Kampuni nyingi za Wachina unakuta Ni share ya watu hata 500

Kampuni nyingi za Wachina unakuta Ni share ya watu hata 500

Kuna shida ya watu kutamani pesa za chap chap Hasa sisi vijana tunaomaliza chuo.unakuta MTU kapata kazi Fulani lakini kule hakuna kazi nyingi na hi hutokea sana serikalini MTU anaenda wiki nzima ila Massa anayofanya kazi ni kidogo sana na mshahara anapata.sasa watu walio nje ya mfumo huo wanaona ya Nini kutumia nguvu na akili Wakati Kuna dodo chini ya mpera.
Kuna msemo usemao ukitaka kwenda mbali nenda mwenyewe ila ukitaka kwenda mbali zaidi nenda na mwenzako huu usemi umefanikiwa kwa jamii baadhi kama wahindi,waarabu.Jews. na wachaga kidogo.Tazama biashara za wahindi kama wale wa TATA holding wanapeana mashavu kila bara waendalo.hata hawa wa hapa wanaungana na kuanzisha biashara ndogo mpaka inakuwa kubwa.
Ni mjadala mkubwa sana huu
Ndo nasema sisi sijui tulikosea wapi, yaani kuna sehemu tulikosea kabisa
 
Kwa mara ya kwanza watakuja kama nzige, baada ya miezi utasikia, nina udhuru, mtoto wa binamu ana sendoff siwezi kukosa sbb familia haitanielewa. Wa pili atakwambia leo Man U anakipiga na Real siwezi kosa hiyo mechi. Wa tatu atakwambia jumapili ni komunio sitafika site. bla bla bla mpaka kundi linaishia.
Malila hapo kuna kuwa na Uzuru wa kufa mtu. Utasikia Mtoto kalazwa, kuna msiba, Kuna vikao vya kifamilia.

Yaani ni uzuru juu ya Uzuru
 
Wachina inapo kuja swala la Ushirikiano wako juu sana. Viwanda vyao vingi na hata kampuni zinazo kuja kuwekeza huku na kupewa tenda za kujenga Barabara na Majumba ni muunganiko wa watu wengi walikaa na kuunda.

Unakuta kampuni au kiwanda kimeanzishwa na watu 100 au hata 500 na kila mmoja ana majukumu yake. Katika watu 500 kuna Ma injinia humo, kuna watu wa masoko kuna kila aina ya mtalamu na wote wana piga kazi.

Unakuuta malengo yao ni kuwa na viwanda hata 500 ambapo baada hata ya miaka 30 Wote watakuwa na viwanda.

Hufanya hivyo ili kuunganisha nguvu/mitaji yao na kuwa na nguvu moja.


KIBONGOBONGO

Hilo bongo haliwezekani kila mtu anataka aonekane yeye, watu wanawaza kudhurumiana tu kuibiana na kadhalika.

Unakuta mtu ana kampuni ya ujenzi wa Barabara muda wote wa uhai wake ataishia kujenga barabara za vijijini tu make hana mtaji wa kushika tenda kubwa na pia hataki kuungana na wenzake na wenzake pia hatawaki kuungana.

Ni vigumu sana kushindsna na Wachina wenye nguvu kubwa sana na walio ungana. Ndo maana wameshika tenda Africa nzima za kujenga majumba na Barabara.
Ubinafsi haujawahi na hutatuacha salama...Well said friend..well said.
 
Waafrica Ni shida sana,culture yetu Ni ya kutaka mafanikio ya faster tu. Wivu,uvivu ndo vimejaa mwetu. Lakin nahisi kuna njia ya kuweza kuandaa kizazi kijacho kikaanza kubadilka. Kuliweka kwenye mfumo wa elimu kwenye elimu ya uraia lakin pia Kwa kuweka Sheria Kali ya kudhibiti wa saliti . Na mahakama zetu zisiwe na upendeleo. Hiyo inaweza kusaidia Ila sijui lini litafanyika. Wenzetu hata wazungu wanalindana kazini lakin waafrica kazi kusutana, kuchongeana Kwa boss na kufukuzana tu Basi. Mungu atunusuru tu. But wachache mjaribu it can work
Mkuu unaona hata viongoz wa dini nao ni wasaliti
Wanapanga mambo wakiwa wote badae anazunguka wengne nakusema sikuhusika Ila nashangaa Jina langu kuwepo, period kabsa wanaudh Sana
Kazi kujipendekeza kuchongea wengne tuu unafiki mwanzo mwisho
Halafu ni wazee unafikir sisi vijana tutajifunza nn kama sio kuwaiga tuu japo ni upumbavu
USHAURI
Kuwepo sheria Kali Sana ya kudhibiti usalit wa Aina yoyote ile
 
Wabongo selfish inatumaliza. .lakini shida tulionayo na hatutaki kufikiri mbali au hutuwez kuhimili pressure au challenges zinazokuja mbele yetu.
Utaanzisha biashara lakini kabla ya ku take off tayari watu wanakuja nyuma na shida kibao.
Uki wa ignore chuki zina anza huku wewe bado hujawahi kuiona faida hata kidogo lakini wao wanajua unapata saaana.
Kingine ni uvumilivu hatuna, biashara mpaka isimame jamani sio mchezo.
Wengine tunafeli sababu ya kuibebesha ofisi mzigo usio stahili. Ajiri wafanyakazi kulingana na mahitaji sio sababu mdogo wako anashida ya Ajira unamuweka pale.
Biashara itakufa tu
 
Wachina inapo kuja swala la Ushirikiano wako juu sana. Viwanda vyao vingi na hata kampuni zinazo kuja kuwekeza huku na kupewa tenda za kujenga Barabara na Majumba ni muunganiko wa watu wengi walikaa na kuunda.

Unakuta kampuni au kiwanda kimeanzishwa na watu 100 au hata 500 na kila mmoja ana majukumu yake. Katika watu 500 kuna Ma injinia humo, kuna watu wa masoko kuna kila aina ya mtalamu na wote wana piga kazi.

Unakuuta malengo yao ni kuwa na viwanda hata 500 ambapo baada hata ya miaka 30 Wote watakuwa na viwanda.

Hufanya hivyo ili kuunganisha nguvu/mitaji yao na kuwa na nguvu moja.


KIBONGOBONGO

Hilo bongo haliwezekani kila mtu anataka aonekane yeye, watu wanawaza kudhurumiana tu kuibiana na kadhalika.

Unakuta mtu ana kampuni ya ujenzi wa Barabara muda wote wa uhai wake ataishia kujenga barabara za vijijini tu make hana mtaji wa kushika tenda kubwa na pia hataki kuungana na wenzake na wenzake pia hatawaki kuungana.

Ni vigumu sana kushindsna na Wachina wenye nguvu kubwa sana na walio ungana. Ndo maana wameshika tenda Africa nzima za kujenga majumba na Barabara.
ipo hivyo kaka somali people wakiwa ughaibuni, mfano Uingereza wanachangishana kama watu kumi pound 1000. Tayari wanakuwa na pound 10,000/= wanafungua mgahawa wao wenyewe ndio wanakuwa wafanyakazi pia wao wenyewe wanakuwa suppliers wa mahitaji ya mgahawa,mfano nyama, nyanya,mafuta nk nk kwa kugawana.Baada ya muda mgahawa ukichanganya wanaajiri watu na wao wanaendelea kuwa ma suppliers maisha yanakwenda
 
ipo hivyo kaka somali people wakiwa ughaibuni, mfano Uingereza wanachangishana kama watu kumi pound 1000. Tayari wanakuwa na pound 10,000/= wanafungua mgahawa wao wenyewe ndio wanakuwa wafanyakazi pia wao wenyewe wanakuwa suppliers wa mahitaji ya mgahawa,mfano nyama, nyanya,mafuta nk nk kwa kugawana.Baada ya muda mgahawa ukichanganya wanaajiri watu na wao wanaendelea kuwa ma suppliers maisha yanakwenda
Haya huku inawezekana sema sijui tulikoseaga wapi.

Watu 20 wakichangishana laki 5 kila mmoja ni Miliom 10. Zinatosha wanafungua mgahawa.

Kwenye hao 20 watakuqepo wakupika, kuosha vyombo, cashier, kila kotu na wanakuwa wanapeana zamu.

Dah tuna matatito sana
 
Wabongo selfish inatumaliza. .lakini shida tulionayo na hatutaki kufikiri mbali au hutuwez kuhimili pressure au challenges zinazokuja mbele yetu.
Utaanzisha biashara lakini kabla ya ku take off tayari watu wanakuja nyuma na shida kibao.
Uki wa ignore chuki zina anza huku wewe bado hujawahi kuiona faida hata kidogo lakini wao wanajua unapata saaana.
Kingine ni uvumilivu hatuna, biashara mpaka isimame jamani sio mchezo.
Wengine tunafeli sababu ya kuibebesha ofisi mzigo usio stahili. Ajiri wafanyakazi kulingana na mahitaji sio sababu mdogo wako anashida ya Ajira unamuweka pale.
Biashara itakufa tu
Hao unawaeleza ukweli haina haja ya kiwadanganya..waambie tu. Bora lawama kuliko hasara
 
Mkuu unaona hata viongoz wa dini nao ni wasaliti
Wanapanga mambo wakiwa wote badae anazunguka wengne nakusema sikuhusika Ila nashangaa Jina langu kuwepo, period kabsa wanaudh Sana
Kazi kujipendekeza kuchongea wengne tuu unafiki mwanzo mwisho
Halafu ni wazee unafikir sisi vijana tutajifunza nn kama sio kuwaiga tuu japo ni upumbavu
USHAURI
Kuwepo sheria Kali Sana ya kudhibiti usalit wa Aina yoyote ile
Haina haja ya sheria kama watu wenyewe hawana Uaminifu ni hawana tu
 
Uzi mzuri sana, kama alivyosema kaka Malila hapo juu kipindi namaliza chuo tukapanga na mdau mmoja tuingie poli kwenye kilimo, tumepanga vizuri na bajeti kabisa. Sasa tunamalizia makubaliano na kuhitimisha tuingie field jamaa ananiambia amepata mishe so atatoa pesa tu ila huko shamba siku moja moja ndio ataweza fika ila sio full time, sikupepesa macho nikamchinjia baharini, so hii ni changamoto kubwa sana mtu anataka aone pesa bila kutoa jasho.

Lakini kingine naona tunakatishana sana tamaa, unaweza ukaomba ushauri wa kibiashara kwa mtu majibu utayopewa ni so negative, au unaweza kuanzisha biashara lakini hao hao unadhani ni marafiki au ndugu wanaanza ku curse kwa tutaona jamaa hafiki mbali biashara yenyewe hiyo.

Wabongo wengi hatupendi kuona mtu anapanda ngazi, me nshaamuaga kuwachinjilia mbali watu wote wanaoleta negative energy katika hustle zangu.
 
Aisee kweli Wabongo tuna tatizo tena tatizo kubwa sana na kwa hili sijui ka tutakuja kuendelea asee

Ubinafsi na tamaa ni tatizo kubwa sana.

Lakini chanzo cha yote haya ni Umasikini,,Unakuta mtu keshapigika Zaidi ya miaka 5 labda bila mchongo cku akiote mchongo anaona kashachelewa sana so cha kwanza kufikiria ni kupiga ili aende sawa na wengine
 
Nipo. Umepotea sana mkuu sikusikii
Kaka nipo sana, ndo maana nimekusoma nikaona nichangie kidogo.
Nimejichimbia Njombe naotesha parachichi za kikundi tangu 2016 mpaka 2018 ndo namalizia awamu ya kwanza ya upandaji. Ukiachia mbali majukumu ya kikundi, lakini na mimi mwenyewe nilikuwa naotesha miti ya mbao na parachichi.
 
Niliamua kufanya mchezo wa hatari kwa kujitolea kupiga kazi kwa niaba ya wenzangu kwa miaka mitano hivi. Kuna Watz waliniunga mkono vizuri, ndo nikajua uwepo wa matatizo la wadau kutopenda kufanya kazi. Nilifanya nao miradi kadhaa ya binafsi. Na miradi mitatu ya pamoja. Miradi miwili ya pamoja imefanikiwa vizuri ikiwemo parachichi na samaki. Mmoja umekwama sbb ya siasa, tumeusitisha kabisa. Miradi ya watu binafsi mingi imedorora sana, kisa watu hawataki hata kwenda kuona mradi wake ukoje. Anataka kuona kwa njia ya picha tu.

Kwa hiyo, kama unataka kujitolea kufanya kazi kwa niaba ya Watz, pesa ipo, wewe toa mchanganuo vizuri. Lakini utakutana nao kwenye kugawana faida tu.
 
Wachina inapo kuja swala la Ushirikiano wako juu sana. Viwanda vyao vingi na hata kampuni zinazo kuja kuwekeza huku na kupewa tenda za kujenga Barabara na Majumba ni muunganiko wa watu wengi walikaa na kuunda.

Unakuta kampuni au kiwanda kimeanzishwa na watu 100 au hata 500 na kila mmoja ana majukumu yake. Katika watu 500 kuna Ma injinia humo, kuna watu wa masoko kuna kila aina ya mtalamu na wote wana piga kazi.

Unakuuta malengo yao ni kuwa na viwanda hata 500 ambapo baada hata ya miaka 30 Wote watakuwa na viwanda.

Hufanya hivyo ili kuunganisha nguvu/mitaji yao na kuwa na nguvu moja.


KIBONGOBONGO

Hilo bongo haliwezekani kila mtu anataka aonekane yeye, watu wanawaza kudhurumiana tu kuibiana na kadhalika.

Unakuta mtu ana kampuni ya ujenzi wa Barabara muda wote wa uhai wake ataishia kujenga barabara za vijijini tu make hana mtaji wa kushika tenda kubwa na pia hataki kuungana na wenzake na wenzake pia hatawaki kuungana.

Ni vigumu sana kushindsna na Wachina wenye nguvu kubwa sana na walio ungana. Ndo maana wameshika tenda Africa nzima za kujenga majumba na Barabara.
Walionywa mfano wakandarasi...... Kuna kazi nyingi wameanza kujifunza na kushirikiana, mfano kuna daraja liligharumu bilioni 10 waliungana wakandarasi 10 hivi
 
Walionywa mfano wakandarasi...... Kuna kazi nyingi wameanza kujifunza na kushirikiana, mfano kuna daraja liligharumu bilioni 10 waliungana wakandarasi 10 hivi
Hiyo waliungama kwa kazi moja na baada ya hapo kila mtu anashika zake.

Hii mchi Makandarasi Wazawa wangeungana na kuwa na hata Kampuni 5 tu au 4 zingetosha kabisa na wangeweza kushindana na wachina
 
Niliamua kufanya mchezo wa hatari kwa kujitolea kupiga kazi kwa niaba ya wenzangu kwa miaka mitano hivi. Kuna Watz waliniunga mkono vizuri, ndo nikajua uwepo wa matatizo la wadau kutopenda kufanya kazi. Nilifanya nao miradi kadhaa ya binafsi. Na miradi mitatu ya pamoja. Miradi miwili ya pamoja imefanikiwa vizuri ikiwemo parachichi na samaki. Mmoja umekwama sbb ya siasa, tumeusitisha kabisa. Miradi ya watu binafsi mingi imedorora sana, kisa watu hawataki hata kwenda kuona mradi wake ukoje. Anataka kuona kwa njia ya picha tu.

Kwa hiyo, kama unataka kujitolea kufanya kazi kwa niaba ya Watz, pesa ipo, wewe toa mchanganuo vizuri. Lakini utakutana nao kwenye kugawana faida tu.
Na lawama juu, na baada ya kugawana faida hutawaona tena kila mtu atakuambia anapumzika kwanza au ngoja kwanza ajipange upya. Au mambo yanaingiliana
 
Kwa mara ya kwanza watakuja kama nzige, baada ya miezi utasikia, nina udhuru, mtoto wa binamu ana sendoff siwezi kukosa sbb familia haitanielewa. Wa pili atakwambia leo Man U anakipiga na Real siwezi kosa hiyo mechi. Wa tatu atakwambia jumapili ni komunio sitafika site. bla bla bla mpaka kundi linaishia.

mkubwa yaani hii yako nimekutana nayo live sijui umeijuaje mzee. watz kwa visingizio ni balaa
 
Baba yangu mkubwa ni Engineer alianzisha kampuni ya ujenzi wa nyumba baadae akawaingiza watoto wake wawili mmoja kama mhasibu maana alisoma uhasibu TIA na mwingine ndo msimamizi msimamizi wa kampuni ili baadae waje kuwa warithi wa kampuni hiyo!
Baada ya miaka 3 akagundua mtoto wa kike alikua anachukua hela na kujenga gorofa bila yeye kujua!! Wakati wa kiume alianzisha Kampuni nyingine ya ujenzi kwa siri
unaelewa nn?
Hao watoto ni ma ndoroooooobo
 
Back
Top Bottom