Kansa ya matiti inammaliza mke wangu nikiwa nashuhudia, sina la kufanya. Sijui kama naweza kusahau hili

Whether protein is bad or signal is bad.
Sisi wanadamu hatuwezi kuwa waathirika wa vina Saba vyetu wenyewe..

Genes Kama blueprint ya kuzalisha protein ( Cells ) Ni kiwanda kinachozalisha protini kulingana na taarifa au signo zinazozifikia au kupokea.

Badili signo kubadilisha uzalishaji wa proteins hizo.... Environment.
# Epigenetics.
#Mawazo + Hisia jirani wa kansa.
 
Njoo tupeane moyo.

Nimeanza kumuuguza dada yangu cancer kuanzia mwaka 2019,

Tuliambiwa afanye Chemo baadae afanyiwe upasuaji....

Akaanza mizunguko minne akamaliza, ikaongezwa minne akamaliza. Akarudishwa Muhimbili Kwa ajili ya upasuaji, madaktari wakatuambia arudi ocean road uvimbe haujapungua.

Ikaongezwa mizunguko 8 Tena , akapewa transfer Muhimbili awamu hii mgonjwa akagoma kufanyiwa Op. Akakaa nyumbani mwaka bila matibabu ya hospital.

Ziwa likatoboka likawa linamwaga maji pamoja na usaha, tukarudi hospital,wakasema aanze chemo upya ikaenda mizunguko 6 na mionzi 16. Kamaliza mwez wa 10 mwaka huu Kwa Sasa kapewa mapumziko ya miezi mitatu na dawa anatumia.

Eneo la ziwa limefutika na wekundu kama kamwagiwa maji ya moto.

Cancer ni stage 4.


Ushauri wangu
Kama unaweza mpeleka ocean road mpelekee pale.
Pili kidonda kisafishwe Kila siku na maji ya drip wekeni na fragine ya vidonge mnatwanga mnapakaa eneo la kidonda kabla ya kukifunga

Kidonda usikifunge na khanga Wala kitenge funga na bandage.

Ajitahidi kunywa juisi ya stafeli angalau Kila siku glass Moja.
Majani yake pia chemsha anywee.

Mungu atutie nguvu katika Janga hili 🙏🙏🙏🙏🙏
 
Kuna mtu mmoja nilikutana nae machakos kenya nikiwa na shida fulani,ni daktari mwenye bustani ya dawa na alinisaidia nikapona kabisa,katika moja ya maongezi yake alizungumzia cancer ila sina hakika na jambo alilonalo mkeo kama liko mahala anapoweza kufanyia kazi,
Nitajitahid nikutafutie mawasiliano yake uone kama kuna analoweza kukushauri ama kukusaidia
 
Pole ndugu yangu na pole kwa familia yako mkuu.
Mtie moyo kwa madhira anayopitia.
 
Apumzike kwa amani brother, alikumbwa na kansa ya eneo gani?
 
Pole sana mkuu MWENYEZI MUNGU asaidie, mama yangu alifariki na kansa ya titi mwaka 2013, alikuwa kashafanyiwa operesheni ndo maisha mkuu tutafanyaje!?
 
Pole Man!

Nimeumizwa sana na Hilo!

Hebu ajaribu urine therapy,ule wa asubuhi na mapema anywe tu was kwake mwenyewe!

Nimeongozwa na mithali 5:15 ,sio tiba ngeni hata mababu,wachina na wahindi hasta king Solomon alitumia!!

Hivyo TU!!

 
Pole Man!

Nimeumizwa sana na Hilo!

Hebu ajaribu urine therapy,ule wa asubuhi na mapema anywe tu was kwake mwenyewe!

Nimeongozwa na mithali 5:15 ,sio tiba ngeni hata mababu,wachina na wahindi hasta king Solomon alitumia!!

Hivyo TU!!

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…