Kampuni ya tiGO kutumia Nguvu kubwa kulazimisha Watanzania kuweka salio kwenye namba zao za simu

Yes,
hili nalo neno mkuu 👊

waziri wakati fulani kulikua na malalamiko ya bandle, akasema wengi hatuna ujuzi na uelewa wa kutosha dhidi ya matumizi mujarabu ya bandle na ya simu janja. Sasa nadhani wazo lako pia wengi hatuna awareness nalo vya kutosha huku tukilalamikia mtandao kumbe tatizo liko kwetu wenyewe...
 
wanayumba sasa kuna kipindi walikua na campen kabisa ya kuhamasisha watu wanunue salio kwa njia za kielektronic
maana inawapunguzia gharama ya kuchapisha voucher pia ni rafiki kwa mazingira watu wamehamasika sasa wanaanza kulialia nadhan walisahau kwamba mifumo yao inatambua voucher ya kukwangua pekee ili kumtambua active user mimi mwenyewe kuna services flan nmepigwa pin eti kisa siwekagi salio
 
too much of something is harmful ndio hiyo sasa 🐒

sasa hivi wanataka vyote tena dah...
 
Mm niliwapuuza na hiyo message yao .. maana hii line kwanza natumia kwa ajili ya transactions tu tena za maana tuu ila hiyo message waliyoleta nikawapotezea maana there's is no point of blocking a certain number since huduma zote unazipata/unazitumia kutoka kwao yan win-win situation sasa nashangaa wanavolazimisha ku recharge.
 
Kwani Una muda gani hujaweka salio?
 
Mimi walinifungiaga, ikawa na uwezo wa kupigiwa simu tuuu!
Yaani ukiitumia meseji haifiki, pesa haiingii, menu ya tigo pesa haina ufikiaji, sim banking pia.
Nilivyowasiliana nao wakasema haiwezi kurudi hali ya awali, nikaitupa.
 
Nina line ya vodacom tangu 2019 sijawekea salio ila hadi leo ipo hewani. Ila halotel miezi 6 tu utakutana na emergency call.
 
Hii Leo nimepokea ujumbe unaonilazimisha kuweka Salio ndani ya siku tatu, ikiwa Leo ni tarehe 2 mwisho tarehe 5.

Na naambiwa laini yangu itafungiwa kupiga simu kwasabu sijaweka Salio muda mrefu
Nadhhani hii iko kwenye T&C za mitandao yote. Unatakiwa angalau uweke vocha ya TZS. 500 (minimum) ndani ya siku 90. Ili kuifanya laini yako iwe active katika huduma zote.
- Mfano hai:
Nina laini ya Tigo ambayo imefungiwa USSD code zote, hata *102# haikubali, haipokei simu, haitoi simu yeyote, haipokei sms yeyote na haitumi sms yeyote.
  • Wamenianchia ussd code moja tu *150*01# inaayoniwezesha kuingia kwenye account ya biashara na kuendelea na miamala ya Till namba husika.
  • Uzembe uliofanyika ni kutumia simcard kwa muda mrefu, zaidi ya miezi mitatu, bila kuweka salio la kawaida ila niliendelea kuitumia katika miamla inayohusiana na TILL number tu karibu kila siku. Hii simcard kwa sasa ina zaidi ya miaka 2 na bado naitumia hadi muda huu ninapoandika hapa.

Hivyo iwapo umeon hizo jumbe, fanya kununua vocha ya 500 weka ili uendelee kutumia huduma zote.
 
Na kawaida muda mwingi namba inakuwa hewani Sasa wanasema watanifungia, na hakuna lolote zaidi ya ubabe wakijinga kwenye soko,
Uzoefu wangu: Kwa simu card iliyo hewani na haidawi na mtandao husika deni lolote, itaendelea kuwa hewani ila kuna sms fulani utakuja kuzipokea inakuwa kanakwamba ndio umesajiri upya laini yako siku hiyo.
 
Mkuuu punguza kupenda vya bure. Bure ina gharama zake. Lkn Mkuu, hivi buku 1 ndio inakutoa povu kiasi hiki???
 
Mimi Vodacom nawakubali, nimeweka laini yao kwenye simu ndogo na huwa siweki salio, naitumia tu kwa mazoea kwa sababu ndiyo laini yangu ya kwanza kuisajili nilipoanza kumiliki simu ya G-Tide na huwa sitaki kuiacha kabisa iuzwe kwa wengine. Nina zaidi ya mwaka sijaweka salio ila huwa naitumia kwenye M-Pesa mara chache.

Sasa huwa ikipita miezi kadhaa nashtukia wameniwekea MB za ofa, naichomoa laini naiweka kwenye smartphone natumia bando, likiisha nairudisha kwenye simu ndogo, ikipita miezi kadhaa wanaweka MB za ofa, mtindo ni ule ule.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…