Niliamua kufanya mchezo wa hatari kwa kujitolea kupiga kazi kwa niaba ya wenzangu kwa miaka mitano hivi. Kuna Watz waliniunga mkono vizuri, ndo nikajua uwepo wa matatizo la wadau kutopenda kufanya kazi. Nilifanya nao miradi kadhaa ya binafsi. Na miradi mitatu ya pamoja. Miradi miwili ya pamoja imefanikiwa vizuri ikiwemo parachichi na samaki. Mmoja umekwama sbb ya siasa, tumeusitisha kabisa. Miradi ya watu binafsi mingi imedorora sana, kisa watu hawataki hata kwenda kuona mradi wake ukoje. Anataka kuona kwa njia ya picha tu.
Kwa hiyo, kama unataka kujitolea kufanya kazi kwa niaba ya Watz, pesa ipo, wewe toa mchanganuo vizuri. Lakini utakutana nao kwenye kugawana faida tu.