Kanisa la Wasabato Mnapaswa Mkosoe maovu ya serikali zaidi kuliko kukosoa wenzenu wa Roman Catholic

Kanisa la Wasabato Mnapaswa Mkosoe maovu ya serikali zaidi kuliko kukosoa wenzenu wa Roman Catholic

Kanisa haliipongezi serikali, sijawahi kusikia wakikaa vikao vya kuipongeza serikali. Ila lina wajibu wa kuiombea serikali na kukemea dhambk na nadhani wanafanya hivyo...
Huwezi kuponga dhambi kama kanisa kama unashindwa kuikosoa serikali pale anapokosea huo ni Unafiki na uoga.
 
Unajua maana ya neno kanisa??
Kanisa maana yake ni walioitwa watoke.
Yesu alikuwa nakanisa lake dogo la watu 12
Mwanzo.
Ama ulitaka liwe ni jengo ili ulitambue kuwa ni kanisa

Kanisa lazima liwe jengo hiyo ndio maana yake ya msingi, hizo maana zingine za ziada ni nyongeza tuu
 
Huwezi kuponga dhambi kama kanisa kama unashindwa kuikosoa serikali pale anapokosea huo ni Unafiki na uoga.
Kanisa litaikosoa serikali pale inapoenda kinyume na neno.
Na sio kinyume na katiba
Katiba imeundwa na wanadamu inakosewa.
Ila neno ni la Mungu halikosewi
Kanisa haliwezi kushikilia msingi wa mwanadamu.
Kwakuwa sio yakini.
Ila msingi wa neno la Mungu
Sasa kanisa linakosoa mikataba,mara sijui linadai maji,mara shule, mara bandari.
Upuuzi kw kanisa
 
Kanisa lazima liwe jengo hiyo ndio maana yake ya msingi, hizo maana zingine za ziada ni nyongeza tuu
Unaona sasa ulivyokariri.
Kwamba kanisa ni jengo?
Kama kanisa ni jengo basi hata waislamu na wapagani wanayo tena mazuri tuu
Kanisa ni nini ?
 
Huwezi kuponga dhambi kama kanisa kama unashindwa kuikosoa serikali pale anapokosea huo ni Unafiki na uoga.
Kazi ya kanisa sio kuikosoa serikali, nenda kasome miongozo ya kanisa lako. Hatutaki kanisa liende kinyume na misingi yake.

Nakuunga mkono kwenye issue ya kuponda imani zingine, kujiona kwamba wao(wasabato)ni special kuliko, ndio waliochaguliwa etc ila swala la kuikosoa serikali haijawahi kuwa kazi ya serikali.
 
Viongozi wakuu wa sabato ni ccm .sasa wataikosoaje ccm? Ukiangali trend utaona jinsi wanavoisifia ccm na kuwaalika viongozi wa ccm kwa ajili ya matamko au kuwasafishia mambo yao..

Mbona hata hizo dini zingine kuna ccm lakini wakiona serikali imekosea wanakosoa?
 
KANISA LA WASABATO MNAPASWA MKOSOE MAOVU YA SERIKALI ZAIDI KULIKO KUKOSOA WENZENU WA ROMAN CATHOLIC.

Anàandika, Robert Heriel
Mtibeli.

Mimi nimezaliwa kwenye Usabato, nimekua na kulelewa kwenye Usabato. Kimsingi Mimi ni Msabato ingawaje ni Mtibeli kiasili. Yaani tuseme ni Mtibeli aliyezaliwa katika Dhehebu la kisabato. Sasa sisi Watibeli ni Watu wa kusema ukweli hata kama unatugusa wenyewe. Hatunaga ushabiki.

Licha ya Wasabato wengi kubobea katika Mafundisho ya biblia na dini yao lakini wanaupungufu mkubwa wa kuisema Kweli hasa linapokuja suala la siasa, utawala na serikali.

Ni ngumu sana kusikia Kanisa la Sabato likikemea maovu ya Serikali. Kwa upande wangu sijawahi kusikia. Ila wakati huohuo ni rahisi kusikia kanisa la Wasabato wakiipongeza serikali na kuiombea. Hapa ndipo Watibeli tunapoona kuna tatizo fulani la Unafiki.

Wasabato wamefundishwa kutojihusisha na siasa. Kanisa pia moja ya sera zake ni kutojihusisha na siasa.

lakini Wasabato ni mabingwa duniani wa kukosoa dini zingine hasahasa Ukatoliki ambao ndio Mama wa Ukristo. Hata biblia inayotumika ni Wakatoliki walioiratibu na kuipanga. Ukisema bila ukatoliki hakuna biblia utakuwa upo sahihi kwa sababu Biblia ilikusanywa na wakatoliki. Nisitoke nje ya mada, na wala Wakatoliki wasidhani nawatetea hapa.

Hakuna kanisa lolote au dini yoyote itakayokuwa ya haki na sahihi zaidi ya ile inayotetea haki na kuikosoa serikali. Hakuna dini wala dhehebu hilo.

Manabii wote, mitume wote, Makuhani wote, Waamuzi wote walijihusisha na siasa hasa pale mambo yanapoenda Mrama au viongozi wa kisiasa wanapogeuka wadhalimu au kutenda maovu.

Yesu mwenyewe ambaye ndio msingi wa ukristo aliikosoa serikali na vyombo vya Dola.

Sasa iweje Wasabato wanajitoa katika wajibu huo.

Utatakaje Haki bila kujiingiza kwenye siasa ? How?

Yaani uwaambie waumini wako waache dhambi wakati msingi wa dhambi unabebwa na siasa.

Waumini watashikaje amri za Mungu bila kukemea viongozi wao wa kisiasa? how?

Amri kama ya kufanya kazi ambayo ni moja ya amri za Mungu, Muumini anafanya kazi kwenye serikali yenye mazingira ya mengi ya rushwa, wizi, ufisadi, dhulma alafu muda huohuo Kanisa halikemei serikali ikiwa na baadhi ya viongozi madhalimu, hivi kweli inakuja Akilini?

Unasema lengo la kanisa ni uinjilishaji,haya utafanyaje uinjilishaji kwa Watu na jamii inayodhulumiwa?
Badala ya kusaidiana na jamii kukabiliana na baadhi ya viongozi madhalimu ninyi mnawatia moyo wakijinga kuwa ati tumaini lipo wakifika Mbinguni kwani duniani kuna dhiki.

Wasabato tumekuwa kama Wamishenari walioungana na makoloni kututawala na kulainisha mioyo yetu kwa aya za kuokoteza.

Tumekuwa Machawa wa Watawala.

Haya mnahubiri neno la kweli, lakini kweli gani yenye mipaka? Kweli inayohusu Watu duni, dhalili, Waumini wasio na Mamlaka ndio kweli?

Kweli inayowaogopa Watawala na serikali? Hiyo ni kweli gani hiyo?

Tumekalia Sabato
Alama ya mnyama!
Sijui Papa!

Kama mnashindwa kuikosoa serikali mnayoiona mtawezana na Mambo ya Mnyama au huyo Papa kweli?

Tuacheni kuwa Machawa wa serikali!

Mbona Wakatoliki na Walutheri mabaraza yao kila mara hutoa matamko ya kukosa serikali pale wanapoona unakosea?

Dini ya kweli ni ile inayopigania Haki. Na huwezi pigania haki bila kuigusa siasa na serikali kwa sababu hao ndio wanahusika na mambo ya kutoa Haki.

Tusiwapotoshe waumini kuwa ati ufalme wa duniani hatuhusiani nao ilhali ibiblia iko wazi kuwa sisi ni Watu wa duniani na asilimia mia moja tunautawala huku duniani. Huko mbinguni sio kwetu na hata biblia yenyewe inakiri hilo. Ndio maana hata tukienda huko kama biblia isemavyo hatutakaa milele isipokuwa miaka elfu tuu.

Acha nipumzike sasa!

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam

Wasabato hawataki waumini wajihusishe na siasa na uongozi wa nchi,hii imani ya ajabu kweli,wao wakiamka na wakilala ni alama ya mnyama na ukatoliki,hovyo kabisa.

Bila kusahau Catholic ndio kanisa mama la ukristo duniani.
 
Kazi ya kanisa sio kuikosoa serikali, nenda kasome miongozo ya kanisa lako. Hatutaki kanisa liende kinyume na misingi yake.

Nakuunga mkono kwenye issue ya kuponda imani zingine, kujiona kwamba wao(wasabato)ni special kuliko, ndio waliochaguliwa etc ila swala la kuikosoa serikali haijawahi kuwa kazi ya serikali.
Miongozo hiyo imewekwa na wanadamu ambao ndio hao nasema wamegeuka Machawa.

Kusema kanisa lisiikosoe serikali au viongozi wa serikali wakikosea wakati manabii na viongozi wa kiimani karibia wote waliokosa serikali mpaka wengine kuwekwa jela ni kwenda kinyume na Biblia.

Muongozo mkuu wa Wasabato ni Biblia. Na biblia inataka Watu wakemee maovu ikiwemo ya Wanasiasa.

Yohana mbatizaji unamjua?
Isaya
Nehemiah
Musa
Yona
Yeremia
Wote hao waliikosoa serikali
 
Wasabato hawataki waumini wajihusishe na siasa na uongozi wa nchi,hii imani ya ajabu kweli,wao wakiamka na wakilala ni alama ya mnyama na ukatoliki,hovyo kabisa.

Bila kusahau Catholic ndio kanisa mama la ukristo duniani.

Hapa ndio kuna kukwama
 
Ndugu, vijikanisa vidogo vidogo visivyo na mifumo hasa hivi vya kipentekoste ni tatizo, bila kuisifia CCM wanaweza kujikuta wanakosa leseni za biashara zao, nukuu yaliyomkuta Mbarikiwa na kanisa lake kwa kusimamia haki. Kumbuka yaliyomkuta Kakobe baada ya kuihoji CCM, kumbuka yaliyotaka kumkuta mtumishi Mwingira aliposema Lissu hakamatiki ni sauti kutoka mbinguni tuifuate..

Kongole kwa kanisa katoliki kukupita maskofu wenu TEC, nyie ni vinara wa haki - wengine si kwamba hawataki wanataka ila wanaogopa tonge litadondoka.
 
Wewe unatafuta like na kusifiwa kupitia mgongo wa Kanisa la Waadventista wa Sabato

Hayo malalamiko yako siyo sehemu ya kazi ya Kanisa unasema Yesu alikemea leta mfano wa aya Yesu alikemea hapa tuone wapi alikemea

Yesu alikuja ulimwenguni wakati Taifa lake la Kiyahudi likiwa chini ya ukoloni wa Warumi na walikuwa wakiwatesa hasa lkn kauli yake ilikuwa Ya Mungu mpeni Mungu na Kaisari mpeni kaisari wewe unasema alikemea leta aya yako

Warumi kupitia mtume Paulo anasema mamlaka zote zinatoka kwa Mungu yeye ndiye huziweka na kuziondoa unafikiri Kanisa halijui hili

Waadventista wanapitia changamoto ya kunyimwa haki yao ya kuabudu siku ya jmosi tumeshuhudia mara kadhaa hata utumishi kupanga usaili siku ya jmosi nani umewahi kusikia akiwatetea zaidi ya kufanyiwa kejeli lkn limekuwa likijitahidi kuwasilisha hoja zao bila kelele kama hao wengine

Ukitaka kupata sifa tafuta njia nyingine siyo kulisema hovyo Kanisa la Waadventista wa Sabato

Utapiganiaje Haki bila kujihusisha na siasa, hapo ndio uje na Facts?
Sasa like na sifa zitanisaidia nini Mimi?

Alafu kama wewe ni Msabato basi umenianbusha sana. Nilitegemea uje kwa hoja ili hata wasiowasabato wakisoma washawishike na hoja zako.
Sasa kama yesu hakuingia kwenye siasa Unafikiri kilichomfanya asulubiwe ni nini? Embu tumia akili hata kidogo.
 
Inamana mpaka leo haujajua kipimo cha kanisa halisi na la kweli la Mungu.

Mungu aliweka vipimo na mizani.

Ili wanawake waliweke kila kanisa na kulipima.

Kama halitoshelezi basi Mungu hayuml ndani yake.

Wengi wanadhani wapo na Mungu kumbe ni zamani walishamuacha.

Mariamu na yusufu walizani hvyo pia kumbe walimuacha hekaluni.

Kanisa ni mwiko kujihusisha na siasa.

Kudai haki , ama kampeni zozote zile.

Kazi ambayo kanisa limeachiwa ni kuhubiri injili kwa kila kiumbe, kazo ambayo makanisa hawaitaki kabisa kwa sasa

Wapo bize na mashule,mahospitali, vyuo na mambo mengine ya kidunia.

Hayo ni mazuri ila sio kazi ya kanisa halisi.

Biblia inasema katoliki ni kahaba mkuu na mama wa makahaba, amezaa binti makahaba wanafanana nae

Na kila kanisa litalotoka kwa roman mwisho wa siku hurudi tena kwenye mifumo ile ile waliyotoka
Kkkt, anglican, pentecost na mengine yote.

Katoliki ni adui kuu wa dunia hii, ushoga upo nyuma ya vatican,marekan ni mdomo wake tu.

Uchafu wote wa makanisa asili ni roman.

Kifungu gani kimeitaja katoliki kama kahaba mkuu.
 
Soma
Luka 13:31-32
mafarisayo walimuambia ondoka hapa Herode anataka kukuua

Sasa hapo Yesu alijihusishaje na siasa?

Hofu ya Herode ilikuwa ni Yesu kuitwa mfalme wakati huo huo Herode naye alikuwa ni mfalme

Hata kama ni wewe mtu ukiona anataka kuchukua cheo chako utafanyaje
 
Yaani ulichokiandika ni sawa na kusema Chadema hawakemei dhambi au kuhubiri injili kama wenzao wa NCCR na UDP ambao nimekuwa nawasikia wakifanya hivyo na kazi yao Chadema ni kuponda CCM

Wasabato waamini dhehebu lao ni la kweli.na kwenye kweli kuna Haki.
Swali linakuja, kwa nini hawakemei uovu ambao unafanywa na serikali?
Huo ndio msingi wa swali.

Ukasema kunachangamoto ya kusali jumamosi, sawà!
Sasa tuambie utapataje haki ya kusali jumamosi na utaomba haki hiyo kwa namna ipi ikiwa unaamini utawala wa dunia ni washetani? Kwamba unamuona Shetani haki ya kumuabudu Mungu wako?
 
Back
Top Bottom