Inside10
JF-Expert Member
- May 20, 2011
- 29,909
- 32,414
Hawa jamaa uliwatag ni mabingwa wa kumwaga LIKE kwenye comment zangu
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hawa jamaa uliwatag ni mabingwa wa kumwaga LIKE kwenye comment zangu
Walikuwa sahihi maana sio karoko bali ni parokoNa kuna wapuuzi walikuwa wanatetea kuwa sio karoko [emoji17]
Ahahaa yan kama una notification ya likes 50 lets say, ukiona tu imeanza na ya mmoja wapo hapo, basi jua zoote ni zake!.🤑Hawa jamaa uliwatag ni mabingwa wa kumwaga LIKE kwenye comment zangu
Kweny dini kuna waganga wanaoseme wanatumia vitabu na kuna wavaa suti , wote wachawi wana nguvu za giza nyuma yake kupumbaza watu.Mungu yupo ndani mwako,,,,kwenye hizi dini ndo walozi wengi wamejificha humo,,,,,na wanacheza sana na saikolojia za waumini wao, ukienda kichwakichwa unachezea ndoige za kutosha
Tatizo watu hawasomi wakaelewa na wanaosoma wakaelewa hua wanajitoa mapema baada ya kugundua hapa ninapigwa, Biblia ipo wazi kabisa wala haina konakona Ila washenzi wanatengeneza konakona zao kuwapiga watu kuna wapiga ramli waliovaa suti na Mkononi wameshika Bible na wanapaza sauti kuliita Jina la Yesu Mazabauni kwa sauti Kuu bila uoga na watu wanawaamini akasema "Watu wangu wanahangamia kwa kukosa maarifa" watu wanaokusanyika km makutamo Biblia hawaisomi wengi wao wale unaowaona wamekusanyika pale kwa fulani na kwingine Biblia hawaisomi Ila wanapenda kusomewa tuneno Neno na kuombewa wao wenyewe kuomba hawaombi Ila wanataka kuombewa sasa wale wapiga ramli chonganishi waliovaa suti wanajua jinsi ya kudeal nao lakini wengi hawaisomi Biblia na kuielewa wachache wanaoisoma na kuielewa uanza kwa kuhoji wengine huwazuia wasihoji Ila wanapoendelea kuhoji huambiwa watoke wakaanzishe cha kwao km wanaona kilichopo hakifai maana yake wengi wapo sababu wanahofia kufukuzwa lakini si kwamba wapo sababu wanapenda kuwepoKweny dini kuna waganga wanaoseme wanatumia vitabu na kuna wavaa suti , wote wachawi wana nguvu za giza nyuma yake kupumbaza watu.
1. Kifo cha binti kimetuhuzunisha sana, kama dada wa Lazaro tunamlilia Mungu kama angelikuwepo haya yasingetokea. Katika mapungufu ya binadamu ndipo uwezo wa Mungu unadhihirika.Kanisa Katoliki Jimbo la Bukoba limemsimamisha kutoa huduma za kichungaji Padri, Elipidius Rwegoshora kufuatia tuhuma zinazomkabili za kuhusika katika mauaji ya mtoto mwenye ulemavu wa ngozi, Asimwe Novart.
Askofu wa Jimbo Katoliki Bukoba, Jovitus Mwijage ametangaza uamuzi huo kupitia gazeti la Kiongozi linalotolewa na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), toleo lake la Juni 21 -27, 2024
Gazeti hilo limemnukuu Askofu Mwijage akikiri kuwa mtuhumiwa ni padri wa jimbo lake na amemsimamisha kutoa huduma zote za kichungaji mpaka hapo suala lake litakaposhughulikiwa na vyombo vya sheria.
“Tunahuzunishwa na taarifa ya mauaji ya Asimwe, kwani sisi kama Kanisa Katoliki ni walinzi wa kwanza wa uhai wa wanadamu. Tunaiombea familia yake na kuiombea roho yake ipate pumzio la amani mbinguni.
“Hata hivyo, tumesikia taarifa ya watuhumiwa na mmojawapo akiwa ni Padri Rwegoshora. Ni kweli padri huyo ni wa jimbo Katoliki Bukoba na tumechua uamuazi wa kumsimamisha kutoa huduma zote za kichugaji mpaka hapo suala lake litakaposhughulikiwa na vyombo vya sheria.
“Baada ya vyombo vya sheria kumaliza kazi yake, ndipo taratibu nyingine za kanisa zitafuata,” amesema Askofu Mwijage.
Asimwe menye umri wa miaka miwili na nusu alinyakuliwa mikononi mwa mama yake na watu wasiojulikana Mei 30, 2024 katika Kijiji cha Bulamula, Muleba mkoani Kagera.
Chanzo: Mwananchi
Pia soma
- Mtoto Asimwe Novath aliyekuwa na miaka miwili na miezi sita akutwa amefariki na mwili kufungwa kwenye mfuko
- Kifo cha mtoto albino kinataka amri ya Rais sio masikitiko ya Rais
- Tumeshindwa kumlinda Asimwe
- Kufuta mauaji ya albino, ni kutokomeza kabisa Waganga wapiga ramli
- KWELI - Fr. Elipidius Rwegoshora, ambaye ni Mtuhumiwa wa mauaji ya mtoto mwenye ulemavu wa ngozi Asimwe Novath, ni Padri katika Jimbo la Bukoba
- Kifo cha Asimwe Novath (Albino); Baba mzazi na Paroko msaidizi washikiliwa kwa tuhuma za mauaji
Juu ya sheria zipi mkuu?Hapa mada ya uraia haitakosa! Ila huyu padre itakuwa Askofu alishamchoka la sihivyo Kanisa lingekanusha tu na habari ingekuwa kwisha.(Kanisa katoliki lipo juu ya sheria)
Wanaoijua hii wanaelewa RomaLocutaCausaFistinaEst
Ni muhimu sanaSheria ifuate mkondo wake
Na waziri mkuu alitoa maelezo yanayofanana na ya jeshi la polisi akiwa bungeniKumbe ni kweli? Nilitaka kushangaa, Polisi wamethubutu vipi kukurupuka kumtaja Parko msaidizi bila ushahidi..!
Wale mliokuwa mnasema paroko hawezi kuthuhumiwa nyoosheni mikono juu