Kamati Kuu ya CHADEMA, mkiteua wabunge wa Viti Maalumu kuingia Bungeni, mtakuwa mmefanya kosa kubwa sana

Kamati Kuu ya CHADEMA, mkiteua wabunge wa Viti Maalumu kuingia Bungeni, mtakuwa mmefanya kosa kubwa sana

That is not an offer , ni haki yao ya kikatiba , labda waamue kuiacha tu kwa sababu ya mikakati ya kisiasa , lakini hawajapewa na mtu , hii imepatikana kutokana na idadi ya kura za mgombea wao wa Urais
Hiyo "Idadi ya kura za Mgombea Urais" imetambuliwa rasmi na chama? Inakubalika?
Ikiwa chama kimekubaliana na yale matokeo ya kura alizopatiwa Lissu na ile Tume ya MFUKONI ya Jiwe, sisi ni akina nani tuendelee kujadili hili au kupinga?
 
waangalie wats best for chadema for the sake of chadema, hakuna mgomo unaoweza kumbadilisha jiwe na vyombo vyake vya maamuzi,
hvyo chadema wachangamkie fursa angalau wapate jukwaa la ajenda zao achilia mbali ruzuku kwa uendeshaji wa chama.
Kamati Kuu Ya CHADEMA Ipo Kwenye Kikao. Mjadala Mkubwa Ni Viti Maalumu. Je Wakubali Au Wakatae?

Unadhani Wakubali Kwa Msingi Kwamba Fisi Hasusiwi Bucha? Au Wakatae Kwa Msingi Kwamba Hawakubaliani Na Mchakato Mzima Wa Uchaguzi Na Matokeo Yake? Nini Maoni Yako?

Jadili kwa maslahi mapana ya Taifa, amani, haki na ustawi wa Demokrasia ya kweli nchini
 
Wakihalalisha haramu kuwa halali basi wajue CCM itarudia michezo hii tena na tena na wananchi watawaona kuwa ni chama cha ruzuku tu hakipo tayari kutetea principle zao!

Chadema hawawezi kudai eti bora waende bungeni na hivyo eti kwa uchache wao huo wakatetee wananchi!! , wakawatetee kwa nani?, yaani wakawateteee wananchi kwa serikali hii hii ya CCM iliyowapora uchaguzi waziwazi?

Chadema hawawezi kutangaza kutoutambua uchaguzi hakafu wakatoka hapo eti wanataka wanufaike na uchaguzi huo wasioutambua!

Kamati kuu isimame imara, ikikubali kuhalalisha ujinga basi nayo itakuwa jinga na haitokuwa na maana iwepo!

Na wawe makini na watu wa dini watakaotumwa kwao kuwalainisha ili walainike na pia wawe makini na ID za mitandaoni zitakazokuwa zikitumika kuwapa ushauri wa kukubaliana na haramu ile.

Chadema isimamie msemo wae wa Sasa basi, ili tuanze chapter mpya ya kudai tume huru ya uchaguzi na katiba mpya!
Wakawatete wananchi waliogoma kuyatetea maslahi yao? Wakatetee Maiti?
 
kwa mfumo huu wa sasa hata CHADEMA ikipata kura 99%
wataambiwa wamepata 15% tu

Kama Chadema inataka kujimaliza tena kwa aibu kubwa na pia wananchi waidharau basi ipeleke wabunge wa kupewa na NEC bungeni.

Struggle hapa ni tume huru ya uchaguzi na katiba mpya, na struggle hiyo haiwezi kupatikana katka bunge la CCM

Wananchi tuko tayari kuchangia chama kwenye struggle hiyo kwa senti zetu
Labda wananchi wa Dar...na majiji na manispaa...Sasa ndugu yangu hiyo elimu ya uraia hao chadema wataifikishaje kwa walengwa huko vijijini...fedha inaitajika..chadema hawana Strong source ya income zaidi ya ruzuku ya serikali.

Ukisema wanachama watachangia..wanaweza kufanya hivyo kila mwezi kwa miaka mitano...jibu la haraka haraka ni hapana...chadema wanamfadhili anayeweza kuwapa fedha kila mwezi zaidi ya milioni mbili kila mwezi kwa miaka mitano..jibu la haraka haraka ni hapana...chadema uwekezaji wowote unaoweza kuwapa fedha za kuendesha chama kulipa wafanyakazi wake na kufanya siasa kila mwezi kwa miaka mitano..jibu Ni hapana..Sasa chama kitaendelea kufanya siasa na kuwa hai kivipi..ndio hapo umuhimu wa ruzuku unaonekana.

Hao wabunge wakiwa bungeni pia hata Kama Ni wachache watawasemea wenzao na kukosoa serikali na kukisemea chama
 
waangalie wats best for chadema for the sake of chadema, hakuna mgomo unaoweza kumbadilisha jiwe na vyombo vyake vya maamuzi,
hvyo chadema wachangamkie fursa angalau wapate jukwaa la ajenda zao achilia mbali ruzuku kwa uendeshaji wa chama.

Kwani Chadema ipo kwa ajili ya nini?
Kushika dola au kula ruzuku tu, yaani wakishapata ruzuku yao huwaoni tena wakisumbua sumbua?

Kisha baada ya miaka mitano waje tena washiriki uchaguzi ili wapate ruzuku tu?

Hoja ya ruzuku ni kwa chama kinachofanya siasa za "siasa biashara", lakini kwa chama kinachosimamia principles hakiwezi kuhalalisha haramu iwe halali haafu kitegemee haramu hiyo itazaa matunda mema.

Jiwe anataka legitimacy kwa umma na jumuia ya kimataifa ili atawale smoothly, na Chadema wameshikilia kete muhimu katika hilo. Chadema wasikubali hilo, wapiganie reforms za msingi katika nchi
 
Labda wananchi wa Dar...na majiji na manispaa...Sasa ndugu yangu hiyo elimu ya uraia hao chadema wataifikishaje kwa walengwa huko vijijini...fedha inaitajika..chadema hawana Strong source ya income zaidi ya ruzuku ya serikali..ukisema wanachama watachangia..wanaweza kufanya hivyo kila mwezi kwa miaka mitano...jibu la haraka haraka ni hapana...chadema wanamfadhili anayeweza kuwapa fedha kila mwezi zaidi ya milioni mbili kila mwezi kwa miaka mitano..jibu la haraka haraka ni hapana...chadema uwekezaji wowote unaoweza kuwapa fedha za kuendesha chama kulipa wafanyakazi wake na kufanya siasa kila mwezi kwa miaka mitano..jibu Ni hapana..Sasa chama kitaendelea kufanya siasa na kuwa hai kivipi..ndio hapo umuhimu wa ruzuku unaonekana..
Hao wabunge wakiwa bungeni pia hata Kama Ni wachache watawasemea wenzao na kukosoa serikali na kukisemea chama
Chadema ina wanachama milioni 7, wanatosha kukiendesha chama kwa ada na michango mbalimbali.

Kukosoa serikali hii ndani ya bunge la CCM hakusaidii kwa sababu serikali hii haigopi tena ukweli wala haiheshimu tena wananchi.

Inabidi elimu ya uraia itolewe ili serikali ianze tena kuogopa wananchi na hivyo iweze kushinikizwa kupatikana kwa mifumo ya tume huru ya uchaguzi na katiba mpya.

Kuliko kuingia bungeni kuhalalisha haramu bora Chadema ife huenda hsta Hashim Rungwe Spunda akashika tochi ya kutafutia mabadiliko ya msingi katika nchi.

Chama kinachokubaliana na kudhulumiwa ili kipewe ruzuku siyo chama serious cha kushila dola!
 
Uingize watu bungeni kuhalalisha haramu?

Watu tayari wameshajua tofauti kati yao na CCM ndiyo maana watu wako na upinzani ila CCM wamefanya uharamia wa kutisha kwenye uchaguzi huu.

Sasa kwa nini ushiriki vikao vya wachawi ama wewe ni mtu safi?
Hivi unajua kama chadema watagoma means in five yrs chadema itakuwa iko kimya?
 
Chama siyo Saccos. Kujali ruzuku badala ya kutetea principles ni kugeuka kuwa chama "ruzuku". Chama cha namna hiyo bora kife kije kingine kinachopigania chaguzi za wananchi ziheshimiwe na tupate mifumo ya kuwezesha hilo. Unfortunately hilo haliwezi kuwezekana kupitia bunge hili la CCM.
Chama kiendelee kutoa elimu ya uraia kwa wananchi kuhusu umuhimu wa tume huru ya uchaguzi na katiba mpya, Wananchi wao wenyewe watajua cha kufanya come the day isiyo na siku wala jina.
Lakini CCM wakuibie Ngamia kisha wakupe sungura na wewe unapokea tu huo ni ujuha na wananchi wataidharau Chadema zaidi.
Yaani wakuvurugie uchaguzi wa wabunge na rais, kisha wakupe viti maalum halafu useme eti ukipiga kelele bungeni kutetea wananchi watajali, let me tell you one thing They care nothing kuhusu kelelekelele hizi za eti maslahi ya wananchi, wangekuwa wanaheshimu maslahi ya wananchi wasingewadharau wananchi kwa kuwaharibia uchaguzi wao!
CCM hawana mamlaka ya kutoa viti maalum. Hivi ni viti ( bila shaka wanastahili zaidi ya hapo) ambavyo ni stahili ya CHADEMA na vimetokana na kura walizopigiwa. Sio fadhila ya NEC wala CCM. Aidha ruzuku haitoki kwenye mfuko wa CCM bali inatokana na kodi ambazo wananchi wote wanachangia bila kujali itikadi yao. Sio fadhila, ni haki yao na wanastahili kulipwa ili waendeshe shughuli zao. Kusema kuwa wakipokea watageuka kuwa ni chama "ruzuku" ambacho hakijali "principles" ni upuuzi maana wakati hao unaowanyooshea vidole wanafilisiwa, wanapigwa, wanafunguliwa kesi za kutungwa, wanapofungwa, wanapopigwa mabomu, wanapodhalilishwa na vijana wadogo ambao madaraka yamewafanya wakose adabu, wanafukuzwa bungeni, wanapozuiwa kufanya kampeni, wanaponyimwa stahili zao n.k. wewe shujaa na wenzako kama wewe wenye "principles" hamkujitokeza kusimama nao.

Badala yake mnajificha kwenye majukwaa kama haya na kujimwambafai. Mngekuwa mnasimama nao toka mwanzo hali isingefikia hapa. Polisi wangejua kuwa wakimgusa mmoja wao kwa uonevu mngejitokeza kwa wingi, wangeacha kuwabughudhi. Mngesimama kidete kuhakikisha haki inatendeka kwenye vituo vya kupigia kura sio wasimamizi wala NEC ambao wangethubutu kufanya waliofanya.

Wakina Salome Makamba, Pendolino Peneza, Suzan Kiwanga, Nusrat na wengine wengi tu wametupwa ndani au wamenyang'anywa haki yao ya kugombea lakini nyinyi wenye " principles " ambao mko tayari kufia chama mliufyata. Waacheni ambao wameonyesha kwa matendo kuwa ni watetezi wa wananchi na chama chao wapewe nafasi ya kuendelea kufanya. Mkitaka wasifanye hivyo , nyie Great Thinkers, anzeni kuwaonyesha kwa matendo kuwa mko pamoja nao. Kama hamuwezi, nyamazeni.

Amandla...
 
Kususa kama chama itakuwa anguko kuwepo hata wachache bungeni sauti yao itakuwa muhimu japo watakuwa hawana meno sana,kutokupeleka kabisa wanajizika wenyewe kisiasa
Miaka mitano mmejiapiza kuwa Chadema itakufa itakufa sasa majuzi mmejionea kwenye mikutano ya Lissu. Msichoelewa ni kufikiri kwamba CHADEMA ni viongozi kumbe ni wananchi.
 
Wakihalalisha haramu kuwa halali basi wajue CCM itarudia michezo hii tena na tena na wananchi watawaona kuwa ni chama cha ruzuku tu hakipo tayari kutetea principle zao!

Chadema hawawezi kudai eti bora waende bungeni na hivyo eti kwa uchache wao huo wakatetee wananchi!! , wakawatetee kwa nani?, yaani wakawateteee wananchi kwa serikali hii hii ya CCM iliyowapora uchaguzi waziwazi?

Chadema hawawezi kutangaza kutoutambua uchaguzi hakafu wakatoka hapo eti wanataka wanufaike na uchaguzi huo wasioutambua!

Kamati kuu isimame imara, ikikubali kuhalalisha ujinga basi nayo itakuwa jinga na haitokuwa na maana iwepo!

Na wawe makini na watu wa dini watakaotumwa kwao kuwalainisha ili walainike na pia wawe makini na ID za mitandaoni zitakazokuwa zikitumika kuwapa ushauri wa kukubaliana na haramu ile.

Chadema isimamie msemo wae wa Sasa basi, ili tuanze chapter mpya ya kudai tume huru ya uchaguzi na katiba mpya!
[emoji106][emoji106][emoji106][emoji120][emoji120][emoji120][emoji122][emoji122][emoji122]
 
CHADEMA kwanza jiulizeni kwa nini CCM wanataka Aida aende Bungeni kwa nguvu? Wanataka kuwatumia nyie kuhalalisha udhalimu wao. Na mkikubali hata 2025 itakuwa hivyo hivyo. Jifungeni mkanda hivyo hivyo. Maalim aliweza kule Zanzibar (2015-2020) bila ruzuku lakini mmeona sapoti ya watu kwake mwaka huu. Kwanza mlishapoteza sapoti. Mshukuruni Lissu. Sasa kama mnataka hata hiyo imani iliyojengwa na Lissu ipotee, fanyeni ujinga wa kuweka njaa zenu mbele.
 
That is not an offer , ni haki yao ya kikatiba , labda waamue kuiacha tu kwa sababu ya mikakati ya kisiasa , lakini hawajapewa na mtu , hii imepatikana kutokana na idadi ya kura za mgombea wao wa Urais
Kura zipi wakati wamesema wameibiwa kura zao? Huwezi kusema umekamata kura feki halafu urudi tena useme nina kura halali za urais hivyo ni haki yangu kupata viti maalum. Yaani nyama ya nguruwe haramu lakini mchuzi wa hiyo nyama halali.
 
Back
Top Bottom