga kiasi ichoo.
 
nakubaliana na wewe mkuu


Sex is overrated,zinaa sio nzur mbali na kupoteza fedha na muda…inavutia majanga pia kwenye maisha na kizazi chako…moja kat ya kaz kubwa tunapaswa kuifanya binadamu n kujizuia,kujitawala,kujithibiti na kujiweza….
Majanga hayana mahusiano yeyote na dhambi za mtu, labda yawe ni matokeo ya kanuni zingine za kimaisha ila sio kiroho. Matendo mrma au dhambi ni kwa ajili ya upendo wa dhati kwa Mungu, utii kwa Mungu, upendo kwa Binadamu na jirani na mwsho ni kwa ajili ya mbio za uzima wa milele. NA SIO MAJANGA AU MATATIZO YA WATU.
 
Pombe,wanawake,gari ya mjerumani aisee hivi vitu vinamaliza pesa
 
Ufahamu wako ulipoishia ndo na akili yako ilipoishia, lakini ili uzidi kupata maarifa inapaswa ujifunze mambo na sisi tunaomtegemea Mungu uombe na msaada wa kiroho ukufunulie inavyopaswa kuwa.

Hapa tunasema tabia ya uzinzi na upande mwingine wa kiroho inakuwa dhambi inashusha mafanikio ya uchumi ndo ilivyo, hatushindanishi akili za Mungu kwenye hili, tunachosema nikwamba uzinzi umechukuliwa kama uchafu wa kiroho na uchafu wa kiroho unaleta tabia mbaya kwenye mwili zinazozuia mambo yako ya kiroho kwenda vizuri, matokeo ya dhambi yanakuwa effect kwenye tabia ya mtu, Sasa mtu anapenda uzinzi huku unachafua roho na kimwili anakuwa na tabia mbaya zitakazoathiri maisha yake, imagine uishi kwa kutapanya mali iliyochumwa labda na wazazi au hata wengine wametapeli mihela mingi ukatumie kujiangamiza.

Kingine hicho Cha kubarikiwa waovu na watu wanaofanya mema Hilo lipo mikononi mwako, Mungu aliweka kanuni za kila mwanadamu za mafanikio na mafanikio ya mwanadamu yanaanza kwenye asili yake yaani ukoo wake, mali na urithi mtu hurithi kwa babaye hivyo mali zipo kwenye ngazi ya asili, na tabia ndo inayomhusu mtu kama mtu na Mungu wake, hivyo waovu na wema wakifata kanuni wanapata mali, haya tunaambiwa ushike sana ulichonacho asije mtu akakunyang'anya, hapo ndo tunaona hiyo dhambi ya uzinzi kwa vile inaathiri tabia itakufanya utapanye ulichonacho Sasa unavyovingapi? Vya kutapanya hovyo? Au unatapanya utajiri wa kizazi chako utacholeta duniani?
 
Back
Top Bottom