Kamera za ulinzi kufungwa Kariakoo kwa gharama ya Tsh Milioni 514

Kamera za ulinzi kufungwa Kariakoo kwa gharama ya Tsh Milioni 514

Katika kuhakikisha biashara zinafanyika saa

24, Jiji la Dar es Salaam limeingia mkataba na Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA) unaogharimu jumla ya shilingi milioni 514 wa usimikaji wa mifumo ya kamera za ulinzi katika barabara na maeneo ya Kariakoo ambapo jumla ya kamera 40 zitakazofanya kazi kwa saa 24 zitafungwa katika awamu ya kwanza ya mpango huo kwa ajili ya ufuatiliaji wa hali ya usalama na udhibiti wa matukio ya kihalifu.

Akizungumza baada ya kusaini makubaliano hayo Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Edward Mpogolo amesema lengo la mpango huo ni kuimarisha usalama wa wanachi na wafanyabiashara na kuongeza ufanisi wa shughuli za kibiashara.

Amesema, kamera hizo hizo zitasaidia kurahisisha utambuzi wa matukio, kuimarisha ufuatiliaji wa wahalifu na kutoa ushahidi wa haraka inapohitajika.

My take:

Hawa watu wanaliibia sana hili Taifa na ifike wakati wenye akili kwenye vyombo vya dola waungane na Wananchi Wazalendo wachukuliwe hatua.

Baada ya Wizi mkubwa uliofanywa kwa kuongeza gharama za ujenzi wa viwanja vya michezo, leo umesainiwa mkataba kufunga Kamera 40 tu Kariakoo kwa gharama ya milioni 514.

Acha niendelee kuwaamini CHADEMA kuwa No Reform No Election. Nchi hii inaibiwa sana

View attachment 3240972
Kama HK Vision set ya camera nane ni laki 8 sidhani kama Camera 40 zinafika hata million 50 za kitanzania. Kweli serikali yetu kama kichwa cha mwendawazimu. Kila mtu anajinyolea tu.
 
Kama HK Vision set ya camera nane ni laki 8 sidhani kama Camera 40 zinafika hata million 50 za kitanzania. Kweli serikali yetu kama kichwa cha mwendawazimu. Kila mtu anajinyolea tu.
Wamesema camera zitakuwa ngapi labda vipi kuhusu kijumba Cha kuchunguza matukio na vifaa vyake zikoje vipi kuhusu mafunzo kuendesha mradi
 
Waliompa dili siyo wajinga!
% yake ni 51.4m/-!
Siyo pafupi!
Awamu ya mama ni deals, deals, deals!
Akiondoka watu wamefura hela!
Na kawaida ya pesa ikifura na yale ma -Cardiovascular disease huwa hayachezi mbali na na-Cancerous nayo huwa yanapiga jaramba sio mchezo mchezo. !

Duh 🙄! Pale unapotaka sasa kufaidi maisha hao waheshimiwa wanakuwa tayari wamesha piga hodi mu Nyumba 😳🙄 !
Inaanza kuwa patashika nguo kuchanika !
Tujitahidini bandugu kutenda haki tu kwa sana maana anayejua khatima yako ni Mungu pekee ! Au the Universe au Karma au Call it what you like !

We are just simple creatures na tutabaki Hivyo tupende tusipende 😳
Au nasema uongo ndugu zanguni ???!!
😅😂🤣🤣🙋‍♂️✅🫡
 
Mkuu kwa mchanganuo na ufafanuzi wa aina hii unaondoa mashaka na sintofahamu kwa wananchi. Hongera sana Mkuu, umeeleweka!!
Acha kuwa zwazwa hizo bei kazitoa wapi? Muulize hilo swali akikujibu ni tagg
 
Ili huu mjadala uwe na maana, hebu tufanye uchambuzi mdogo hapa kwa bei na gharama za soko zilizopo kwa sasa. Hii itasaidia kupima kwa uhakika.

Nitafanya uchambuzi wa shughuli hii kwa ununuzi kamera za kiwango cha juu, tukichukua gharamani za vifaa, installation na huduma za ziada baada ya ufungaji.

Hii itatufanya tuweze kuona kama bei ya Tsh milioni 514 ni halali au ni ya juu kuliko inavyostahili.

1. UFUNGA KAMERA ZA CCTV ZA KIWANGO CHA JUU
Kamera 40 zitafungwa katika soko la Kariakoo kwa madhumuni ya kuimarisha usalama.

Kamera hizi zitahakikisha maeneo yote muhimu ya soko yanachunguzwa na kurekodiwa kwa video, hivyo kusaidia kupambana na wizi, ghasia, na uhalifu mwingine.

Kamera zitahakikisha usalama wa wateja na wafanyabiashara katika soko kubwa na lenye shughuli nyingi.

Aina ya Kamera Zitatumika
Kamera ni lazima ziwe za ubora wa picha wa juu, kuhakikisha kuwa picha zinakuwa wazi hata kwenye giza, zina uwezo wa kupiga picha kwa umbali mrefu, na zina teknolojia ya kutambua harakati.

Nitachambua baadhi ya kamera za kiwango cha juu ambazo zinaweza kutumika kwenye mradi huu.

2. AINA ZA KAMERA ZA KIWANGO CHA JUU NA BEI ZAKE

(A) Axis Communications Q-Series

  • Bei: Tsh 10,000,000 - 20,000,000 kwa kila kamera
  • Sifa:
- 4K resolution (Picha za ubora wa juu)
- Infrared night vision
- AI Motion Detection
- Face Recognition Technology
- IP67-rated (Inafaa kutumika kwenye hali mbaya ya hewa)
- Cloud storage kwa usalama wa data
  • Kiasi cha Kamera: 40 kamera
  • Jumla ya Gharama kwa Kamera 40: 40 × Tsh 15,000,000 = Tsh 600,000,000 (Bei ya wastani kwa kila kamera).

(B) Bosch MIC IP Fusion 9000i
  • Bei: Tsh 8,000,000 - 15,000,000 kwa kila kamera
  • Sifa:
- 40x optical zoom
- Thermal imaging (Mwangaza wa joto kwa ulinzi wa hali ya juu)
- Weather-resistant
- Real-time video streaming
  • Kiasi cha Kamera: 40 kamera
  • Jumla ya Gharama kwa Kamera 40: 40 × Tsh 12,000,000 = Tsh 480,000,000.
(C) Hikvision DarkfighterX Series
  • Bei: Tsh 7,000,000 - 12,000,000 kwa kila kamera
  • Sifa:
- Super low-light performance
- True color night vision
- Smart IR technology
- IP67 rating
  • Kiasi cha Kamera: 40 kamera
  • Jumla ya Gharama kwa Kamera 40: 40 × Tsh 10,000,000 = Tsh 400,000,000.
3. GHARAMA ZA USAKINISHAJI, VIFAA VYA ZIADA, NA HUDUMA ZA BAADA YA USAKINISHAJI

(A) Gharama za Usakinishaji na Wiring

Usakinishaji wa kamera za CCTV unahitaji nyaya za umeme, switches, na vifaa vya kuunganishia ili kuhakikisha kila kamera inafanya kazi ipasavyo.

Hii itajumuisha wiring kutoka kwenye NVR (Network Video Recorder) hadi kwa kamera. Hii inaweza kugharimu Tsh 70,000,000 kwa mradi mkubwa kama huu.

(B) Mfumo wa Kuhifadhi Video (NVR / Server)
Kamera 40 za CCTV zitahitaji server au NVR (Network Video Recorder) ili kuhifadhi video inayoendelea kurekodiwa kutoka kwenye kamera. Mfumo huu utakuwa na uwezo wa kuhifadhi video kwa siku kadhaa ili kurahisisha upatikanaji wa video endapo kutahitajika kwa uchunguzi wa uhalifu.
- Gharama ya NVR/Server: Tsh 50,000,000 (kwa uwezo wa kuhifadhi video kwa muda mrefu, na salama).

(C) Gharama za Monita na Vifaa vya Kuonyesha Video
Kwa ufanisi, itahitaji monita (screens) kwa ajili ya kuangalia video za kamera, ambapo vituo vya kudhibiti usalama vitahitaji kuunganishwa na monita za ubora wa juu.
- Gharama za Monita: Tsh 10,000,000.

(D) Huduma za Matengenezo ya Baada ya Usakinishaji
Baada ya kuanzishwa kwa kamera, itahitajika huduma ya matengenezo na usimamizi wa vifaa, ili kuhakikisha kwamba vifaa vinaendelea kufanya kazi ipasavyo na kuwa na matengenezo ya mara kwa mara.
- Gharama za Huduma ya Matengenezo (kwa mwaka): Tsh 20,000,000.

4. UWEZEKANO WA GHARAMA YA TSH MILIONI 514

Gharama za Vifaa (Kamera)

Tuchukulie tunatumia Hikvision DarkfighterX Series kwa bei ya wastani ya Tsh 10,000,000 kwa kamera.
- Jumla ya Kamera 40: 40 × Tsh 10,000,000 = Tsh 400,000,000

Gharama za Usakinishaji na Vifaa Vya Ziada
  • Usakinishaji & Wiring: Tsh 70,000,000
  • NVR/Server: Tsh 50,000,000
  • Monita: Tsh 10,000,000
  • Huduma ya Matengenezo: Tsh 20,000,000
Jumla ya Gharama:
Tsh 400,000,000 (kamera) + Tsh 70,000,000 (usakinishaji) + Tsh 50,000,000 (NVR/Server) + Tsh 10,000,000 (monita) + Tsh 20,000,000 (huduma) = Tsh 550,000,000.

5. MAJUMUISHO
Kwa kutumia kamera za kiwango cha juu kama Hikvision DarkfighterX Series, gharama halisi ya mradi huu ni karibu Tsh 550,000,000, ambayo ni zaidi ya Tsh milioni 514 zinazozungumziwa.

Hivyo, kazi yetu kwenye hili ni kujua ni aina gani ya kamera na vifaa vingine vitakavyotumika kwa shughuli hii ili kuona gharama iliyotajwa itaendana na bei husika.

Ova
Unadhani hatuwajui mnavyocheza na makaratasi?

Nakuuliza swali moja tu!

Nipe tu uthibitisho wa hizo bei ulizoweka hapo!

Nasubiri majibu yako. Usituone tunaosema humu ni mazwazwa!
 
Nadhani tungeona mchanganuo wake kutoka Kwa hao walioingia makubaliano.
 
WIZI MZURI NI USEME TUTAFUNGA KAMERA KARIAKOO YOTE KWA THAMANI YA SHS BILIONI MOJA, USITAJE IDADI YA KAMERA, HUU TUNAUITA UIZI MZURI, LAKINI UNAPOTAJA NA IDADI YA KAMERA HAPO NDIPO UNAKOSEA
ulinzi na usalama wa watu, makazi na biashara zao ni muhimu zaid ya upotoshaji wowote ule unaolinganisha pesa, maisha na uhai wa mwanadamu,

Infact,
camera40 ni chache mno ukilinganisha na baadhi ya makanisa humu nchini yenye yaliyofungwa kamera zaid ya 40 kwa gharama ya zaid ya milioni mia8🐒
 
Mkuu kwani Kariakoo ndio Tanzania nzima, na Kamera 40 zitaona mitaa na vichochoro vyote vya Kariakoo???
ni muhimu pawepo pa kuanzia hususani kariakoo kulingana na potentiality ya kwa uchumi wa mtu moja moja na kwa taifa kwa ujumla 🐒
 
Mkuu ujue kwa fedha ya Bilioni 1, hapa una maanisha Kamera 1 shilingi milioni 25,700,000/=. Duh!!
zipo za hadi 30m gentleman,
yapo makanisa hapo dar yamejengwa kwa 2b, na yamefungwa kamera za usalama za kisasa zenye thamani ya 800m.

usalama wa maisha na uhai wa mwanadamu haulinganishwi na thamani ya kiwango chochote cha fedha gentleman 🐒
 
Mkuu ni kamera 4,000 au 400 au 40??

Mchanganuo wa kina kwa lugha nyepesi unahitajika kufafanua kwa wananchi kuhusu matumizi ya fedha hii ya milioni 514.

Hii fedha Sio mchezo ati??
kwa mfano,
uhai wako thamani yake inaweza kua kamera ngapi kwa haraka haraka gentleman?🐒
 
wanafanisha camera za majumba na hizi zinazofungwa kwenye miji kuna mmoja anasema camera moja china inauzwa laki 8 daah 😁😁😁
 
Fisiem wanavyotafuna pesa za umma utadhani ni mchwa. Ndio maana hawataki kufanyike uchaguzi huru na haki. Uchaguzi ungekuwa ndio mtihani wa taifa basi wangetaka wao ndio wawe watunga mtihani wenyewe, wajifanyie huo huo mtihani wenyewe na wajisahihishie huo huo mtihani wenyewe halafu wajitangazie matokeo ya huo huo mtihani wenyewe. Bata wahed!
 
Back
Top Bottom