Pre GE2025 Karibu Watanzania wote wana asili na ushabiki wa Simba au Yanga; basi angalieni ofa za ufadhili wa timu zenu isiwe kampeni ya uchaguzi mkuu 2025!

Pre GE2025 Karibu Watanzania wote wana asili na ushabiki wa Simba au Yanga; basi angalieni ofa za ufadhili wa timu zenu isiwe kampeni ya uchaguzi mkuu 2025!

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Tunaelekea kwenye uchaguzi wa 2025, na ghafla tunaanza kusikia ofa za ufadhili wa Simba na Yanga, wakati timu za ligi kuu zipo nyingi. Kwa nini?

Tatizo sisi Watanzania huwa tunaghiribiwa kirahisi sana. Tuliwahi kuuza nchi na watu wetu huko nyuma kwa zawadi za shanga na vioo vya kujitazamia kutoka kwa Waarabu. Haka katabia kabaya bado tunako. Hatuangalii mbali, hassa pese inapotembezwa. Sasa nawaonya Watanzania wenzangu, tuwe macho, kwamba hizi mbinu za kusema tunafadhili au tutawatafutia ufadhili wa timu ambazo wengi wenu mna ushabiki nazo isije ikawa ni kwa ajili ya kuwalainisha kutoa kura zenu 2025.

Kumbukeni kwamba, nikigombea uraisi, na 60% ya wanachama na mashabiki wa Simba na Yanga wakanipigia kura, napita kuwa raisi kiulaini sana!

Kuleni fedha za ufadhili watakazowaletea, lakini pigeni kura kuchagua watu wanaotufaa sio kwa sababu ya shukurani kwa ufadhili wa timu yako!

Pia soma:Uzi Maalum wa Kauli tata na za kushangaza kutoka kwa Viongozi na Wanasiasa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
 
Mbona hilo liko wazi. Kwenye Simba day na Yanga day haukuona simu zinapigwa live? Pamba day, sijui nani day ulisikia simu?
 
Mbona hilo liko wazi. Kwenye Simba day na Yanga day haukuona simu zinapigwa live? Pamba day, sijui nani day ulisikia simu?
Na vitendo hivi vinanajisi tasnia ya michezo nchini. Kwa nini hawa watu wako desparate kisi hiki lakini?
 
Nje mada. Hivi ni kweli Kuna watu wanampigia mtu kura kisa amepewa mshiko? Kwani huko nakopiga kura yeye anakuwepo?
 
Nje mada. Hivi ni kweli Kuna watu wanampigia mtu kura kisa amepewa mshiko? Kwani huko nakopiga kura yeye anakuwepo?
Kwani unaposikia rushwa katika chaguzi hao wanaotoa rushwa wanakuwapo wakati watu wanapiga kura?
 
Tunaelekea kwenye uchaguzi wa 2025, na ghafla tunaanza kusikia ofa za ufadhili wa Simba na Yanga, wakati timu za ligi kuu zipo nyingi. Kwa nini?

Tatizo sisi Watanzania huwa tunaghiribiwa kirahisi sana. Tuliwahi kuuza nchi na watu wetu huko nyuma kwa zawadi za shanga na vioo vya kujitazamia kutoka kwa Waarabu. Haka katabia kabaya bado tunako. Hatuangalii mbali, hassa pese inapotembezwa. Sasa nawaonya Watanzania wenzangu, tuwe macho, kwamba hizi mbinu za kusema tunafadhili au tutawatafutia ufadhili wa timu ambazo wengi wenu mna ushabiki nazo isije ikawa ni kwa ajili ya kuwalainisha kutoa kura zenu 2025.

Kumbukeni kwamba, nikigombea uraisi, na 60% ya wanachama na mashabiki wa Simba na Yanga wakanipigia kura, napita kuwa raisi kiulaini sana!

Kuleni fedha za ufadhili watakazowaletea, lakini pigeni kura kuchagua watu wanaotufaa sio kwa sababu ya shukurani kwa ufadhili wa timu yako!

Pia soma:Uzi Maalum wa Kauli tata na za kushangaza kutoka kwa Viongozi na Wanasiasa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Ingia CCM mkuu kama unataka kufaidika na Yanga na Simba. Hizi ni taasisi zilizochangia upatikanaji wa uhuru wa Tanzania. Na CCM ni zao la muunganiko wa TANU na ASP.

Karume aliyechangia ujenzi wa majengo ya timu hizi mbili ni Rais wa kwanza wa serikali ya Mapinduzi Zanzibar, huwezi kukwepa siasa za nchi hii na uwepo wa Simba na Yanga.
 
Ingia CCM mkuu kama unataka kufaidika na Yanga na Simba. Hizi ni taasisi zilizochangia upatikanaji wa uhuru wa Tanzania. Na CCM ni zao la muunganiko wa TANU na ASP.

Karume aliyechangia ujenzi wa majengo ya timu hizi mbili ni Rais wa kwanza wa serikali ya Mapinduzi Zanzibar, huwezi kukwepa siasa za nchi hii na uwepo wa Simba na Yanga.
Hapo ndipo tunapoachana Mkuu - kwamba siku zote tunafanya mambo ili kufaidika. Mtu anachaguliwa kuwa waziri na tunatarajia afaidike. Unaamua kuchagua upande fulani ili ufaidike. Kwa nini hatufanyi mambo ili Tanzania ifaidike?

Mie ningekuwa raisi wa Tanzania, ningewakuza sana watu wa upinzani ili nchi ifaidike. Ningehakikisha nawajengea uwezo hadi wawe washindani halisi wa CCM, ili kuwe na ushindani wa kweli na chama kinachotawala watambue kwamba wakifanya uzembe wataondoka, kama ilivyo UK au USA. Na ningewaamsha watu wafikie mahali wasikipigie kura chama kwa sababu tu wao ni wanachama wa chama hicho. Ningewajengea falsafa kwamba unaweza kuwa CCM ukakipigia Chadema, au ukawa Chadema ukaipigia CCM. Tukifika hapo Tanzania itaendelea kwa kasi sana, tunawaeza hata kuwazidi South Africa, Nigeria na Egypt kwa kuwa na uchumi ulio na nguvu, biggest economy in Africa.

Naikitika sana hakuna mtu atakaetokea kuwa raisi atakuwa na mawazo kama yangu, na mie sina mpango wa kuingia kwenye huo wendawazimu wa siasa za Tanzania zinazotaka lazima uwe na roho mbaya
 
Ingia CCM mkuu kama unataka kufaidika na Yanga na Simba. Hizi ni taasisi zilizochangia upatikanaji wa uhuru wa Tanzania. Na CCM ni zao la muunganiko wa TANU na ASP.

Karume aliyechangia ujenzi wa majengo ya timu hizi mbili ni Rais wa kwanza wa serikali ya Mapinduzi Zanzibar, huwezi kukwepa siasa za nchi hii na uwepo wa Simba na Yanga.
Wakati huo ilikuwa rahisi sana, hatukuwa na mfumo wa vyama vingi. Kumbuka kabla ya vyama vingi kuanza, Yanga walikuwa wanaishangilia timu ya "CCM, CCM, CCM", hata wakicheza mechi za ndani, kwa mfano dhidi ya Simba. Ushangiliaji huo ulikoma baada ya vyama vingi kuanza, hivyo si ajabu Karume kuchangia uwanja wa Yanga. Uliza maveteran watakuambia.
 
Walio wengi si wajinga,hata kama hawasikilizwi kisiasa,lakini baada ya kazi ngumu ya kutafuta ugali,ili kuondoa stress ni utani wa klabu hizo mbili..
Utamaduni wa vilabu vyetu vya Simba na Yanga ni utani na upendo.
Hawataki stress na maisha yanasonga.
Nadhani Chadema jaribu kujifunza kitu,hata kabla hamjaanza kutambaa.
 
Mie siyo Simba wala Yanga, nikiwaambia watu huwa wanabisha as if watanzania wote ni mashabiki wa hizo timu za Kariakoo, siyo kweli.
 
Wakati huo ilikuwa rahisi sana, hatukuwa na mfumo wa vyama vingi. Kumbuka kabla ya vyama vingi kuanza, Yanga walikuwa wanaishangilia timu ya "CCM, CCM, CCM", hata wakicheza mechi za ndani, kwa mfano dhidi ya Simba. Ushangiliaji huo ulikoma baada ya vyama vingi kuanza, hivyo si ajabu Karume kuchangia uwanja wa Yanga. Uliza maveteran watakuambia.
Huwezi kuwazuia wanachama wakongwe wa Yanga na Simba kuwa na kadi za CCM. Manara kawa maarufu kwenye mpira lakini ni mwanaCCM kindakindaki. Jamhuri Kihwelo alishagombea udiwani kule kwao Kigogo kupitia CCM.

Kama wewe ni CHADEMA itakubidi ujiandae kisaikolojia katika suala zima la kukubali kuwa hizi timu mbili za Kariakoo ni mali ya siasa za CCM.
 
Back
Top Bottom