Kamanda Lissu, Usisubiri Jibu la IGP Kuhusu Usalama Wako, Aliyekulinda na Shambulio Lile Yupo, Yeye Aweza, na Ataendelea Kukulinda, Welcome Back Home!

Kamanda Lissu, Usisubiri Jibu la IGP Kuhusu Usalama Wako, Aliyekulinda na Shambulio Lile Yupo, Yeye Aweza, na Ataendelea Kukulinda, Welcome Back Home!

Nakubaliana na wewe,Ila ninavyomfahamu huyu jamaa yetu ni bora shetani kuliko huyu.akija tu segerea inamhusu,Ila Kama anaweza kuandaa jeshi la kupambana na mtesi wake.

huyu shetani akiwa huko huko aliko mie pia ni mwanajeshi wake,bahati mbaya watanzania ulokole umetuzidi sana ndo maana sasa tunaongozwa na watoa roho za watu
 
Kwasababu wapo wanaomtuhumu kwa 'usalit'i, na kwa kadri nijuavyo kuhusu yanayowakuta wasaliti, na nilipomsikia mkubwa akisema "wasaliti tunajua tunawafanya nini"... Nashauri ndugu TAL abaki huko huko hata kwa miaka 5 ijayo. Mbinu inaweza kubadilika badala ya kuua mwili wataua akili

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu leo umeandika. Hongera sana. Ingekuwa siku zote tunaishi kama watu wa Mungu hivi sasa tungekuwa tuko mbali sana.

Kwa upande mwingine huyo YEYE ndiye anayetuonya tusijiingize kwenye maangamizo kwa mikono yetu i.e tuchukue hadhari kujikinga na madhara. Ningekuwa mimi ningejikinga kwanza baadae nikasubiri nguvu za YEYE.
Z
 
Mkuu Paskali, ungekuwa wewe ni Lissu Je ungetia mguu?
Angetia mguu in Msukuma na njaa yake bado ipo palepale. Wasiojulikana ni wauaji wa kulipwa (hitmen) ambao hulipwa baada ya kukamilisha kazi waliyotumwa. Mara zote watu wa aina hiyo huwa wana njaa Kali (siyo Pascal) ndo maana wanakubali kufanya kazi chafu kama hiyo na ikumbukwe ni miaka 3 sasa ya njaa.

Kama wangekuwa na uwezo wangemfuata wakammalize hukohuko Ubelgiji ili walipwe kitita kamili wangoje kazi nyingine kama hiyo. Wakristo tunaamini kuwa Yesu ni mwana wa Mungu na alikuja duniani kuwakomboa wanadamu lakini walio wake hawakumpokea badala yake walimuuwa Mungu Baba akiangalia.

Pamoja na ushauri mzuri wa mayalla, Mh. Lissu abaki hukohuko mpaka hali itakapokuwa muafaka maana waliotaka roho yake bado wapo na njaa yao. Mungu husaidia wanaojisaidia.
 
Watoto wa Lisu si wanasomeshwa na Acacia?

Wawe makini huko Ulaya maana Lisu amekubaliana na ushoga ,tusije tukaona picha wanaolewa

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app

Watoto wa viongozi karibia wote wamesoma na kusoma ulaya, hebu weka picha za mabwana zao hapa. Tena ukiweza weka picha ya Makongoro Nyerere na Januari tuwaone mabwana zao.
 
Lissu alipigwa Risasi na Bashite, spika anajua vizuri sana ndio maan wakamfuta ubunge.
Spika aliambiwa kabisa kuwa Lisu atapigwa risasi afe. Na ccm wote walikuwa wanajua na ndio waliratibu kila kitu.
Hata Paskali unajua vizuri sana na Watz wote wanajua hata ccm wanajua ndio mana wanendelea kumsimanga
 
Wanabodi,

Nimesoma mahali kuhusu Kamanda Tundu Lissu kuandika barua mbili kwa IGP kuomba kuhakikishiwa usalama wake ndipo arejee nyumbani Tanzania.

Mkuu Joka Kuu, asante kwa taarifa hii ya Lissu kuandika barua kwa HIP, kuhakikishiwa ulinzi na usalama wake kwanza ndipo arejee home, nyumbani Tanzania.

Hatua hii ni nzuri na muhimu sana ili angalau Lissu na dereva wake warejee nyumbani ili sasa ndio vyombo vyetu vya uchunguzi ndipo vianze kazi uchunguzi ya kuwabaini wasiojulikana, waliomshambulia Lissu, maana tangu ameshambuliwa vyombo vya uchunguzi vilishindwa kufanya uchaguzi wowote hadi wamhoji Lissu na dereva wake.

Jeshi letu la polisi ni jeshi lenye utu sana, baada tuu ya shambulio, polisi waliarifiwa within minutes, na kutoka eneo la tukio na kituo cha polisi ni just 10 minutes drive kutoka kituo cha polisi hadi kwenye crime scene, lakini polisi walifika baada ya masaa 2, wakakuta Lissu ameisha kimbizwa Dodoma hospital na hawakukuta mtu mwingine yoyote aliyeshuhudia, wala hakuna hata mlio wa risasi uliosikika.

Licha ya shahidi muhimu wa tukio hilo, dereva wa Lissu kutojeruhiwa na alikuwa available siku nzima, ila polisi wetu walingia utu na ubinaadamu wa kutochukua maelezo ili kumpa nafasi shahidi kupumzika na kupumzisha mawazo, watamchukia maelezo wakati wowote kwani maelezo yana haraka gani kuchukuliwa mapema huku watu wana photographic memory hata baada ya miaka 3, watakumbuka every details hata tiny details.

Lissu na dereva wake walipokuwa Nairobi ambapo ni karibu, jeshi letu la polisi liliingia utu wa kutowahoji ili kusubiria wapone. Walipokwenda Belgium kufuatia kule ni ulaya, na rais Magufuli hapendi safari zisizo za muhimu, kwa vile uchunguzi huo sio muhimu na hauna haraka, jeshi letu la polisi lilingia tena huruma kuwaacha hadi wapone na kurejea nyumbani Tanzania ndipo liwahoji na uchunguzi ndipo uanze.

Hivyo sasa wanasubiriwa kwa hamu Tundu Lissu na dereva wake warejee nyumbani nchini Tanzania ndipo uchunguzi wa tukio lile uanze.

To be honest, baada ya mimi kuangalia ile hard talk ya BBC, nilisema hivi
Kwa mliomsikia Tundu Lissu kwenye Hard Talk, unadhani atarejea nchini? Mimi sina hakika na akirejea, atakuwa ni shujaa kuliko hata Nelson Mandela! - JamiiForums

Hivyo Kamanda Tundu Lissu, Karibu Sana Nyumbani, huna haja ya kusubiri majibu ya Kamanda Sirro kukuhakikishia ulinzi wako. Yule YEYE aliyekulinda na kukuepusha na kifo licha ya kupigwa risasi 16, ni ulinzi mzuri kuliko Vijana wa Siro.

Kuhusu wale wasiojulikana waliokushambulia, according to postulates na theories mbalimbali kuwahusu wasiojulikana hao, japo malengo yao kwako hayakutimia, lakini sasa hata ukirejea, wasiojulikana wale, hawawezi tena kuikamilisha tena kuikamilisha ile kazi kwasababu kazi nyingine ni kama uchawi, mchawi ukiisha mshtukia, hakulogi tena.
Hitimisho

Kwa maoni yangu, namshauri Kamanda Tundu Lissu, kama ni kurejea tuu nyumbani, arejee tu nyumbani Tanzania wala asisubiri jibu la barua zake kwa IGP kuhusu kumhakikishia usalama wake, kwasababu kwanza just his survival is beyond human beings ability and capabilities, its Devine intervention hivyo Aliyemlinda na shambulio lile baya la kutisha na kusikitisha hadi kubakia hai Yupo, Aliyesimamia matibabu akatibiwa hadi akapona Yupo, Aliyeyafanya yote hayo ni YEYE Aweza, na Ataendelea kumlinda, Usikute yote hayo Lissu anayopitia, ni mapito tuu ili YEYE kuonyesha Uweza Wake, hata katika ukombozi wa Ulimwengu huu, ni kwa Kupigwa Kwake, sisi tuliponywa, hivyo at this juncture, Tundu Lissu hatakiwi tena kuendelea kutegemea uwezo wa binaadam katika ulinzi wa uhai na usalama wake, amtegemee YEYE. Tundu Lissu Atamke maneno haya, "NAYAWEZA YOTE KATIKA YEYE ANITIAYE NGUVU"

Welcome Back Home, Kamanda Mdogo wangu Lissu (mimi ni kaka yake kule shuleni Ilboru)

Mwacheni Mungu Atwe Mungu
Welcome back home Kaka Mdogo Tundu Lissu.
Mimi Kaka yako Mkubwa
Karibu Nyumbani.
Paskali.


Ila wasukuma mna roho ngumu sana
 
Pascal Mayalla, Mayalla jaribu kuvuta hisia tu kuwa siku moja ukasikia risasi 38 zinapigwa nje ya nyumba yako na wewe ukiwa ndani, achana na kukulenga bali zipigwe tu na baada ya muda zitulie kisha uambiwe toka nje.

Sent using Jamii Forums mobile app
achana na huyu jamaa, hajawahi hata kupigwa ngeta itakuwa bunduki ......

Yaani mateso yote hayo aliyoyapitia Lissu bado watu wanamfanya dhihaka...Kweli labda kama huyu Mungu wa Ibrahim na Isaka si Mungu wa kweli - lakini kama ni wa kweli aisee kuna watu watapata laana nzito ya vizazi na vizazi......
 
Paskali nakupa pongezi kwa bandiko lako refu. Mimi kama mimi nasema Tundu Lisu arejee nchini japo usalama wake ni mdogo. Najua kwa sasa atakaporejea si rahisi kuuwawa tena kwa mbinu ile, ila kitakachofanyika wale wenye ile dhamira wataagiza kesi zake zianze mara moja, ili afungwe kwani tayari wameshaandika hizo hukumu. Wasiwasi wangu ni pale Lissu atakapofungwa atakutana na mazingira gani huko jela, hasa ukizingatia ulemavu alionao.

Swali langu kwa mamlaka za nchi hii, kulikuwa na lawama nyingi za kuficha nia ovu shida ya shambulio la Lisu, walikuwa wanasema Lissu alipotishiwa kushambuliwa alisema kwenye vyombo vya habari na hakuripot rasmi polisi. Leo kaandika barua rasmi kwa IGP tena barua mbili lakini hajibiwi na wale waliokuwa wanasema hakuripoti kutishiwa kwake!

Kuna waliokuwa wanasema kuwa kutibiwa kwake hakukufuata utaratibu, wala hakuandika barua kumtaarifu spika kuwa yuko wapi, hivi sasa kaandika barua 2 kwa IGP, lakini hajajibiwa! Je kwa wale wenye shaka na malalamiko ya Lisu na wale anaowatuhumu kwa hiki kinachoendelea, watashindwa kuamini malalamiko ya Lisu na anaowatuhumu? Kuna sisi tunaondelea kuamini tuhuma za Lisu na anaowatuhumu, na haya yanayoendelea ndiyo yanakazia kile tunachokiamini.
 
Hatuwashangai nyie hata mikutano yenu hamuhitaji kuandika kuomba ulinzi kama vyama vingine. Bashiru analindwa na PLATOON nzima ya ffu sijui kwa lipi.
mugah di mathew,
Sasa kama kazi ya polisi inajulukana ni kulinda raia na mali zao, je Mh Lissu ni au si raia? kama ni raia, polisi itawandikia wangapi? au yeye tu?

Nadhani hela wanayo ila si ya kuandikia raia kuwajulisha kuwa wanawalinda!! Na zaidi mlinzi wa kweli ni YEYE yule aliemkinga na kile kifo!!
 
Back
Top Bottom