Kamishna Jenerali wa Zimamoto: Changamoto ya maji Kariakoo ilisababisha kuchelewa kuzimwa kwa moto

"Wao kama zimamoto ndio wanajua jana? Ina maana hawajafanya analysisi na kujua maeneo ambayo wanatakiwa wawe na sehemu ya kupata maji?''
 
Tumetoka kwenye changamoto ya upumuaji tumehamia kwenye changamoto ya maji...
 
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji John Masunga amesema sababu ya kuchukua muda mrefu kudhibiti moto katika Soko la Kariakoo ni kutokana na kutokuwa na sehemu za kuchukulia maji ndani ya Kariakoo hivyo iliwalazimu kuyafuata Airport.
Kariakoo yenyewe ilitakiwa iwe imezungukwa na Hydrant Jengo zima, Hilo la kusema watoe taarifa mapema lina msaada gani kama maji yako mbali? Si yale yale tu, wanakuja wamechelewa halafu gari haina maji, nyambaafu kabisa.
 
Kwa hiyo Kariakoo ni City ya bure kabisa. Inapitwa na Mwanza City Center
 
Kwa chumvi siyo ?
Chumvi na vifaa vya bati ni vitu viwili tofauti, bati linaweza kuliwa ndani ya muda mfupi sana, mfano mdogo mzuri : Angalia nyumba zilizojengwa maeneo ya pwani, nyingi zao mabati yameshaliwa tena na upepo wa chumvi tu na sio chumvi kali kama maji.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…