1. Fr hapa ametajwa kama mtuhumiwa wa kushiriki mauaji. 2. Hakuna muuaji bado aliyetajwa. 3. Polisi watakusanya ushahidi na kama utakuwa na uzito 4. watuhumiwa watakuwa na kesi ya kujibu. 5. Kutafuta utetezi kwa jinsi gani wao si wahusika. 6. Mahakama itapima ni ushahidi wa upande gani na ni wa nani unamtia hatiani. 7. Itatoa hukumu na adhabu. 8. Atakaye ona hajaridhika atakata rufaa. 9. Hivyo, kutoa hukumu kwa sasa na kuwaona watuhumiwa kama wenye hatia ni kuonyesha tu hatujui Katiba, sheria ya kanuni ya adhabu na ya mwendo wa makosa ya jinai zinasemaje. 10. Na mbaya zaidi katika mambo haya tunakimbilia kunyoosheana vidole kutokana na chuki za kiimani tunazo'entertain'. Bure kabisa!