Kampuni ya China Tanzania Security yafafanua madai ya Walinzi wa Vituo vya Mwendokasi kutolipwa mishahara ya miezi mitatu

Kampuni za Ulinzi zoooote zinazosimamiwa na Wazawa ni kipengele namaanisha zoooote unazozijua wewe zinazosimamiwa na Wazawa ni kipengele kwenye malipo

Kwanza mshahara una range kuanzia 100,000 hadi 150,000 ukizidi sana 200,000 hamna hamna 250,000 tena hio ndio kima cha juu zaidi ila kampuni nyingi ni humo 150,000 kwa mwezi

Nazungumzia kampuni za ulinzi za Wazawa sio za Wageni mfano kampuni ya Wageni km Garda na wengine huwezi kumkuta mlinzi wa kampuni ya Garda eti analalamikia malipo wale ni wazungu kampuni inasimamiwa na Wazungu sio ngozi nyeusi na inaongozwa kizungu zaidi

Sasa njoo kweenye kampuni za Wazawa ni kisanga kwenye malipo uswahili uswahili mwingi yaani mnaishia kumalizana chini kwa chini miezi miwili mtu hujalipwa chochote kunamake na ole wako uende ukatoe malalamiko danadana kibao HR na Mwasibu watakurusha mpaka uelewe jua lako mvua yako mbu wako wao hawajali hilo mpaka ufie lindoni

Kampuni zote za ulinzi za Wazawa kwenye malipo ni kipengele mshahara hawalipi kwa wakati mpaka mshikane mashati ndio wanalipa tena wakiona wewe unabishana nao sana wanakulipa kisha wanakufukuza kazi kisa tu eti umedai chako yaan kudai haki yako ndio ufukuzwe kazi? Wewe kampuni wooote waliopo ofisini wanaliowa na kujilipa ila wanaoenda kulinda hawalipwi miezi inakatika ila waliopo ofisini wanalipwa na kujilipa

Mfano kuna hii kampuni nyingine ipo hapa External Ubungo inaitwa Nathanai Security Company, hii pia ndio km hao China Tanzania unafanya kazi hulipwi yaaan wao wanakufanyisha kazi tu ila mshahara kukulipa hawataki, Serikali iangalie hizi kampuni za Wazawa ni kipengele kwenye kulipa mishahara ya wafanyakazi wao wanaolinda malindo yao

Wewe mwenyewe si unaona majibu ya Bwana Temba hapo anajibu km hajali fulani haya mbwa tunaweza tuwafukuze kazi na tusiwalipe na hawana cha kutufanya waende popote wanapotaka kwenda hizo ndio kauli zao
 
Ulinzi kampuni za watu binafsi bora uuze duka la mangi utaambua kitu mwisho wa mwezi sio kazi ya ulinzi malipo kidogo kulipwa kwenyewe kwa masimango kibao kazi gani sasa hio?
 
"Kuhusu suala la Mshahara ambayo wanadai ni ya miezi miwili na siyo mitatu," Kwa hiyo wafanyakazi wanakula mawe?
 
"Kuhusu suala la Mshahara ambayo wanadai ni ya miezi miwili na siyo mitatu," Kwa hiyo wafanyakazi wanakula mawe?
Cha ajabu Jeshi la Polisi na Wiraza ya Ulinzi wanaosimamia na kuratibu hizo kampuni ziweze kufanya kazi inavystahiri hukuti wakizungumzia sababu wanaosimamia na wamiliki ni watu wao ambao moja kwa moja wanahusika na Serikali
 
 
"Nani alituma ile taarifa JamiiForums?!?"
"Tutamtafuta mpaka tumpate na mshahara tutamkata!!!"
"Mnajua mmetuharibia jina la kampuni ninyi!!!"
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…