Kamati kuu CCM yamtosa Hussein Bashe, adaiwa si raia wa Tanzania

Kamati kuu CCM yamtosa Hussein Bashe, adaiwa si raia wa Tanzania

Baada ya kuona picha sasa ninadhani nimemkumbuka huyu bwana. Nadhani alisoma Mzumbe enzi za IDM kozi ya Busness Administration.

Sijui kama wanaweza fanana, lakini picha inanikumbusha kuwa ni yeye. Alikuwa rafiki mzuri wa mdogo wake na Edward Lowassa. Hebu wana Mzumbe watupe taarifa zidi.
 
:glasses-nerdy:tunakumbuka mambo ya saidi maulid kuwa siyo raia, na wachezaji wengine waliokuwa wakiambiwa kuwa sio raia mimi nilijua mambo haya ni kwa simba na yanga kumbe ccm wameanza kuyachukua mambo haya ya kijinga
 
bashe ni mtoto wa kitanzania alikumbwa na bahati mbaya ya kuzaliwa na wazazi waliotokea nje ya nchi....
 
,,,duu huyu dogo wamemuonea....nasikia chilligati ametangaza kuwa atavuliwa vyeo vyake vyote ....na hataweza hata kupiga kura ...nadhani wamembana ili asiweze hata kugombea kupitia chama kingine...unless aweze kuchalange hili suala mahakamani kabla ya uteuzi.....ni wazi safari yake kisiasa imefikia ukingoni......the like of balozi bandora,yule mwenyekiti wa ccm kagera -anatoli,jenerali ulimwengu,na yule mama wa uwt[forget the name].unless otherwise....huyu bashe alikuwa kwenye bifu kali sana na Rizwani....na katika siku za karibuni alikuwa anaonekana kupata nguvu sana!!!
 
bashe ni mtoto wa kitanzania alikumbwa na bahati mbaya ya kuzaliwa na wazazi waliotokea nje ya nchi....


ishu ya bashe na waziri mkullo haitofautiani...bashe kazaliwa na wazazi wasomali.....wakati huyu mkullo kazaliwa na wazazi wamalawi.....

ni double standards tu...mwakalebela anatuhuma ..ametupwa ...wakati mramba naye ana tuhuma pia amepitishwa........sijui inakuwaje haapa!!

wakati wa kura za maoni kuna waliotoa rushwa na kukamatwa...na kuna ambao walikuwa wanapewa ULinzi wa PCCCB ili waweze kugawa rushwa bila bugudha ....lol!!
 
Kwa jinsi nilivyokijua chama cha CCM, enzi hizo usipokariri vikao vya chama na wajumbe wake.... sahau kufaulu darasa la saba! Kweli mambo yamebadilika, sasa huyu si mtoto mdogo kabisa, hivi hata katiba ya chama anaijua kweli? Ambayo sisi wakongwe tulilazimishwa kuikariri hata kama hatuikubali? au ndio nguvu ya walichonacho?

Hata wapiga kura wa Nzega (shame on you) huyu mtoto alitakiwa awe chipukizi kwa miaka mitano ijayo kabla hata hajafikiria kugombea ujumbe wa nyumba kumi. Na ndio maana tunahitaji ku-retire the white elephant and whoever is associated with it.
 
Msisahau pia ni muajiriwa wa RA kama Circulation Manager wa magazeti ya New Habari. kabla ya hapo alikuwa ameajiriwa na magazeti ya Mwananchi kwa post hiyo hiyo lakini alifukuzwa, inasemekana alifukuzwa kutokana na kuhusishwa na genge la wizi wa magazeti.

Na hapo New Habari -- tangu aajiriwe, mauzo ya magazeti yamekwenda chini kiasi cha kutisha sasa hivi! Ni mtu wa RA bila wasiwasi wowote na kampeni yake kule Nzega iligharamiwa na huyo RA -- mamilioni ya kuhonga wapiga kura na Takukuru waliagizwa kutoingilia kutokana na agizo la RA. Mimi nafikiri kukatwa jina lake kumetokana na rushwa tu, siyo uraia. Uraia ni sababu tu, kwani wakisema rushwa watamhusisha RA pia.

Vikao vya CCM vimejaribu kuridhisha pande zote: Bashe (kwa kutoshitakiwa kwa rushwa na kutopitishwa hasimu wake Sellelii); na Selleli (kwa kutompitisha Bashe na pia kumpoza asiende Chadema.)
 
Aliyekuwa mgombea wa CCM ngazi ya ubunge huko Nzega ajulikanaye kama Hussein Bashe ametumuliwa uanachama. Kulingana na hatua hiyo Bashe kapoteza uongozi wa aina yoyote aliokuwa nao katika chama.

Kulingana na habari hizo, Bashe kapoteza uanachama kwa kuhofiwa kuwa si raia wa Tanzania. Maswali mengi yataulizwa, je ilikuwaje akafika hapo alipokuwa amefikia katika uongozi ndani ya CCM?

Haya tutasubiri habari zingine kutoka Immigration, kama kuna deportation process yoyote.
 
Bashe atimuliwa CCM
• Adaiwa raia wa Somalia, afananishwa na Ulimwengu

na Martin Malera, Dodoma

HALMASHAURI KUU ya Chama cha Mapinduzi (NEC), imemvua nyadhifa zote na kumfukuza uanachama kada wake maarufu, Hussein Bashe, baada ya kubaini kuwa sio raia wa Tanzania.

Bashe ambaye alishinda kura za maoni kwenye jimbo la Nzega lililokuwa likishikiliwa na Lucas Selelii, (CCM), pia alikuwa mjumbe wa Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) na mjumbe wa Halmashauri Kuu (NEC).

Akitangaza uamuzi huo juzi majira ya saa 11 alfajiri baada ya kumalizika kwa kikao cha NEC cha mchujo wa wagombea ubunge na Baraza la Wawakilishi, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Kapteni mstaafu, John Chiligati, alisema CCM imeamua kumtimua Bashe uanachama na kumuengua kuwania ubunge katika jimbo la Nzega, baada ya kubaini kuwa ni raia wa Somalia.

Alisema uchunguzi uliofanywa na chama hicho kwa kushirikiana na Idara ya Uhamiaji, umebaini kuwa Bashe licha ya kuzaliwa nchini, ni raia wa Somalia na hajaukana uraia wake.

“Bashe sio raia wa Tanzania, alikuwa akiishi kwa mazoea tu. Tulipojaribu kutafuta uraia wake kwa kuwashirikisha watu wa Uhamiaji, walituthibitishia kuwa sio raia, licha ya kuzaliwa nchini na alikuwa akiishi kwa mazoea tu. Hii ni kama iliyowahi kumtokea Jenerali Ulimwengu na ndivyo ilivyo kwa Bashe,” alisema Chiligati.

Akifafanua suala la uraia wa kada huyo wa CCM, Chiligati alisema Bashe alizaliwa nchini, lakini baba yake ambaye hata hivyo hakumtaja jina, alihamia nchini na kuukana uraia wake miaka 10 baada ya Bashe kuzaliwa.

Alisema licha ya kuwa baba yake alichukua uraia wa Tanzania, Bashe naye anapaswa kusaka uraia wa Tanzania, kwani kisheria haruhusiwi kurithi uraia wa baba yake.

Alipoulizwa kwa nini suala la uraia wa Bashe limeibuka kipindi hiki alichoshinda kura za maoni katika jimbo la Nzega wakati amewahi kuwania nafasi mbalimbali ndani ya chama ikiwemo nafasi ya Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Chiligati alisema safari hii chama hicho kimepokea malalamiko rasmi kutoka kwa mmoja wa washindani wa Bashe (hakumtaja jina), alidai kuwa kada huyo sio raia.

“Kama nilivyosema, alikuwa akiishi kwa mazoea, lakini safari hii tumeletewa malalamiko, tukayapeleka Uhamiaji, wakabaini kuwa kweli sio raia, tukaamua kumkata na kumvua nyadhifa zake pamoja na uanachama hadi hapo atakapoweka mambo yake sawa,” alisema Chiligati.

Msemaji huyo wa CCM alisema mbali ya Bashe, NEC pia ililetewa malalamiko dhidi ya Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkullo, Mbunge wa Kilosa kwamba naye ni raia wa Malawi.

“Kama ilivyokuwa kwa Bashe, tulipeleka suala hilo uhamiaji nao walipofanya uchunguzi, walibaini kuwa ni madai ya uongo. Kama ingekuwa kweli, tungechukua hatua kama tulivyochukua kwa Bashe,” alisema Chiligati.

Kutokana na hali hiyo, Chiligati alisema CCM imempa muda Bashe kuweka mambo yake sawa ili aweze kuwa raia wa Tanzania, arudishiwe uanachama wake na kupata fursa ya kushiriki kuwania nafasi mbalimbali za uongozi nchini.

Alipoulizwa kwa nini NEC haikumpitisha Selelii aliyeshika nafasi ya pili Nzega, Chiligati alisema Mbunge huyo wa zamani wa Nzega hakubaliki, kwani alipishana kwa kura chache sana na mshindi wa tatu, Hamis Andrea.

Kuhusu aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Soka Nchini (TFF), Chiligati alisema NEC imezingatia zaidi suala la maadili kwani ni sawa na mchezaji aliyepigiwa kipenga katika dakika ya kwanza ya mchezo wa soka.

Mwakalebela ambaye alishinda kura za maoni katika jimbo la Iringa Mjini, amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Iringa, akidaiwa kutoa rushwa wakati wa mchakato wa kura za maoni.

Alipoulizwa kwa nini Mbunge wa Bariadi Mashariki Andrew Chenge na Bazil Mramba wa Rombo, wamepitishwa kutetea nafasi zao wakati wanakabiliwa na kesi za matumizi mabaya ya madaraka kama ilivyo kwa Mwakalebela aliyedaiwa kutoa rushwa, Chiligati alisema wamezingatia maoni ya wanasheria kuwa kesi zao haziwezi kuathiri uteuzi wao.

“Chenge bado anatuhuma na hajafunguliwa kesi, Mramba ana kesi ya matumizi mabaya ya madaraka, nayo haiwezi kuathiri uteuzi wake. Mwakalebela ndio kwanza anaanza na rafu na kapigiwa filimbi ndani ya dakika ya kwanza, hapo tumeangalia maadili zaidi,” alisema Chiligati. Katika hatua nyingine, Bashe aliliambia Tanzania Daima jana kuwa anatarajia kuzungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, akiwa na vielelezo vinavyoonyesha kwamba ni raia wa Tanzania.


Source: Tanzania Daima.
 
Maelezo ya Chiligati hayajitoshelezi kuhusiana na kupitishwa kwa Chenge na Mramba. Hapo hakuna hoja ya msingi ya kwanini Mwakalebela aondolewe na hawa wengine waingie.
 
Ndani ya CCM na vikao vyake hakuna UHAKIKA.
WACHAKACHUAJI
 
Double standards! Ha ha ha! Ukimwangalia Chiligati na umri ule anayasema maneno hayo anatia hata aibu!
 
rostam_aziz.JPG





abood.JPG
 
Katika ujinga wa mwafrika kuna jambo moja ambalo tunaongoza na hilo ni kutotumia akili, na hili bado halijasafishika miaka nenda rudi.

Kwanza, katika hatua za kujiandikisha uanachama wa CCM jambo la "status" yake bwana Bashe halikuangaliwa mpaka mtu anafika katika nafasi ya kutaka kuwa mbunge?

Pili sheria gani inaruhusu watu walio na kesi mahakamani (mzee Mramba) na wale wenye tuhuma (mzee Chenge) waendelee kuhodhi nyadhifa zao au hata kuruhusiwa kugombe tena nyadhifa hizo?

Kesi za watu kama hawa zinaweza kabisa kuathiri utaratibu mzima wa kura za maoni na hata kura za ubunge ukizingatia kuwa kuna suala la ubadhilifu wa fwedha ambalo linawahusu wazee hawa.
 
keshafukuzwa na sasa abaki na biashara zake na aombe uraia... kwisha

CCM ni zaidi ya uijuavyo and no one is bigger than the party chairman

dogo sasa ndio atakua al shabab rasmi
 
CCM ina wenyewe Bashe alidandia train kwa mbele madhara yake haya! Alikuwa na bifu na akina Benno Malisa na Mtoto wa Mfalme Ridhiwani.....akiwa upande wa Masauni! Mzee Mzima Mwenyekiti alikuwa anamlia timings. Wamekula kichwa na anakesi ya uhamiaji. RA mbona si raia na anaendelea kutesa?
 
KUNA KITU HAKIENDI SAWA NDANI YA CCM NA HASA KATIKA SEKRETARIAT YAKE. TAZAMA HAYA:

-Chenge, Mramba, Blandes, wako mahakamani na wote tayari wameambiwa kuna kesi ya kujibu
-Mwakalebela anaondolewa kwa sababu ya kuwa mahakamani?!
-Mfanyakazi wa serikali akifunguliwa tu mashtaka anakuwa nje ya kazi mpaka kesi iishe
-Bashe anaondolewa kwa sababu za uraia, lakini mkoa mzima wa Tabora ukiondoa Samweli Sitta, umechukuliwa
na wasomali.

Muda umefika kwa CCM kuwa na independent body ya kuchuja wagombea, siyo hii NEC na CC ambao pia ni wagombea wanaowachuja wagombea wenzao.
 
Back
Top Bottom