Kamati ya Mambo ya Nje ya Umoja wa Ulaya (EU) wataka kujua msaada wa Euro Mil. 27 za COVID-19 kwa Tanzania uliahidiwa kwa vigezo gani?

Hatutapona marekani last time ulipofutwa uchaguzi Zanzibar walionda msaada kwenye REA,sijui sahivi watafuta lipi
Serikali ya Sweden imezuia pesa pale REA zilizokuwa zitumike kusambaza umeme vijijini awamu ya tatu. Sababu, serikali imelikoroga na wamiliki wa vituo binafsi vya kuzalishia umeme
 
Usipanic sana. Kunywa Maji mengi alafu lala kupunguza stress
 
Tupo uchumi wa kati hatuitaji misaada yao .. kwanza ukitegemea sana misaada akili inadumaa ,,,, wakwendree huko .. tutakopa na kulipa
 
Sijui kuhusu hayo masharti, sikushiriki kwenye hayo makubaliano kama hata yalikuwepo, Umi Mwalimu yupo kama kuna cha kujibu atafanya hivyo, ...
Walichofanya serekali ya CCM ni kufanya ufisadi wa kimataifa,yaani ufisadi across borders.Serekali ya Magufuli inajinasibu kuwa ni serekali inayopambana na ufisadi lakini imefanya ufisadi huu wa kutisha wa nje ya mipaka ya Tanzania na hii haijawahi kutokea tokea tupate uhuru.Masharti yote haya walikuwa wanayajua lakini kwa kuwa nia yao ilikuwa ovu,nia ya kuiba hela nje ya mipaka ya Tanzania basi wakaamua kuchukua hizo hela na kutupilia masharti yao mbali.Kwa mwendo huu serekali hii ya kifisadi wa kimataifa haiwezi kufika mbali.
 
Hoja yao sio corona. Hoja yao ni inakuwaje watoe hela za msaada wa corona kwa nchi ambayo imesema haina corona na hawatoi takwimu zozote juu ya corona??? Hizo hela zinatumika kwenye nini??
Hoja ya msingi sana hii. Unatoaje msosi kwa mtu ambaye anasema HANA NJAA? 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣
 
Vile vipimo vilivyoonyesha papai lina Covid 19 hukuvisikia?
 
Sio kwel, kila kitu tuna tumia pesa zetu za ndani.. Subirini hata uchaguzi mtasikia pesa ilitoka wapi..
Yaani Meko ni muongo mnooo
 
Vile vipimo vilivyoonyesha papai lina Covid 19 hukuvisikia?
Swali langu ni moja tu,kama vipimo vilikuwa ni fake na vinazuia kutii masharti ya EU pamoja na WHO kwa nini wachukue hela za watu ambazo hawawezi kutii masharti yake?Huo siyo wezi?Huo siyo ufisadi?
 
Maswali ya wana lumumba bana, hadi kichwa kinauma! Haya jibu mwenyewe huenda ikaona faraja ya moyo!
 
Africa haijawahi kwenda sawa kwa kuwasikiliza au kutekeleza matakwa ya Ulaya.
Sio Nigeria au Africa Kusini au Kenya imesonga kwa kuwasikiliza hao wazungu kizazi kipya.
Hawa wazungu kizazi kipya sio tu wamekosa ushawishi au mvuto tu ni wazungu hao hao wanakopa sana kutoka Jamhuri ya watu wa China kuendesha nchi zao.
Sio hiyo tu wazungu hao ambao zamani ndio walikuwa wana kila aina ya viwanda wamejikuta wamepoteza ushindani mkubwa kwa viwanda vya magari,nguo,kusindika vyakula,Toys.Ujenzi wa mitambo mikubwa na meli kwa Japan,China,Korea,Indonesia, India,Brazil,UAE,Vietnam, Thailand.
Kitu ambacho wanaharakati wa nchi zetu hawajui kutoka Ulaya ni kwamba walipora malighafi kutoka Afrika kwa karne nyingi ndio wakapata mtaji.
 
Kuna Maabara ya COVID Mabibo iko full nondo kila kitu, hivyo sidhani kama ni ngumu kwa Serikali kuelezea jinsi ilivyotumia fedha kama ni kweli ilipokea msaada kwaajili ya kudili na COVID, ...
Kuwa na maabara ni suala moja, na kutoa takwimu ni suala jingine. Kwa mujibu wa masharti ya pesa za EU, ukishazipata lazima utoe takwimu kwa WHO ambayo sehemu kubwa iko funded na EU baada ya USA kujitoa kuisaidia. Je tuna publish takwimu hata mkama maambukizi ya corona ni 0?
 
Ila mkuu wakipiga pini hakuna rangi tutaacha kuona sisi wananchi, ni vyema wakiweza wangedili na hali hii bila kuumiza uchumi wa nchi. Tutaumia sisi huku walengwa wanakula maisha
Sisi tunalima , tunakula viazi, ugali, maharage, na wali. Shauri yao wanaotembea na ma V8. Wayajijuuuu
 
Lakini ni ukiukwaji wa kiwango cha kutisha kwa nchi iliyokuwa sii kufikia mbali bali kuanza safari ya demokrasia kama Tanzania ghafla bin vuu hakuna tena kitu kama uchaguzi wa raia kumchagua kiongozi.
Walianza na kupora uchaguzi wa serikali za mitaa baada ya kunogewa na huu uhuni mkubwa bila wakuwawajibisha wakavamia uchaguzi mkuu na kuupora kwa nguvu wakiwatumia Nec, wakuu wa mikoa, wilaya, Rpc's, Ocd's na usalama wa taifa.
Kwa kweli japo sisiem walikuwa sii safi ila Kikwete aliipekeka nchi mahali fulani hivi pa kufikia taifa letu kuwa na mchango duniani kwa kuheshimu haki, usawa na utawala wa kidemokrasia.
Bunge lilifikia mahali ambapo mijala ilikuwa na misuguano japo wapinzani hawakuwa na uwezo wa kimaamuzi kwa sababu ya uchache wao bungeni.
Sisiem walimiliki zaidi ya theluthi mbili japo wapinzani waliongoza kamati za mahesabu ya serikali na taasisi zizizo za kiserikali kukidhi vigezo vya wafadhili kama watch dog.
Sijui kama taifa tumetumbukia je katika huu ukatili wa kupindukia mipaka
Wateule wa rais kufanya ukatili kwa raia wakitumia magari ya namba bandia tena za UN kwenye jinai na wanabaki salama kudhihirisha wana baraka zote kufanya wanayofanya kutoka mamlaka iliyo kuu.
Mungu turehemu na vikwazo naomba kama ikiwezekana vielejezwe kwa watawala na sii raia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…