Kamera za ulinzi kufungwa Kariakoo kwa gharama ya Tsh Milioni 514

Ukiwatazama tu mkao wao kwenye hicho kikao wanaonekana kabisa hawana uadilifu hata senti
 
Gharama za kufunga na kusimamia ni vitu viwili tofauti!

Huwezi kufunga Camera 40 tu kwa milioni 514. Huo ni wizi na dharau kubwa kwa walipa kodi wa Taifa hili.
kwa jnsi mfumo wa upigaji ulivyo, yawezekana kuwa kila kitu kimekuwa "included".

Kwa maana kwamba mkataba wa kufunga na kusimamia kwa hiyo pesa.

Ukija mkataba mwingine utaja na gharama ingine.

Nimeuliza hivyo ili bwana Tlaatlaah atusaidie kujibu maana majibu yake ni mepesi mno.
 
China Town Ubungo pamefungwa Camera 500 kwa kuanzia 😀😀😀
 
Mambo mengine wanazidisha bana, yaani hatari sana hapo kariakoo wapo vijana hatari sana kwa teknolojia ya kamera, tena wangeweza kufunga wireless camera zenye kujichaji kwa jua
Ndo mtuelewe tunaposema No Reform No Election.

Katiba mbovu na mfumo mbovu wa uchaguzi ndo vinasababisha tunapata viongozi wa hovyo wanaliibia hili Taifa huku wananchi wakiishi kwa shida na tabu zinazozuilika.
 
Tuichambue M514 alafu tujue zinafungwa kamera gani, watuonyeshe quotation ya hizo bidhaa. Yan kakubali
kabisa kamera million Mia tano?.
sidhani kama kupoteza uhai na maisha hata ya mtu moja tukwasababu za kiusalama kudorora, inaweza kulinganishwa na milioni 514 au hata billion gentleman.

I think ilisha tangazwa na viongozi wetu kitaifa kwamba,
there will be no discussions katika suala la usalama wa watu, makazi na biashara zao.

umoja, amani na utulivu wa waTanzania popote walipo utalindwa kwa nguvu na gharama zote bila mbambamba za kibaka au tapeli yoyote wa kisiasa
 
Hizo pesa ni ndogo sana. Kwa Camera arobaini?

Hivi mnataka waweke camera za aina gani hapo Kariakoo? CutePanda? Ring doorbell camera?
=============

Hivi bakresa ametumia kiasi gani cha pesa kufunga cctv camera azam tv? Acheni utani.
 
Ok, umoja amani na utulivu huku wapigaji wakijinafasi.

Ipo siku hakuna marefu yaso na ncha.
 
Unakuta kampuni itakayohusika hapo kuiba pesa kwa kufunga hizo camera ni ya mwanalumumba.

Miezi 6 tu zishajifia na wanarudi kusema hazikufaa kwa "mazingira " yetu wanaandika tena fungu lingine.

Ndio kuupiga mwingi huko kwa awamu ya mama Abdul.
 
Kikubwa zifungwe tu wasingie mitini

Ova
 
Ok, umoja amani na utulivu huku wapigaji wakijinafasi.

Ipo siku hakna maref yaso na ncha.
ramli za kishirikina na imani potofu za mtu moja moja, haziwezi kuzuia ulinzi na usalama wa waTanzania usiimarishwe na kua wa kisasa zaidi
 
Hizo pesa ni ndogo sana. Kwa Camera arobaini?

Hivi mnataka waweke camera za aina gani hapo Kariakoo? CutePanda? Ring doorbell camera?
=============

Hivi bakresa ametumia kiasi gani cha pesa kufunga cctv camera azam tv? Acheni utani.
Kamera moja yauzwaje?
 
Hizo pesa ni ndogo sana. Kwa Camera arobaini?

Hivi mnataka waweke camera za aina gani hapo Kariakoo? CutePanda? Ring doorbell camera?
=============

Hivi bakresa ametumia kiasi gani cha pesa kufunga cctv camera azam tv? Acheni utani.
Mzifunge tu na zote zikamilike tu
😄

Ova
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…