Shimba ya Buyenze
JF-Expert Member
- Dec 22, 2014
- 182,097
- 1,099,383
Unaongelea Ibrahim Hussein aliyeandika Mashetani? Kezilahabi ni mkimya na haongei sana. Alikuwa profesa wa fasihi mlimani mpaka alipoamua kuhamia Botswana.Kuna Wakati nilisikia kuwa Kezilahabi ni mgonjwa WA akili... Sijui ilikua kweli
Kweli hii ni changamoto kubwa inayolikabili taifa letu!
Hili inabidi litazamwe katika mfumo mpana wa kijamii. Jamii yetu inaionaje dhima ya elimu na maarifa katika maendeleo yake? Kuna faida gani ambazo Mtanzania atazipata kwa kujisomea vitabu? Kwa vile tafiti zimeonyesha kwamba usomaji wa vitabu umeporomoka sana, ni lazima tujiulize: Kwa nini watu wetu hawapendi kusoma vitabu? Je, vitabu ni ghali sana? Hakuna waandishi wazuri? Makampuni ya uchapishaji yanaendeshaje biashara zake? Ni nani anayefaidika na kazi za wanafasihi wetu? Tutafute kiini. Tuihamasishe jamii. Kufanya vinginevyo haitasaidia sana.
Natamani mamlaka husika zingeyafanyia kazi mawazo yenu haya!..ni CHANGAMOTO kubwa kwelikweli.
..waandishi wa vitabu [hadithi, mashairi..]hawawezi kupatikana ktk mazingira hayo ya shule zetu kuwa na uhaba mkubwa wa vitabu, haswa vitabu vya watoto.
..jambo lingine watoto wetu hawafundishwi SANAA, MUZIKI, na TAMTHILIA. Kwa hiyo itakuwa vigumu kuwa na wachoraji, wanamuziki, au waigizaji filamu, waliopikwa na wenye uwezo wa kufanya kazi na zikatambulika kimataifa.
..Na kama hatufanyi mambo yote hayo, lugha yetu adhimu ya KISWAHILI nayo tutashindwa kuihifadhi, kuikuza, na kuieneza.
Hakika kama taifa tunatakiwa kulifanyia kazi hili kwani mbali na kuelimisha na kuburudisha jamii, fasihi ni chanzo cha ajira kwa vijana wengi wanaohaha mitaani na vyeti mikononi!
Aisee! Kwetu bado tunasafari ndefu sana. Maana elimu yenyewe inaendeshwa kwa mihemko ya kisiasa badala ya kuendeshwa kimkakati...wenzetu wanaweka msisitizo tangu ngazi ya awali kabisa ktk kitu wanaita "STEAM."
..S ni Science.
..T ni Technology.
..E ni Engineering.
..A ni Arts.
..M ni Mathematics.
..Mambo haya tunatakiwa tuyasisitize toka ELIMU YA MSINGI.
Cc SHIMBA YA BUYENZE
Aisee! Kwetu bado tunasafari ndefu sana. Maana elimu yenyewe inaendeshwa kwa mihemko ya kisiasa badala ya kuendeshwa kimkakati.
Wazo kuntu hili [emoji122] [emoji122] [emoji122]..usisubiri msaada wa serekali.
..inabidi wazazi wawe involved in their children's education.
..kama shule haina maktaba mzazi inabidi ujitoe na kununua vitabu vingi iwezekanavyo kwa watoto wako.
Riwaya ya kwanza ya Kezilahabi wakati akiwa bado kijana. Wakati huo akiwa bado hajakomaa kifalsafa na katika Rosa Mistika falsafa yake ya maisha kama ua waridi linalopita ndiyo ilikuwa inajengwa. Ukitaka kumwelewa sawasawa na kuona ukomavu wake wa kifalsafa jaribu kusoma vinovela vyake viwili viitwavyo Nagona na Mzingile; na hata baadhi ya mashairi yake katika Kichomi na Karibu Ndani.
Bado una hivyo vitabu?Nimebahatika kusoma Mzingile, Rosa Mistika na Ushairi wa Karibu ndani.... ufundi mkubwa umo katika Mzingile, unasoma kitabu hamu haiishi. inafika mahala unashindwa kuelewa mwandishi ana dhima ipi? Ingawa ni dhahiri kuwa alikuwa anauchambua na kuukosoa utawala wa awamu ya kwanza ambao ulikuwa ni ule wa "zidumu fikra za Mwenyekiti".... hapo ndipo unamkuta Mhusika mkuu KAKULU.......yeye ( Kakulu) alijua kila kitu hata kuzaliwa kwake kulikuwa kwa ajabu. Alizaliwa mama akiwa akitembea huku akiwa na vinyweleo mwili mzima, mbaya zaidi alianza kutamka maneno hapo hapo.
Bado una hivyo vitabu?
Natafuta sana cha rosa mistika niliuliziaga maktaba ya mkoa wa moshi na moro bila mafanikio yeyotehapana........tatizo letu watz. Nilimuazimisha mtu kapotea navyo.
Huo ndiyo uzuri wa fasihi komavu. Unaweza kuichambua unavyotaka; na ukawa sahihi. Kakulu (Kazee) anaweza kuwa anamwakilisha Nyerere kama unavyosema: Anaabudiwa japo mawazo na fikra zake zimeshapitwa na wakati (na pengine hazikuwa sahihi kuanzia mwanzo).Nimebahatika kusoma Mzingile, Rosa Mistika na Ushairi wa Karibu ndani.... ufundi mkubwa umo katika Mzingile, unasoma kitabu hamu haiishi. inafika mahala unashindwa kuelewa mwandishi ana dhima ipi? Ingawa ni dhahiri kuwa alikuwa anauchambua na kuukosoa utawala wa awamu ya kwanza ambao ulikuwa ni ule wa "zidumu fikra za Mwenyekiti".... hapo ndipo unamkuta Mhusika mkuu KAKULU.......yeye ( Kakulu) alijua kila kitu hata kuzaliwa kwake kulikuwa kwa ajabu. Alizaliwa mama akiwa akitembea huku akiwa na vinyweleo mwili mzima, mbaya zaidi alianza kutamka maneno hapo hapo.
Vitabu hivi vinapatikana UDSM (Mlimani) katika maduka yao ya vitabu. Ni tuvitabu tu tumechapwa kizembe kizembe ukiviona unavidharau kumbe....Bado una hivyo vitabu?
Shukrani mkuuVitabu hivi vinapatikana UDSM (Mlimani) katika maduka yao ya vitabu. Ni tuvitabu tu tumechapwa kizembe kizembe ukiviona inavidharau kumbe....
Vipo katika maduka ya vitabu Dar pale Posta mpya. Vimechapishwa upya!Natafuta sana cha rosa mistika niliuliziaga maktaba ya mkoa wa moshi na moro bila mafanikio yeyote
Huo ndiyo uzuri wa fasihi komavu. Unaweza kuichambua unavyotaka; na ukawa sahihi. Kakulu (Kazee) anaweza kuwa anamwakilisha Nyerere kama unavyosema: Anaabudiwa japo mawazo na fikra zake zimeshapitwa na wakati (na pengine hazikuwa sahihi kuanzia mwanzo).
Kezilahabi pia anatambulika kuwa na ugomvi mkubwa na dini hasa ya Kikristo. Inasemekana aliwahi kusoma misheni na alikuwa na lengo la kuwa padri. Sijui walimkorofisha nini huko. Katika kazi zake zote dini huwa inamsumbua. Kwenye Rosa Mistika, watu wa dini hawawezi kumsaidia Rosa kwa lolote. Katika Gamba la Nyoka, padri Madevu anamlala Mama Tinda na baadaye inagundulika kuwa alikuwa ni jasusi hatari la CIA lililotumwa kuja kudhoofisha juhudi za ujenzi wa Ujamaa nchini. Kuna wachambuzi wanaodhani kuwa Kakulu anayeongelewa katika Mzingile ni Yesu/Mungu mwenyewe!
Wachambuzi wengine wanaamini kwamba Kakulu anawakilisha maisha menyewe. Kwamba hata uzaliwe kwa namna gani; na uwe na kipaji cha kutenda maajabu na hata kuanzisha mkondo/mvuvumko wako wa kimawazo na maarifa, mwishowe utazeeka na mawazo yako yatapitwa na wakati.
Kezilahabi ni mwanafalsa. Tasnifu yake ya uzamivu (PhD) kutoka Chuo Kikuu cha Wisconsin, Madison ni juu ya falsafa ya Kiafrika. Ni mfuasi pia wa tapo la falsafa lijulikanalo kama Existentialism. Ni vizuri kuwa angalau na fununu juu ya tapo hili na jinsi linavyoyaona na kuyachambua maisha na nafasi ya binadamu kabla ya kusoma na kuzielewa sawasawa kazi zake za kifalsafa hasa Nagona na Mzingile; na hata baadhi ya mashairi yake.