Karipio la Rais Samia: Unaiba hela ya Umma ikusaidie nini? Utazikwa nayo? Utajibu nini Mbele ya Mungu?


Na wizi wa chama chake kutumia nguvu kuiba kura asiusahau au Mungu Huo hauoni?
 
Ya kaisari mpe kaisari ya Mungu mpe Mungu hiyo. Watu wanaangalia matumbo yao tuuu kwa Mungu atajua huko huko akifika.
 
Alifikiri kujinyenyekeza kwa majizi/mafisadi watamuacha salama kumbe unawafanya wakuone huna lolote na wanakupiga vzr huku wakijitahidi kukupamba kuwa unaupiga mwingi na wewe ni bora kuliko mwendazake mama ukicheka na nyani utavuna mabua shauri yako
 
Wahenga walisema "..Ukicheka na NYANI, utavuna MABUA.."

JPM tutakukumbuka daima
Hakika ,angekuwepo Leo tungeambiwa Mashirika ya Umma yanafanya kazi nzuri,ikiwemo ATC ,na yangetoa gawio Serikalini😌😌😌
 
Hakimu wa haki ni Mungu
Sisi kama walokole tunasimama na kauli ya Mama.
Mungu atahukumu na watakufa wataziacha mali.
Mtu akikudhulumu ht usipambane ili kurudisha haki yako, ww tulia tuu ukimuachia Mungu ili lile neno la kuangamia kwa kukosa maarifa litimie
 
wezi wamevunja kanuni zilizowekwa ndo maana wanaiba na hakuna kitu kibaya kinawatokea, endelea kusema hukumu ya Mungu wakati watu walishavuka mstari hawana cha kuogopa na wanapiga kweli kweli.
Wamegeuza Katiba...maandishi yameangalia chini.Wanapiga tu bila kuangalia
 
Tukaze roho tupitishe sheria ya kifo kwa mtu yeyote ambaye atabainika kuhujumu uchumi kwa makusudi na kutoa rushwa.

Mtaona kama huu upuuzi utaendelea.
 
Mkuu Sheria ya kunyonga si bado ipo hai? Hebu tundika wawili watatu hv tukuelewe🤣🤣
 
Na ukiiba au ukila rushwa, sheria ni wanakutwanga risasi. Unafikiri wachina wamefikaje hapo? Hakuna mzaha kwenye mali ya umma. Wamagharibi wakawaita kila majina, ooh madikteta, waminyaji haki, waliziba masikio. Leo JPM ataendelea kukumbukwa.
 
Wawajibike na iwe fundisho kwa wengine. Mali zao zote zichunguzwe.
Ndo mambo aliyokuwa akipambana nayo Magu, baadhi ya viongozi waliozoea upigaji na wafanyabiashara wakamuona mbaya. Hii nchi kuna asilimia kiasi fulani ya biashara zinaenda kwa kulipa kodi kiujanja ujanja na udanganyifu. Malipo ya serikali ndo bei zinaongezwa sana bila kusahau wizi wa mali za chama. Ilibidi tu JPM aondoke. Leo hii kuna watu wanathubutu kusema "chama kimerudi kwa wenyewe" "msile sana" inafikirisha, sijui ili watu waendelee "kufanya walivyozoea" Kwamba yule msukuma alikuja "kuziba rizki zetu" Haya ndiyo matokeo, mengi yatajitokeza, bado sana
 
Maza anatuangusha sn hafai yaani aibu kuwa na mkuu wa nchi wa namna hii naameapa kulinda katiba ya nchi maanake ni maslahi ya kwa mali za umma, kama hawezi kulinda mali za umma hatufai hata kdg
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…