Pre GE2025 Karibu Watanzania wote wana asili na ushabiki wa Simba au Yanga; basi angalieni ofa za ufadhili wa timu zenu isiwe kampeni ya uchaguzi mkuu 2025!

Pre GE2025 Karibu Watanzania wote wana asili na ushabiki wa Simba au Yanga; basi angalieni ofa za ufadhili wa timu zenu isiwe kampeni ya uchaguzi mkuu 2025!

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Hapo ndipo tunapoachana Mkuu - kwamba siku zote tunafanya mambo ili kufaidika. Mtu anachaguliwa kuwa waziri na tunatarajia afaidike. Unaamua kuchagua upande fulani ili ufaidike. Kwa nini hatufanyi mambo ili Tanzania ifaidike?

Mie ningekuwa raisi wa Tanzania, ningewakuza sana watu wa upinzani ili nchi ifaidike. Ningehakikisha nawajengea uwezo hadi wawe washindani halisi wa CCM, ili kuwe na ushindani wa kweli na chama kinachotawala watambue kwamba wakifanya uzembe wataondoka, kama ilivyo UK au USA. Na ningewaamsha watu wafikie mahali wasikipigie kura chama kwa sababu tu wao ni wanachama wa chama hicho. Ningewajengea falsafa kwamba unaweza kuwa CCM ukakipigia Chadema, au ukawa Chadema ukaipigia CCM. Tukifika hapo Tanzania itaendelea kwa kasi sana, tunawaeza hata kuwazidi South Africa, Nigeria na Egypt kwa kuwa na uchumi ulio na nguvu, biggest economy in Africa.

Naikitika sana hakuna mtu atakaetokea kuwa raisi atakuwa na mawazo kama yangu, na mie sina mpango wa kuingia kwenye huo wendawazimu wa siasa za Tanzania zinazotaka lazima uwe na roho mbaya
CCM ina miaka 47 ni vigumu sana kwa kizazi cha walio hai sasa kutokuwa na ushawishi au mahusiano na hiki chama.
Huyo Msigwa aliyekuwa hatari sana huko CHADEMA alitoka upinzani akaja CCM na kupokelewa katika mkutano mmojawapo kule Dodoma. Na wengi tu hufanya hivyo.
 
Huwezi kuelewa. Hizi ni topics zinahitaji akili kubwa kuzi discuss.
Hakuna akili yoyote kubwa siasa za nchi hii ndivyo zilivyo na huwezi kufanya lolote lile kuzibadili.

Kubali uishi kama jamii inavyoishi au toka nje nenda kaishi huko Kenya au Somalia.
 
Kuna siku wataondoka tu, kwa namna moja au nyingine. Walikuwepo KANU Kenya, UNIP Zambia, UPC Uganda, wako wapi? Inahitaji tukio moja tu watu kuamua, kuna siku itatokea
Ni ngumu polisi, tume fake ya uchaguzi, mahakama, TISS na jeshi vyote ni matawi ya CCM
 
Hakuna akili yoyote kubwa siasa za nchi hii ndivyo zilivyo na huwezi kufanya lolote lile kuzibadili.

Kubali uishi kama jamii inavyoishi au toka nje nenda kaishi huko Kenya au Somalia.
Kwa hiyo Tanzania ni taifa la watu waliokata tamaa?
 
CCM ina miaka 47 ni vigumu sana kwa kizazi cha walio hai sasa kutokuwa na ushawishi au mahusiano na hiki chama.
Huyo Msigwa aliyekuwa hatari sana huko CHADEMA alitoka upinzani akaja CCM na kupokelewa katika mkutano mmojawapo kule Dodoma. Na wengi tu hufanya hivyo.
Kuna mwandishi maarufu alisema tatizo la Africa ni kwamba ni bara pekee duniani ambalo wezi wanashangiliwa na wale wanaoibiwa!
1724758563799.png
 
Huwezi kuwazuia wanachama wakongwe wa Yanga na Simba kuwa na kadi za CCM. Manara kawa maarufu kwenye mpira lakini ni mwanaCCM kindakindaki. Jamhuri Kihwelo alishagombea udiwani kule kwao Kigogo kupitia CCM.

Kama wewe ni CHADEMA itakubidi ujiandae kisaikolojia katika suala zima la kukubali kuwa hizi timu mbili za Kariakoo ni mali ya siasa za CCM.
Hakuna mahali nimesema si sawa wanachama wa Simba na Yanga kuwa na uanachama wa vyama vya siasa. Elewa mada Mkuu
 
Kwa hiyo Tanzania ni taifa la watu waliokata tamaa?
Kuzipenda Simba na Yanga na kuupenda mpira sio kukata tamaa, achana na haya mawazo hasi yanayojaa chuki, hasira na roho mbaya.

Kuna watanzania wenzetu wengi tu wenye kufaidika na kukua kwa hizi timu. Ni walipa kodi wenzetu hivyo dunia uliyonayo kichwani mwako sio halisia.
 
Hakuna mahali nimesema si sawa wanachama wa Simba na Yanga kuwa na uanachama wa vyama vya siasa. Elewa mada Mkuu
Yanga na Simba kuwa hivi zilivyo hakuna tunachoweza kufanya kuibadilisha hali. CCM imezaliwa kutoka kwa TANU na ASP ambavyo ni vyama vyenye uhusiano wa moja kwa moja na mpira wa Tanzania.

Laumu historia yetu vinginevyo unapaka rangi upepo.
 
tatizo ni upinzani wanajitenga na fursa nyingi za siasa.
kama akuna kosa kisheria sawa tu kwani mbaya nini!
 
Inashangaza mpaka leo hujui kuwa Simba na Yanga ndio siasa ya Tanzania. Pole
 
Back
Top Bottom