Kama Wakenya wameweza, sisi tunashindwa kwenda kujifunza kwao?

Kama Wakenya wameweza, sisi tunashindwa kwenda kujifunza kwao?

Acha utani mkuu[emoji3]
Sio inasemakana. Mpaka sasa hivi soko la mazao ya Tanzania liko Kenya. Pia hata soko lenye bei nzuri ya madini kuanzia Tanzanite mpaka dhahabu liko Kenya. Pia hata mafuta ya Alizet yananunuliwa kwa wingi na Kenya kisha kule yanafanyiwa pakeging na nembo za Kenya yanasafirishwa nje. Kwa ujumla Kenya wametuzidi ktk mambo mengi. Kikubwa hata elimu wametuzidi.
Wametuzidi wakati hawawezi kula bila sisi?
Kenge wewe
 
Tushaanza mkuu siku hizi lesseni unaomba kwenye mtandao,kufungua kampuni unaomba kwenye mtandao ...sawa zipo changamoto mblmbl ndogondogo tena za mtu mmoja mmoja hazikosekani ndio maana ya vyombo vya sheria au viongozi wetu wapo......niseme ukweli Uongozi uliopo umepania kweli watanzania tutoke kimaisha ila hatuwezi kutoka kwa kukaa kulia lia tu hakuna pesa rahisi ingekuwa hivyo kila mtu angekuwa Bhakresa ( nimetoa mfano) ...pence changamoto wajasiriamali tukae tujadili...labda nikuulize wewe ni mwanachama wa chama cha wafanyabiashara hapo ulipo? yaani TCIA? huko watakupa A B C ya haya maswali yako.Raisi wetu SSH anasema kila nchi ina utamaduni na historia yake hatuwezi kutumia utamaduni wa wenzetu kufanikisha ya kwetu hilo la msingi sana ...utamaduni wa kutomuabudu mzungu bali kumheshimu kama binadamu mwenzetu na ndio maana kwao kuna ukabila kwetu hakuna ...hivyo nasi tuna mazuri mengi tu ....tupambane tuache lugha za kukatishana tamaa maisha hayajawahi kuwa mepesi ...na kila leo ni mpya hivyo kujifunza ni muhimu
Nakubaliana na wewe kwa baadhi ya hoja zako
Ila la kulia lia hapana
Kweli kila nchi ina tamaduni zake lakini kwenye biashara nafikiri wote tuanongea lugha moja kwani biashara zilianza zamani sana Kama Silk Road
Toka China mpaka India mpaka Africa wote lugha moja ya biashara
Leo tumepata mazao mengi kutoka nje ambayo yalikuwa sio asili yake Africa bali yameletwa na watu, na sisi pia ya kwetu iwe mbegu, wanyama na hata ndege wamepelekwa sana nje ya nchi

Hakuna anaekata tamaa mkuu bali ni lazima kuwe na sheria zinazoeleweka na pia ukihitaji kujua kitu ufikie sehemu haraka na kujua bila kuzungushwa kwa uroho wa baadhi

Mimi nina kazi yangu na pia ni mfanyabiashara nje ya nchi
Nina tamani sana kupata bidhaa toka nyumbani maana tunaelewana lugha na ni rahisi kujua vingi
Kuna wakati nilikuwa nahitaji Vanilla pods na nilikuwa na soko ingawa mpaka sasa ninalo ila sio kubwa
Nikatafuta wauzaji nikakosa grade I na bei wanapanga hovyo hivyo nikaamua kuingia kwenye mtandao Madagascar. Nilipata kampuni moja genuine nakuwasiliana nao na kununua bila mimi kwenda nikapokea mzigo wangu hapa nilipo hao ni wahindi Madagascar
Sio kupenda wazungu au wengine hapana wao wako straight ana biashara unajiridhisha unasoma profile ya kampuni na kujua kama ina sifa basi
Siku hizi unaweza fanya biashara ya moja kwa moja na hata bongo zipo ila tunataka uaminifu zaidi na waache tamaa
Ukitaka leo gemstones ukiuliza tu tayari unaambiwa yapo jichanganye sasa
Mkuu changamote bado nyingi ila tunajivuta sana

Yapo mapungufu mengi na tunakatishana tamaa
 
Hebu tuchukue kweli matatizo yetu A % yamesababishwa ba CCM kama unavyosema Au pia tuchukulie B % zingine ni matatizo waliyotaja wengine kama elimu,afya ,nk je ni watanzia wangapi leo hii wana uhakika wa kula,kusoma,malazi na kupata huduma ya afya? ...Je wote wanaji shughulisha na nini? Wamesomea? Wana vyeti? Leseni? ....Ninachotaka kusema ni kwamba kumbe tunaweza kuishi hata kama kuna chama kibaya lakini muhimu watu wapate mambo ya msingi manne 1.Chakula 2.Afya 3.Malazi 4.Elimu ....halafu mtu ukaweka nguvu kwenye eneo lako ulilosomea iwe. Kilimo,biashara au ajira ukafuata taratibu zote za nchi fanya kwa bidiii tena ukiomba Mungu wako kila wakati na uhakika utafanikiwa ...tuache kulaumu kuongoza ni kazi jamani ...ni kipaji kwanza..Watanzania tunakosea padogo kusifia sana wenzetu ( hata kama hatujui changamoto zao) kama vile sisi ni mazuzu vile...jamani mimi nakataa nina akili nzuri tu naweza kufanya anachofanya mkenya,mzungu nikiamua.
Mkuu umewahi kuagiza mizigo kwenye malori na ukafika salama kila wakati?
Unaagiza mzigo packaging kwanza umefungiwq yale maboksi waliopokelea wao mizigo wakayachana halafu unafungiwq na katani huku bidhaa zinafika bolt zimemwagika kwenye lorry
Yaliyonikuta huko ni mtihani labda hujaingia kwenye biashara
Sio tunawasifia wazungu hilo neno usilitumie sana kwani tunajua fika wako mbali
Kuhusu elimu sio kila kitu elimu kubwa bali kuna mambo mengi binadamu tunafanya
Kwanza tuwe wachapa kazi na kuaminiana maana uaminifu ni muhimu sana halafu ukweli pia
Sisi wengi ni waizi, uaminifu zero, uongo na ujanja kwenye biashara hata makazini ni kawaida
Sasa nikisema ukweli hapo utasema nisilie hovyo hapana mkuu
Pia uongozi unasema ni mgumu
Sawa lazima uwe mgumu kwa sababu anategemewa mmoja tu aongoze lakini cha muhimu tunachoshindwa ni kufuata Sheria kama zilivyotungwa
Namuona Waziri wa kilimo anamuhoji Afisa wa kilimo anaeishi mjini wakati kapangiwa kazi kijijini tangu 2012 yupo mjini anakula mshahara tu
Sasa mimi nisilalamike nimekuwa nani
 
Wakenya ni aggressive sana kwenye biashara, pia lugha na elimu yao bora inawapa ujasiri wa kuingia popote duniani.
 
Ishu ni Ujuzi, mtaji, connection ya hayo masoko na mifumo ya serikali ndio inakwamisha
HILI NDILO TATIZO LA SEREKALI YENYE WATUMISHI WENYE URASIMU MKALI NA RUSHWA, WATUMISHI WAKE HAWAKO KATIKA KUSAIDIA AU KUWEZESHA BALI WAPO KWA KUKWAMISHA ZAIDI. (Roho mbaya tu)
Wakati mwingine si vibaya kuwashawishi wakenya hao kufungua makampuni hayo hapa Tanzania, hii itasaidia kuwapa ujasiri watanzania wengi, kuyavuta hapa ni kimkakati tu.
 
Mkuu usiwaone wakenya wanakuja wale hawaji na lakisaba [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]. Wale wamejipanga ohoo! Ngoja nikuelezee. Kuna jamaa yangu alikuwa kwenye hizo ishu alinipaga ufafanuzi wakina. Ngoja nieleze kwa urefu, samahani kama nitakosea (spellings natype fastafasta).


1. Kwanza ili uweze kuexport vitu kwenda soko la Ulaya, Marekani, Uarabuni, UAE, Dubai, Saudi Arabia. Lazima uwe na vibali ambavyo vinalipiwa pesa, uwe na vibali vya ubora kama ISO standards,EU standards, Halal standards. Hapo pesa inahitajika

2. Uwe na mtaji wa kununua mazao na kusafirisha mazao mpaka sehemu husika. Hapo pesa inahitajika

3. Uwe na eneo ambalo linakidhi ubora wa kimataifa kwa ajili ya packing, wafanyakazi, mitambo ya packaging. Maana yake ama ujenge kiwanda au ukodi jengo lenye vigezo ndio uanze uzalishaji. Na ili upate certificate ya kimataifa inabidi jengo liwe lako sasa piga hesabu ya kununua kiwanja cha Light industry au heavy industry mpaka unapata hati ya kiwanja ushatoa rushwa mpaka umechoka [emoji1787][emoji1787], kujenga jengo kwa designs,michoro na ubora wa kimataifa EU,USA, ISO standards ni pesa [emoji1787], kuvuta umeme hapo ni kuwapa rushwa tanesco mpaka wakuletee umeme umeshachoka [emoji1787][emoji1787], kuweka mitambo hapo kutafuta mitambo inayotoa bidhaa yenye ubora wa kimataifa na mpaka uitoe mitambo bandarini ushatoa rushwa ya kutosha [emoji1787][emoji1787], kulipa wafanyakazi ambao wana ujuzi wa kuzalisha bidhaa yenye ubora wa kimataifa sio kulipualipua[emoji1787] , mpaka kufikisha ubora wa kimataifa umechoka[emoji1787][emoji1787][emoji1787]. Hapo ni pesa tu inahitajika

4. Uwe na uwezo wakutafuta container special la kusafirisha mazao na kulipakiaa ama kwenye meli au ndege. Hapo ni pesa inahitajika

5. Uwe na connection ya upande wa pili wa unakopeleka na hao unakoexport lazima uwalipe. Na mzigo kufika mpaka kwa mteja lazima ulipe. Hapo pesa inahitajika

6. Uwe na pesa ya marketing ya bidhaa unayozalisha, na kuhudhuria international exhibition mara kwa mara ili kupata wateja wakubwa. Hapo hela inahitajika.

7. Bado kuna kulipa kodi na usafiri wa pande zote mbili, nchi unayotoa mzigo na unakopeleka, hapo kwa Tanzania mpaka uzungushwe na kusumbuliwa kweli kweli [emoji1787]. Na Hapo hela inahitajika.



Baada ya harakati zote hizo ndio sasa unaanza kuingiza hela.

Huo mchakato wa kuzalisha bidhaa za kuexport unataka hela na ubora wa kimataifa. Ukifanya kosa moja TU umekula hasara. Mzigo kama hauna ubora wa kimataifa unatupwa. Huko wenzetu wako very serious, sio huku ukitoa rushwa mzigo feki unavuka [emoji1787]

Ndio maana matajiri wa kibongo hawapo kwenye viwanda vya kuexport vitu kwenda soko la kimataifa. Wao wapo kwenye biashara za kuagiza vitu dubai,china, uturuki. Weka kwenye stoo na madukani unauza unapata hela bila usumbufu. Au wanajenga mahoteli na mabar mkalewe humo na kuzagamuana humo wao waingize hela. Au wanajenga sheli, mkaweke mafuta waingize hela fasta. Au wanajenga shule, mlipie ada watoto wao waingize hela. Au wananunua malori na macontena na mafuta, yapige safari za Congo, Zambia, Rwanda, Burundi, waingize hela. Au wanaweka viwanda vya unga wa ngano, juisi, energy drinks, pombe, mnunue mnywe/mle waingize hela. Au wananunua mabasi ya mkoani, weka nauli pandeni safirini, wao wanaigiza hela.

Sekta ya kuexport vitu sio rahisi kama unavyofikiria. Hao wakenya wamejipanga na ni wazoefu. Msiwachukulie poa.
Sahihi
 
HILI NDILO TATIZO LA SEREKALI YENYE WATUMISHI WENYE URASIMU MKALI NA RUSHWA, WATUMISHI WAKE HAWAKO KATIKA KUSAIDIA AU KUWEZESHA BALI WAPO KWA KUKWAMISHA ZAIDI. (Roho mbaya tu)
Wakati mwingine si vibaya kuwashawishi wakenya hao kufungua makampuni hayo hapa Tanzania, hii itasaidia kuwapa ujasiri watanzania wengi, kuyavuta hapa ni kimkakati tu.
Uoga na uchawi wa watz wenyewe,kwani wakenya wanategemea Serikali.
Mwenye Nia akwamishwi,mbona wapo wabongo kibao wanafanya export kupitia Serikali hii hii
 
Wabongo hawajawekeza sana kwenye exports industry zaidi wamewekeza kwenye import industry
 
Uoga na uchawi wa watz wenyewe,kwani wakenya wanategemea Serikali.
Mwenye Nia akwamishwi,mbona wapo wabongo kibao wanafanya export kupitia Serikali hii hii
Kwa aliyefanikiwa akiusema ukweli wake na njia alizopita mpaka kufanikisha utabaki mdomo wazi, kwa tanzania sio rahisi.
 
Kuna wakati Kikwete aliishia kutuma vijana wakajifunze namna ya kufanya packaging ya bidhaa zetu
Ila tatizo la mswahili huwa hamalizi alichoanza hata siku moja kiufupi huwa wanaangalia nini wananchi wanaongelea halafu wanalianzisha linaishia katikati maana hawqjui kuendeleza

Kweli ukiangalia hata mizigo inayopelekwa mikoani kupitia malori tu au train jinsi walivyo pack utalia ni vurugu
Yaani unaagiza mzigo wa nguo unaweza kukuta spana ya gari imo ndani kisa mzigo wa mwingine wa spea umefumuka
Tunaweza ila je tuna matunda na mboga mboga za kila msimu?
Huku wanataka mzigo anakupa wiki Tatu in advance na uwe haujaharibika na unaweza kukaa kwa siku hata tano bila kuharibika kwa sababu ya masoko

Tunahitaji umwagiliaji sana bila kutegemea mvua kama tuna nia ya kuuza nje
Huku hawanunui kwa msimu wanaletewa kila siku kwa ndege

Ndio maana unaona jirani wanakuja kununua kwetu wakiwa kwao msimu tofauti
Hata SA wananunua sana parachichi kutoka kwetu na kuyauza ulaya kwa sababu lazima wakidhi mahitaji ya kila siku ya ulaya

Kuna tende fulani zinaitwa Majhul zilianzia Morocco na sasa wanazalisha mpaka USA na Saudia na Israel
Yaani ni tende kubwa sana na ni tamu pia
Sasa SA kajiongeza zipo sokoni hapa na nimetoa order yangu kwenda kuuza hapa hapa
Nafikiri na wao wameanza kuzalisha huko
Dunia ya leo kila mmoja anapata faida kubwa kwa chakula na sisi ardhi tunayo

Leo kuna shamba la ndani ya sehemu kubwa Los Angeles ambapo wamepanda kila kitu na hawahitaji ardhi bali ndani ya jengo kubwa wanapanda kila kitu

Sisi tunajivuta kwa mambo mengi sana yaani akili yetu especially tz naona inakuwa taratibu sana au viongozi hawataki maendeleo
Umasikini ni faida kwa ccm
 
Hata Israel walishawahi kuja SUA kujifunza kilimo lakini sasa hivi Tanzania ndio tunaenda kwao kujifunza kilimo cha kisasa my country.
Chai hii! Walikuja lini SUA kujifunza kilimo cha kisasa? Acha uongo sema walikuja kutuelekeza namna ya kufundisha kilimo.
 
Waziri wa mipango na uwekezaji alikuwa mkufunzi wa elimu na saikolojia!
 
Ni watu hatari sana hao, usithubutu kukaa na mkenya ukafanya nao makubariano nao kibiashara,watakupiga tu.
Pia kutafuta biashara za nje ni rahisi sana. Tatizo linakuja kwa nchi yetu,viongozi wa nchi hii ni kama hawataki Watanzania wainuke kiuchumi. Kwanza ukitaka tu kupeleka bidhaa kama hizo nje ukiritimba unaanzia hapa. Itatakiwa vibali vingi uvilipie. Kwa hiyo mwisho watu wanakata tamaa kufuatia ukiritimba uliopo.
Lakini huko nje soko ni kubwa sana la mazao,shida mpaka wewe kupata hivyo vibali vya export ndio pagumu. Wenzetu Wakenya wamerahisishiwa na wanasaidiwa na serikali mtu akijitokeza kutaka kufanya hivyo

Tulipata soko la nanasi mpingo nje, ile nchi nanasi zake mbaya hazina ladhq vidogoo vya njano!! Tulipopeleka sample yetu walizipenda saana!! Shida ikaja kwenye vibali mara rushwa mara utaratibu tulishindwa sisi!! Ila wakenya wananunua wanabrand kwao wanapeleka kwa urahisi saana!!

Tanzania huwezi kutoa biashara kupeleka nje, we tafuta ujanja wako toka nje nunua matakataka lete Tanzania uuze....!! Simple!

Hii nchi tungeamua kuwa serious kidogo tu, hakuna kijana angekosa kazi!! Midege na mimeli ya biashara ingemwagika nchini hatari!!

Watu wanalima wanakosa soko, ukisema usafirishe nje shida! Aliyetulaani alishakufa
 
Kuna haja ya kuwa na kampuni ambayo italipia vibali vyote na kusimamia ubora wa bidhaa na kutafuta masoko ya nje. Commission % inakuwa source of revenue.
Ni watu hatari sana hao, usithubutu kukaa na mkenya ukafanya nao makubariano nao kibiashara,watakupiga tu.
Pia kutafuta biashara za nje ni rahisi sana. Tatizo linakuja kwa nchi yetu,viongozi wa nchi hii ni kama hawataki Watanzania wainuke kiuchumi. Kwanza ukitaka tu kupeleka bidhaa kama hizo nje ukiritimba unaanzia hapa. Itatakiwa vibali vingi uvilipie. Kwa hiyo mwisho watu wanakata tamaa kufuatia ukiritimba uliopo.
Lakini huko nje soko ni kubwa sana la mazao,shida mpaka wewe kupata hivyo vibali vya export ndio pagumu. Wenzetu Wakenya wamerahisishiwa na wanasaidiwa na serikali mtu akijitokeza kutaka kufanya hivyo
 
Hatuwezi, Tanzania ni kichwa cha mwendawazimu

Wakenya ni Wajanja, Wasomi na wana connections nje ya nchi yao

Pia Nchi yao ni rafiki na inawa favour wafanyabiashara ila Tanzania ni nchi ya hovyohovyo
 
Back
Top Bottom