Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 28,297
- 68,017
- Thread starter
-
- #81
Huwezi kuponga dhambi kama kanisa kama unashindwa kuikosoa serikali pale anapokosea huo ni Unafiki na uoga.Kanisa haliipongezi serikali, sijawahi kusikia wakikaa vikao vya kuipongeza serikali. Ila lina wajibu wa kuiombea serikali na kukemea dhambk na nadhani wanafanya hivyo...
Unajua maana ya neno kanisa??
Kanisa maana yake ni walioitwa watoke.
Yesu alikuwa nakanisa lake dogo la watu 12
Mwanzo.
Ama ulitaka liwe ni jengo ili ulitambue kuwa ni kanisa
Kanisa litaikosoa serikali pale inapoenda kinyume na neno.Huwezi kuponga dhambi kama kanisa kama unashindwa kuikosoa serikali pale anapokosea huo ni Unafiki na uoga.
Unaona sasa ulivyokariri.Kanisa lazima liwe jengo hiyo ndio maana yake ya msingi, hizo maana zingine za ziada ni nyongeza tuu
Kazi ya kanisa sio kuikosoa serikali, nenda kasome miongozo ya kanisa lako. Hatutaki kanisa liende kinyume na misingi yake.Huwezi kuponga dhambi kama kanisa kama unashindwa kuikosoa serikali pale anapokosea huo ni Unafiki na uoga.
Viongozi wakuu wa sabato ni ccm .sasa wataikosoaje ccm? Ukiangali trend utaona jinsi wanavoisifia ccm na kuwaalika viongozi wa ccm kwa ajili ya matamko au kuwasafishia mambo yao..
KANISA LA WASABATO MNAPASWA MKOSOE MAOVU YA SERIKALI ZAIDI KULIKO KUKOSOA WENZENU WA ROMAN CATHOLIC.
Anàandika, Robert Heriel
Mtibeli.
Mimi nimezaliwa kwenye Usabato, nimekua na kulelewa kwenye Usabato. Kimsingi Mimi ni Msabato ingawaje ni Mtibeli kiasili. Yaani tuseme ni Mtibeli aliyezaliwa katika Dhehebu la kisabato. Sasa sisi Watibeli ni Watu wa kusema ukweli hata kama unatugusa wenyewe. Hatunaga ushabiki.
Licha ya Wasabato wengi kubobea katika Mafundisho ya biblia na dini yao lakini wanaupungufu mkubwa wa kuisema Kweli hasa linapokuja suala la siasa, utawala na serikali.
Ni ngumu sana kusikia Kanisa la Sabato likikemea maovu ya Serikali. Kwa upande wangu sijawahi kusikia. Ila wakati huohuo ni rahisi kusikia kanisa la Wasabato wakiipongeza serikali na kuiombea. Hapa ndipo Watibeli tunapoona kuna tatizo fulani la Unafiki.
Wasabato wamefundishwa kutojihusisha na siasa. Kanisa pia moja ya sera zake ni kutojihusisha na siasa.
lakini Wasabato ni mabingwa duniani wa kukosoa dini zingine hasahasa Ukatoliki ambao ndio Mama wa Ukristo. Hata biblia inayotumika ni Wakatoliki walioiratibu na kuipanga. Ukisema bila ukatoliki hakuna biblia utakuwa upo sahihi kwa sababu Biblia ilikusanywa na wakatoliki. Nisitoke nje ya mada, na wala Wakatoliki wasidhani nawatetea hapa.
Hakuna kanisa lolote au dini yoyote itakayokuwa ya haki na sahihi zaidi ya ile inayotetea haki na kuikosoa serikali. Hakuna dini wala dhehebu hilo.
Manabii wote, mitume wote, Makuhani wote, Waamuzi wote walijihusisha na siasa hasa pale mambo yanapoenda Mrama au viongozi wa kisiasa wanapogeuka wadhalimu au kutenda maovu.
Yesu mwenyewe ambaye ndio msingi wa ukristo aliikosoa serikali na vyombo vya Dola.
Sasa iweje Wasabato wanajitoa katika wajibu huo.
Utatakaje Haki bila kujiingiza kwenye siasa ? How?
Yaani uwaambie waumini wako waache dhambi wakati msingi wa dhambi unabebwa na siasa.
Waumini watashikaje amri za Mungu bila kukemea viongozi wao wa kisiasa? how?
Amri kama ya kufanya kazi ambayo ni moja ya amri za Mungu, Muumini anafanya kazi kwenye serikali yenye mazingira ya mengi ya rushwa, wizi, ufisadi, dhulma alafu muda huohuo Kanisa halikemei serikali ikiwa na baadhi ya viongozi madhalimu, hivi kweli inakuja Akilini?
Unasema lengo la kanisa ni uinjilishaji,haya utafanyaje uinjilishaji kwa Watu na jamii inayodhulumiwa?
Badala ya kusaidiana na jamii kukabiliana na baadhi ya viongozi madhalimu ninyi mnawatia moyo wakijinga kuwa ati tumaini lipo wakifika Mbinguni kwani duniani kuna dhiki.
Wasabato tumekuwa kama Wamishenari walioungana na makoloni kututawala na kulainisha mioyo yetu kwa aya za kuokoteza.
Tumekuwa Machawa wa Watawala.
Haya mnahubiri neno la kweli, lakini kweli gani yenye mipaka? Kweli inayohusu Watu duni, dhalili, Waumini wasio na Mamlaka ndio kweli?
Kweli inayowaogopa Watawala na serikali? Hiyo ni kweli gani hiyo?
Tumekalia Sabato
Alama ya mnyama!
Sijui Papa!
Kama mnashindwa kuikosoa serikali mnayoiona mtawezana na Mambo ya Mnyama au huyo Papa kweli?
Tuacheni kuwa Machawa wa serikali!
Mbona Wakatoliki na Walutheri mabaraza yao kila mara hutoa matamko ya kukosa serikali pale wanapoona unakosea?
Dini ya kweli ni ile inayopigania Haki. Na huwezi pigania haki bila kuigusa siasa na serikali kwa sababu hao ndio wanahusika na mambo ya kutoa Haki.
Tusiwapotoshe waumini kuwa ati ufalme wa duniani hatuhusiani nao ilhali ibiblia iko wazi kuwa sisi ni Watu wa duniani na asilimia mia moja tunautawala huku duniani. Huko mbinguni sio kwetu na hata biblia yenyewe inakiri hilo. Ndio maana hata tukienda huko kama biblia isemavyo hatutakaa milele isipokuwa miaka elfu tuu.
Acha nipumzike sasa!
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Miongozo hiyo imewekwa na wanadamu ambao ndio hao nasema wamegeuka Machawa.Kazi ya kanisa sio kuikosoa serikali, nenda kasome miongozo ya kanisa lako. Hatutaki kanisa liende kinyume na misingi yake.
Nakuunga mkono kwenye issue ya kuponda imani zingine, kujiona kwamba wao(wasabato)ni special kuliko, ndio waliochaguliwa etc ila swala la kuikosoa serikali haijawahi kuwa kazi ya serikali.
Wasabato hawataki waumini wajihusishe na siasa na uongozi wa nchi,hii imani ya ajabu kweli,wao wakiamka na wakilala ni alama ya mnyama na ukatoliki,hovyo kabisa.
Bila kusahau Catholic ndio kanisa mama la ukristo duniani.
Viongozi wa dini wapo kwa ajili kulea watu kiroho na sio kutwa kurumbana na wana siasa.
Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
Unaweza kutengenisha roho na mwili?
Kwani kazi ya vyama vya siasa nini? Kanisa kazi kuu yake ni kuhubiri injili.
Sio kazi ya kiongozi wa dini kumpangia mwana siasa namna ya kuendesha siasa zake na ndio maana hiyo ikaitwa siasa na nyingine ikaitwa dini kwa maana ni vitu viwili tofauti.Unaweza kutengenisha roho na mwili?
Wewe unatafuta like na kusifiwa kupitia mgongo wa Kanisa la Waadventista wa Sabato
Hayo malalamiko yako siyo sehemu ya kazi ya Kanisa unasema Yesu alikemea leta mfano wa aya Yesu alikemea hapa tuone wapi alikemea
Yesu alikuja ulimwenguni wakati Taifa lake la Kiyahudi likiwa chini ya ukoloni wa Warumi na walikuwa wakiwatesa hasa lkn kauli yake ilikuwa Ya Mungu mpeni Mungu na Kaisari mpeni kaisari wewe unasema alikemea leta aya yako
Warumi kupitia mtume Paulo anasema mamlaka zote zinatoka kwa Mungu yeye ndiye huziweka na kuziondoa unafikiri Kanisa halijui hili
Waadventista wanapitia changamoto ya kunyimwa haki yao ya kuabudu siku ya jmosi tumeshuhudia mara kadhaa hata utumishi kupanga usaili siku ya jmosi nani umewahi kusikia akiwatetea zaidi ya kufanyiwa kejeli lkn limekuwa likijitahidi kuwasilisha hoja zao bila kelele kama hao wengine
Ukitaka kupata sifa tafuta njia nyingine siyo kulisema hovyo Kanisa la Waadventista wa Sabato
Inamana mpaka leo haujajua kipimo cha kanisa halisi na la kweli la Mungu.
Mungu aliweka vipimo na mizani.
Ili wanawake waliweke kila kanisa na kulipima.
Kama halitoshelezi basi Mungu hayuml ndani yake.
Wengi wanadhani wapo na Mungu kumbe ni zamani walishamuacha.
Mariamu na yusufu walizani hvyo pia kumbe walimuacha hekaluni.
Kanisa ni mwiko kujihusisha na siasa.
Kudai haki , ama kampeni zozote zile.
Kazi ambayo kanisa limeachiwa ni kuhubiri injili kwa kila kiumbe, kazo ambayo makanisa hawaitaki kabisa kwa sasa
Wapo bize na mashule,mahospitali, vyuo na mambo mengine ya kidunia.
Hayo ni mazuri ila sio kazi ya kanisa halisi.
Biblia inasema katoliki ni kahaba mkuu na mama wa makahaba, amezaa binti makahaba wanafanana nae
Na kila kanisa litalotoka kwa roman mwisho wa siku hurudi tena kwenye mifumo ile ile waliyotoka
Kkkt, anglican, pentecost na mengine yote.
Katoliki ni adui kuu wa dunia hii, ushoga upo nyuma ya vatican,marekan ni mdomo wake tu.
Uchafu wote wa makanisa asili ni roman.
Kwani kazi ya vyama vya siasa nini? Kanisa kazi kuu yake ni kuhubiri injili.
mafarisayo walimuambia ondoka hapa Herode anataka kukuuaSoma
Luka 13:31-32
Yaani ulichokiandika ni sawa na kusema Chadema hawakemei dhambi au kuhubiri injili kama wenzao wa NCCR na UDP ambao nimekuwa nawasikia wakifanya hivyo na kazi yao Chadema ni kuponda CCM