Kamati ya Mambo ya Nje ya Umoja wa Ulaya (EU) wataka kujua msaada wa Euro Mil. 27 za COVID-19 kwa Tanzania uliahidiwa kwa vigezo gani?

Viongozi wengi wa kiafrika hujikaanga wenyewe kwa kujitengenezea maadui wa ndani.Huo ndio mwanya wa mabeberu kufanya yao.RIP Thomas Sankara and the like.
 
Hii itaathiri sana maeneo mengi japo sehemu kubwa ya msaada huo umeshatumika.
Pia ipo mikataba ya utekelezaji wa misaada imeshasainiwa ambayo huwezi simamisha. Fidia ni kubwa ni bora wafunge macho.
Baadhi ya mikataba hiyo ni ujenzi wa barabara ya kidatu..ifakara kwa njia ya lami.
Mamlaka za maji,
Kulimo cha mbogamboga maeneo mengi nchini..nk
 
Corona ilikuwepo na kulikua nawagonjwa na kuna hospital zilitengwa kuwahudumia.
Vipimo vya corona vilinunuliwa na maabara ilitengenezwa.
Kuna waliokufa kwa corona pia na kuzikwa na serikali.
Kuna waliwekwa karantina wakiwemo WCB n.k
Baadae corona ilidhibitiwa na kupungua kisha kuisha, haikuendelea tena mpaka leo tunaendelea na maisha.
Sasa kwamba toka mgonjwa wakwanza wacorona anatangazwa hapa Tanzania mpaka inaisha hakuna fedha ilikua inatumika?

Sent from my Infinix X603 using JamiiForums mobile app
 
Direct and indirect tax,we unadhani tax ni direct taxi tu
Wewe unaleta nadharia na mimi ninakwambia kwa mujibu wa sheria...

Watanzania tuna mambo sana..Mbona tukisafiri ughaibuni tunakuwa Subject to Paying tax na hatulalami..

Ni takwa la kisheria kupeleka taarifa zako za mapato TRA. Wao ndio watakwambia kama unapaswa kulipa kodi au hapana.. wakisha kukukagua.

Ili uweze kufanya hilo, au kutimiza takwahilo kisheria inahitaji kuwa na namba ya utambulisho wa mlipa kodi.

Leo unaweza kuwa huna mapato mengi ya kutosha kukufanya ulipe kodi kwa mujibu wa sheria na kanuni zinazoendesha TRA ila we hope for the best kesho utafanikiwa na itakubidi ulipe kodi.

Swala indirect na direct hilo sioni linaingia wapi hapa.

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Lakini EU lazima wajue kwamba hata hao waliokuwa Lockdown walishachoka na kutoka nje wenyewe bila kuambiwa na mtu. USA na kwingine waliandamana kwa serikali zao kuwafungia ndani. Kwahiyo, Tz tulichukua the right procedure kubaki nje, na wamejifungia mwisho wametoka wakatukuta tunaendelea kuchapa kazi maana pesa yao kama kweli walitupa ndo ilisaidia kununua vifaa vya hospitali mbalimbali na mavazi ya madaktari wakatuhudumia Vizuri mpaka leo tumesurvive. Tunawashukuru sana kwa msaada wao kweli kweli.
 
pumba tupu.
kwa hiyo tulimuondoa mkoloni mweusi ili ili tutawaliwe kimabavu na mkoloni mweusi?
kama kweli mnajenga miradi mikubwa na kwa hiyo wananchi wanawakubali sasa uoga wa nini hadi mnaogopa mifumo huru ya demokrasia?

Yan hapa tunamsubiri Joe Biden kwa hamu pamoja na icc. madikteta hawana nafasi, hii ni jarne ya 21.
 
Waache tu pesa za misaada zanini ni ujinga pale mtu anakuambia hakusaidii badla upige kazi uendelee unaanza kulilia pesa za msaada waache mapimbi hao
Hata nyerere alishazisema sana hela za misaada huwa hazidumu milele
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…