Kariakoo ukiondoa Wakinga, Wachaga na wenye asili ya nchi za nje, panabaki patupu

Kariakoo ukiondoa Wakinga, Wachaga na wenye asili ya nchi za nje, panabaki patupu

Ni mada fikirish sanai ukiondoa vimelea vya sumu mwambata vijitokezavyo maswala ya aina hii yanapo jadiliwa kwa hisia.
Kariakoo hii, tunaweza kusema lilikuwa ni eneo lenye wakazi wengi wa asili hadi miaka michache iliyo pita. Kwenye miaka ya 70, Kariakoo kulikuwemo na nyumba za makuti za wenyeji. Sasa sijui wenyeji hao walio baki eneo hili ni wangapi?

Nawaza tu, kwa sababu sijui: ingetokea eneo hili likawa ni eneo ambalo lilikuwa na wakazi wa asili, baadhi ya hao walio tajwa kwenye mada; hali ingekuwa ni tofauti na hawa waliokuwa Kariakoo mwanzo?
 
Kwanini wao waendelee kuishi kama sio watanzania,

hawashiriki misiba labda awe kiongozi mkubwa,

hawataki tuoleane.

Lazima muwaoe? Mbona wao hawataki kuwaoa ndugu zako?

Wao wakioana wenyewe na nyie oaneni wenyewe ngoma draw. Hawana mpango na nyie na wewe usiwe na mpango wao.
 
Hujafanya research vizuri mzee, kuna watu kibao pale wanatokea Tanga. Kuna wale wanaosalimia Kukile, kuna wamyamwez na wasukuma wa kutosha pale. Inshort umeongea kwa kutumia common sense tu
EEEeeeennnHEeeee!
Kama ulivyo "tumia 'common sense' " wewe mwenyewe!
 
Huu uzi ulikuwa unalenga nini jamani. Mimi ni mchagga kwa asili na nimekuwa nafanya biashara kkoo miaka 20 sasa. Naomba nimsahihishe mleta uzi kidogo.
Kwanza kwa Tanzania ya leo tumeshakuwa machotara sana kiasi kwamba ni vigumu sana kukuta familia yenye watoto 5 waliooa au kuolewa asichanganye damu so hakunaga tena kabila ila kuna wakazi wa kilimanjaro Arusha tanga mbeya nk. Pili. Wakati naingia kkoo miaka ile wale watu wengi waliokuwa na mitaji na umri mkubwa kwetu wengi walishaondoka kwenye biashara za service wako kwenye biashara ya products so washakuwa japo wapo wachache waliofilisika. Wapo pia wengine wamewekeza kwenye real estate so kutokana mchakamchaka wa kkoo na umri wameshindwa kukompiti. So zaman kkoo ilikuwa makaz wapemba wakaanzisha biashara wachagga wakawapokea na kwasasa kwa kias wapo wakinga kwenye nguo nk lakini makabila mengine yapo sema kwa asili hawajitbulish na asili zao. So makabila yote yapo. Waarabu wapo wasomali wahindi nknk hata wakongo wanigeria nk
 
Kariakoo hii, tunaweza kusema lilikuwa ni eneo lenye wakazi wengi wa asili hadi miaka michache iliyo pita. Kwenye miaka ya 70, Kariakoo

Simulizi za makuzi ya mtanzania huyu toka familia ya kawaida baba akiwa dereva wa taxi na mama akiwa mama ntilie akipika vitumbua, kalimati, maandazi wakati Karim Manji akikua mitaa ya Kariakoo jijini DSM, Pugu Secondary school hadi chuo kikuu...


View: https://m.youtube.com/watch?v=CXuaO36ZLtU
Hongera Prof Karim Manji Kwa kuitangaza Tanzania na Muhimbili University
================

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amempongeza Profesa Karim Manji wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (Muhas) aliyechaguliwa kuwa miongoni mwa washindi wa tuzo ya muhitimu bora wa Chuo Kikuu cha Harvard.

Profesa Karim Manji ameokoa maisha ya watoto wengi wachanga pamoja na waliozaliwa kabla ya wakati na wenye uzito mdogo yaani ‘njiti’ katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) miaka 30 iliyopita.

Rais Samia ametoa pongezi hizo leo Jumapili, Septemba 15, 2024 kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii.

“Pongezi za dhati kwa Profesa Karim Manji, bingwa, mkufunzi na mtafiti katika eneo la tiba ya watoto na afya ya vijana, kwa ushindi wa tuzo ya Alumni Award of Merit kutoka Shule ya Afya ya Chuo Kikuu cha Harvard (Harvard T.H. Chan School of Public Health).”
 
Uwaondoe uwapeleke wapi tena, nadhani tulipofika Tanzania ni ma halfcaste wa makabila mchanyato wenye common denominator ambayo ni Utanzania... Hizo breed unazoongelea ni dying breeds zinazopotea daily
 
View attachment 3170601

Ukitaka kupunguza tatizo la msongamano Kariakoo ondoa wakinga, wachaga na watanzania wenye asili za kihindi, kiarabu, kisomali, kichina, n.k.. hawa ni almost asilimia 70 ya biashara za Kariakoo

Wanaobaki kwa mbali labda ni waha na wapemba kwa makadirikio ni asilimia 20

wanaobaki asilimia 10 ni watu wote unaowajua Tz kuanzia wamasai, wasambaa, wasukuma, wanyakyusa, wafipa, wanyaturu, wangoni, wabena, n.k.
Jaribu kuwaondoa kama hautoona baada ya siku mbili tu pamejaa. Acha kukaririshwa.
 
Uongo mtupu, hizi tafiti uchwara umezitoa wasafi kwa kina babalevo unazileta jf!!

Wewe ni mchaga au mkinga??
 
Mimi mwenyewe zamani nilijua kariakoo ni wajinga na wachaga kumbe hakuna kitu kama hicho.Hapo ni wahindi na makabila yote mchanga Yuko ya Tanzania
 
Uwaondoe uwapeleke wapi tena, nadhani tulipofika Tanzania ni ma halfcaste wa makabila mchanyato...

Waziri mstaafu na mtia nia urais wa Tanzania Prof. Mark J Mwandosya amtembelea kiongozi wake wa kijadi na ndugu kiukoo chifu Kyungu Mwakabanga III, nchini Malawi Part 1



View: https://m.youtube.com/watch?v=GHcwxLUzppk
Kwa mwaliko wa chifu Kyungu Mwakabanga III, Profesa Mwandosya, Mama Lucy Mwandosya, Sekela Mwandosya na wana familia wengine walifanya ziara ya siku tatu, Kasoba, Karonga, Malawi.

Waliwasili Kasoba jumamosi tarehe 2 Januari 2016 na kupokelewa na chifu Kyungu, kaka yake na umati mkubwa wa wana Karonga.

Siku ya pili, jumapili tarehe 3 Januari 2016 tulihudhuria ibada kanisa la kianglikana, Kasoba, lililoanzishwa na babu yake chifu Kyungu.

Baadaye tulioneshwa maeneo mbalimbali ya mji wa Karonga pamoja na jengo la makumbusho. Makumbusho ya Ksronga yako chini ya Uongozi wa chifu Kapote.

Tulipata nafasi ya kukutana na ukoo wa Mwandosya walio Karonga nchini Malawi.

Kabla ya kwenda Malawi jumamosi tulihudhuria mazishi ya Mzee Arthur Mwaitenda, Kyela.

Tanzania mipaka yake ya kikoloni iliwagawa familia, shangazi, babu, baba, mjomba na kujikuta wengine wapo Omani, Uganda, Malawi, Mozambique, Congo, Zambia, RwandaBurundi huku wengine wakiwa Tanganyika n.k
 
Simulizi za makuzi ya mtanzania huyu toka familia ya kawaida baba akiwa dereva wa taxi na mama akiwa mama ntilie akipika vitumbua, kalimati, maandazi wakati Karim Manji akikua mitaa ya Kariakoo jijini DSM, Pugu Secondary school hadi chuo kikuu...


View: https://m.youtube.com/watch?v=CXuaO36ZLtU
Hongera Prof Karim Manji Kwa kuitangaza Tanzania na Muhimbili University
================

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amempongeza Profesa Karim Manji wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (Muhas) aliyechaguliwa kuwa miongoni mwa washindi wa tuzo ya muhitimu bora wa Chuo Kikuu cha Harvard.

Profesa Karim Manji ameokoa maisha ya watoto wengi wachanga pamoja na waliozaliwa kabla ya wakati na wenye uzito mdogo yaani ‘njiti’ katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) miaka 30 iliyopita.

Rais Samia ametoa pongezi hizo leo Jumapili, Septemba 15, 2024 kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii.

“Pongezi za dhati kwa Profesa Karim Manji, bingwa, mkufunzi na mtafiti katika eneo la tiba ya watoto na afya ya vijana, kwa ushindi wa tuzo ya Alumni Award of Merit kutoka Shule ya Afya ya Chuo Kikuu cha Harvard (Harvard T.H. Chan School of Public Health).”

Stori za namna hiyo mbona zipo nyingi tu siku hizi mkuu 'Bagamoyo'.
Tatizo ni kuwa nyingi haziko 'documented'.

Ulisha wahi kumuuliza mtu kama Kalamaganda Kibudu stori zake hadi hapo alipo fikia?

Wapo wengi sana; ila wengi wana kengeuka wanapofika huko juu na kujisahau waliko tokea.
 
Ni mada fikirish sanai ukiondoa vimelea vya sumu mwambata vijitokezavyo maswala ya aina hii yanapo jadiliwa kwa hisia.
Kariakoo hii, tunaweza kusema lilikuwa ni eneo lenye wakazi wengi wa asili hadi miaka michache iliyo pita. Kwenye miaka ya 70, Kariakoo kulikuwemo na nyumba za makuti za wenyeji. Sasa sijui wenyeji hao walio baki eneo hili ni wangapi?

Nawaza tu, kwa sababu sijui: ingetokea eneo hili likawa ni eneo ambalo lilikuwa na wakazi wa asili, baadhi ya hao walio tajwa kwenye mada; hali ingekuwa ni tofauti na hawa waliokuwa Kariakoo mwanzo?
Wengi wamehamia magomeni ndiyo hawa akina Mohammed Said japo yeye ni mmanyema
 
Au mpka nikupe journal niliyoweka finding zangu pale?
EEEEEEHEE!

Bado haitoshi mkuu!
Hiyo 'journal' umei-'publish' kwenye 'peer reviewed publication'?

Au basi tuseme, umejitahidi na kuweka kwenye maandishi 'observations' zako. Hiyo ni hatua mbele kuliko ile ya yule jamaa wa 'common sense'; sasa angalao wapelekee jamaa wa pale Taasisi ya Takwimu hiyo journal yako waifanyie kazi na kuipa utakaso kidogo wa ziada.
Ukifanya hivyo, maswala ya 'common sense' yatakuwa yamefutika.
 
Back
Top Bottom