Kampuni ya China Tanzania Security yafafanua madai ya Walinzi wa Vituo vya Mwendokasi kutolipwa mishahara ya miezi mitatu

Kampuni ya China Tanzania Security yafafanua madai ya Walinzi wa Vituo vya Mwendokasi kutolipwa mishahara ya miezi mitatu

Kampuni za Ulinzi zoooote zinazosimamiwa na Wazawa ni kipengele namaanisha zoooote unazozijua wewe zinazosimamiwa na Wazawa ni kipengele kwenye malipo

Kwanza mshahara una range kuanzia 100,000 hadi 150,000 ukizidi sana 200,000 hamna hamna 250,000 tena hio ndio kima cha juu zaidi ila kampuni nyingi ni humo 150,000 kwa mwezi

Nazungumzia kampuni za ulinzi za Wazawa sio za Wageni mfano kampuni ya Wageni km Garda na wengine huwezi kumkuta mlinzi wa kampuni ya Garda eti analalamikia malipo wale ni wazungu kampuni inasimamiwa na Wazungu sio ngozi nyeusi na inaongozwa kizungu zaidi

Sasa njoo kweenye kampuni za Wazawa ni kisanga kwenye malipo uswahili uswahili mwingi yaani mnaishia kumalizana chini kwa chini miezi miwili mtu hujalipwa chochote kunamake na ole wako uende ukatoe malalamiko danadana kibao HR na Mwasibu watakurusha mpaka uelewe jua lako mvua yako mbu wako wao hawajali hilo mpaka ufie lindoni

Kampuni zote za ulinzi za Wazawa kwenye malipo ni kipengele mshahara hawalipi kwa wakati mpaka mshikane mashati ndio wanalipa tena wakiona wewe unabishana nao sana wanakulipa kisha wanakufukuza kazi kisa tu eti umedai chako yaan kudai haki yako ndio ufukuzwe kazi? Wewe kampuni wooote waliopo ofisini wanaliowa na kujilipa ila wanaoenda kulinda hawalipwi miezi inakatika ila waliopo ofisini wanalipwa na kujilipa

Mfano kuna hii kampuni nyingine ipo hapa External Ubungo inaitwa Nathanai Security Company, hii pia ndio km hao China Tanzania unafanya kazi hulipwi yaaan wao wanakufanyisha kazi tu ila mshahara kukulipa hawataki, Serikali iangalie hizi kampuni za Wazawa ni kipengele kwenye kulipa mishahara ya wafanyakazi wao wanaolinda malindo yao

Wewe mwenyewe si unaona majibu ya Bwana Temba hapo anajibu km hajali fulani haya mbwa tunaweza tuwafukuze kazi na tusiwalipe na hawana cha kutufanya waende popote wanapotaka kwenda hizo ndio kauli zao
 
Ulinzi kampuni za watu binafsi bora uuze duka la mangi utaambua kitu mwisho wa mwezi sio kazi ya ulinzi malipo kidogo kulipwa kwenyewe kwa masimango kibao kazi gani sasa hio?
 
Uongozi wa Kampuni ya China Tanzania Security umetoa ufafanuzi kuhusu madai ya Mwanachana wa JamiiForums.com aliyeandika kuwa wafanyakazi wa ofisi hiyo ambao ni Walinzi wanaosimamia Vituo kadhaa vya Usafiri wa Mabasi ya Mwendokasi hawajalipwa mishahara kwa muda wa miezi mitatu na kuwa wakidai hawapati majibu ya kueleweka.

Mwanachama huyo alieleza kuwa mbali na hali hiyo kumekuwa na changamoto nyingine mbalimbali ikiwemo Wafanyakazi kutosikilizwa na kutojaliwa inapotokea wanapata changamoto wakiwa kazini.

Kusoma zaidi alichoandika Mdau huyo, bonyeza hapa ~ Walinzi tunaosimamia Vituo vya Mwendokasi hatujalipwa mshahara kwa miezi mitatu, tukifuatilia tunapigwa danadana

Ufafanuzi wa CHINA TANZANIA SECURITY
Administration Officer wa Kampuni hiyo, Pascal Temba amezungumza na JamiiForums na kufafanua hoja zilizowasilishwa na Mdau kwa kusema:

Kuhusu suala la Mshahara ambayo wanadai ni ya miezi miwili na siyo mitatu, hiyo inatokana na changamoto ambayo tunapitia ambayo inaweza kutokea katika ofisi yoyote ile.

Suala hilo kwanza halijawahi kutokea huko nyuma nadhani hata kwenu hii itakuwa taarifa ya kwanza kuhusu sisi inayozungumzia mishahara.

Suala la Mikataba siyo kweli kuwa hawana mikataba, yote iliyopo ni Mikataba ya maandishi.

Jambo lingine ni kuwa ofisi inashughulika na changamoto nyingine kadhaa za Wafanyakazi kuanzia mtu mmojammoja, na sio kweli kuwa malalamiko yao hayashughulikiwi sio kweli, naomba niweke vizuri kuhusu hilo.

Pamoja na suala hilo la mishahara lakini masuala ya nidhamu bado yanasimamiwa vizuri, unaweza kukuta kuna mfanyakazi anaanza kukiuka taratibu kwa kutofika kazini, mtu anapochukuliwa hatua za kinidhamu anaweza kwenda mbele na kuzungumza vitu vingine ambavyo havipo.
"Kuhusu suala la Mshahara ambayo wanadai ni ya miezi miwili na siyo mitatu," Kwa hiyo wafanyakazi wanakula mawe?
 
"Kuhusu suala la Mshahara ambayo wanadai ni ya miezi miwili na siyo mitatu," Kwa hiyo wafanyakazi wanakula mawe?
Cha ajabu Jeshi la Polisi na Wiraza ya Ulinzi wanaosimamia na kuratibu hizo kampuni ziweze kufanya kazi inavystahiri hukuti wakizungumzia sababu wanaosimamia na wamiliki ni watu wao ambao moja kwa moja wanahusika na Serikali
 
So technically ni kweli bwana Temba hujalipa mishahara staff wako, tena miezi 2! Kama nimeelewa vizuri, mwezi December na January (kwa mujibu wa majibu yako ) hujalipa mishahara? So Christmas na mwaka mpya watu wamepiga pass ndefu na bado unao ujasiri wa kuja na kujitetea? Interesting. Mmeweza kuona utovu wa nidham wa wafanyakazi lakini hamtaki kujishughulisha na chanzo cha UTOVU wa nidhamu? Strange.
Halafu...., kwamba hadi kampuni za ulinzi nazo tunahitaji from China? Daaa
 
Back
Top Bottom