Karamagi ashinda Uenyekiti wa CCM Kagera

Karamagi ashinda Uenyekiti wa CCM Kagera

Halafu team sukumagang ikionekana hali ni tete kweli kweli! Ukisikia kutesa kwa zamu, ndiyo huku sasa!

Leo hii akina Bashiru Ali ndiyo wamekuwa watetezi wa wakulima! Ila alipokuwa Katibu Mkuu wa chama, alichokumbuka ni kumtetea tu Mwenyekiti na chama chake.
Bashiru asali imepungua ndio maana analalamikia asali yake. Ccm yote ni mishenzi tu haina nia na kusaidia the commoners.
 
Siasa ni mchezo mchafu mkuu.
Watu wanapomshabikia Bashiru sio kwa vile wanampenda bali kuchochea kuni ndani ya ccm wavurugane zaidi.
Nimewasoma San Leo hi bashiru shujaaa kwa lipi labda huyo mweu aliyempanga jiwe kuwa rais wa milele
 
View attachment 2424753
Aliyewahi kuwa Waziri wa Nishati na Mbunge wa Bukoba Vijijini mwaka 2005-2010 Naziri Karamagi ameibuka kidedea ametangazwa kuwa mshindi katika nafasi ya Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Kagera baada ya kupata asilimia 58 ya kura zote zilizopigwa

Karamagi amemshinda mwenyekiti anayemaliza muda wake, Costansia Buhiye aliyedumu katika nafasi hiyo kwa miaka 15.

Buhiye ameambulia asilimia 32 tu ya kura zilizopigwa.

Spika wa Bunge, Tulia Ackson ambaye alikuwa msimamizi wa uchaguzi ametangaa kuwa Karamagi amepata kura 669, Costansia Buhiye kura 452 Medard Mushobozi kura 18 na Novath Kwama kura Tano pekee.

Aidha ametangaza mshindi wa Halmashauri Kuu (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kareem Amri ambaye amepata kura 751 baada ya kumshinda Wilbroad Mtabuzi ambaye amepata kura 368 na Amani Kajuna kura 14.

HABARI LEO
Ulipo mzoga ndipo wanapokusanyika tai
 
Back
Top Bottom