Kaptula la Marx: Unafahamu kwanini kitabu hiki kilipigwa marufuku? Waandishi wetu na Siasa zetu

Kweli hii ni changamoto kubwa inayolikabili taifa letu!

..ni CHANGAMOTO kubwa kwelikweli.

..waandishi wa vitabu [hadithi, mashairi..]hawawezi kupatikana ktk mazingira hayo ya shule zetu kuwa na uhaba mkubwa wa vitabu, haswa vitabu vya watoto.

..jambo lingine watoto wetu hawafundishwi SANAA, MUZIKI, na TAMTHILIA. Kwa hiyo itakuwa vigumu kuwa na wachoraji, wanamuziki, au waigizaji filamu, waliopikwa na wenye uwezo wa kufanya kazi na zikatambulika kimataifa.

..Na kama hatufanyi mambo yote hayo, lugha yetu adhimu ya KISWAHILI nayo tutashindwa kuihifadhi, kuikuza, na kuieneza.
 
Hakika kama taifa tunatakiwa kulifanyia kazi hili kwani mbali na kuelimisha na kuburudisha jamii, fasihi ni chanzo cha ajira kwa vijana wengi wanaohaha mitaani na vyeti mikononi!
 
Natamani mamlaka husika zingeyafanyia kazi mawazo yenu haya!
 
Hakika kama taifa tunatakiwa kulifanyia kazi hili kwani mbali na kuelimisha na kuburudisha jamii, fasihi ni chanzo cha ajira kwa vijana wengi wanaohaha mitaani na vyeti mikononi!

..wenzetu wanaweka msisitizo tangu ngazi ya awali kabisa ktk kitu wanaita "STEAM."

..S ni Science.

..T ni Technology.

..E ni Engineering.

..A ni Arts.

..M ni Mathematics.

..Mambo haya tunatakiwa tuyasisitize toka ELIMU YA MSINGI.

Cc SHIMBA YA BUYENZE
 
Aisee! Kwetu bado tunasafari ndefu sana. Maana elimu yenyewe inaendeshwa kwa mihemko ya kisiasa badala ya kuendeshwa kimkakati.
 
Aisee! Kwetu bado tunasafari ndefu sana. Maana elimu yenyewe inaendeshwa kwa mihemko ya kisiasa badala ya kuendeshwa kimkakati.

..usisubiri msaada wa serekali.

..inabidi wazazi wawe involved in their children's education.

..kama shule haina maktaba mzazi inabidi ujitoe na kununua vitabu vingi iwezekanavyo kwa watoto wako.
 
..usisubiri msaada wa serekali.

..inabidi wazazi wawe involved in their children's education.

..kama shule haina maktaba mzazi inabidi ujitoe na kununua vitabu vingi iwezekanavyo kwa watoto wako.
Wazo kuntu hili [emoji122] [emoji122] [emoji122]
 

Nimebahatika kusoma Mzingile, Rosa Mistika na Ushairi wa Karibu ndani.... ufundi mkubwa umo katika Mzingile, unasoma kitabu hamu haiishi. inafika mahala unashindwa kuelewa mwandishi ana dhima ipi? Ingawa ni dhahiri kuwa alikuwa anauchambua na kuukosoa utawala wa awamu ya kwanza ambao ulikuwa ni ule wa "zidumu fikra za Mwenyekiti".... hapo ndipo unamkuta Mhusika mkuu KAKULU.......yeye ( Kakulu) alijua kila kitu hata kuzaliwa kwake kulikuwa kwa ajabu. Alizaliwa mama akiwa akitembea huku akiwa na vinyweleo mwili mzima, mbaya zaidi alianza kutamka maneno hapo hapo.
 
Bado una hivyo vitabu?
 
Shafi A Shafi, mzee wa VUTA N'KUVUTE maarufu pia kwa riway ya KULI, amefyatua riwaya nyingine inaitwa HAINI hii ni balaa.......inaswiri kabisa kauli ya "watapata taabu sana". hebu itafute uone kilichomo, waweza kumchukia yeyote aliyemo kwenye Dola.
 
Huo ndiyo uzuri wa fasihi komavu. Unaweza kuichambua unavyotaka; na ukawa sahihi. Kakulu (Kazee) anaweza kuwa anamwakilisha Nyerere kama unavyosema: Anaabudiwa japo mawazo na fikra zake zimeshapitwa na wakati (na pengine hazikuwa sahihi kuanzia mwanzo).

Kezilahabi pia anatambulika kuwa na ugomvi mkubwa na dini hasa ya Kikristo. Inasemekana aliwahi kusoma misheni na alikuwa na lengo la kuwa padri. Sijui walimkorofisha nini huko. Katika kazi zake zote dini huwa inamsumbua. Kwenye Rosa Mistika, watu wa dini hawawezi kumsaidia Rosa kwa lolote. Katika Gamba la Nyoka, padri Madevu anamlala Mama Tinda na baadaye inagundulika kuwa alikuwa ni jasusi hatari la CIA lililotumwa kuja kudhoofisha juhudi za ujenzi wa Ujamaa nchini. Kuna wachambuzi wanaodhani kuwa Kakulu anayeongelewa katika Mzingile ni Yesu/Mungu mwenyewe!

Wachambuzi wengine wanaamini kwamba Kakulu anawakilisha maisha menyewe. Kwamba hata uzaliwe kwa namna gani; na uwe na kipaji cha kutenda maajabu na hata kuanzisha mkondo/mvuvumko wako wa kimawazo na maarifa, mwishowe utazeeka na mawazo yako yatapitwa na wakati.

Kezilahabi ni mwanafalsa. Tasnifu yake ya uzamivu (PhD) kutoka Chuo Kikuu cha Wisconsin, Madison ni juu ya falsafa ya Kiafrika. Ni mfuasi pia wa tapo la falsafa lijulikanalo kama Existentialism. Ni vizuri kuwa angalau na fununu juu ya tapo hili na jinsi linavyoyaona na kuyachambua maisha na nafasi ya binadamu kabla ya kusoma na kuzielewa sawasawa kazi zake za kifalsafa hasa Nagona na Mzingile; na hata baadhi ya mashairi yake.
 

Yumkini umevisoma sana hivi vitabu.....
Tumia jukwaa hili kutushirikisha uchambuzi mdogo kuhusu kazi hizi ikiwezekana ukurasa huu jukwaa/ kazi za/ la kezilahabi. Nahisi tumo wengi wapenzi wa kazi zake, twaweza kujifunza mengi kupitia humo.
Kaka Shimba! Fafanua kidogo kuhusu Exstentialism.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…