Kwa mara ya kwanza naomba niandike maelezo ya ziada;
- Kisa hiki ni kisa cha ukweli kabisa (wahusika wamebadilishwa kuficha uhalisia)
- hata mimi mwandishi bado nipo kwenye dilemma ya kujua nani hasa ahukumiwe (au ahukumiwe zaidi) na ndiyo maana nikafikiria kuweka poll hapo juu.
Zaidi sana, ni lengo la mimi kuelezea mkasa huu;
- HUKUMU: Kabla hujamchukia na kumhukumu mtu kwa alilokufanyia, jichunguze kama hukuwahi kufanya kama yeye. Haimaanishi kwa kila kosa basi tunastahili adhabu lakini itatufanya kuwa wapole wakati mwingine tunapofikiria kumuumiza mtu mwingine. Mara nyingi, hasa kwenye mahusiano (na hii imenikuta hivi karibuni) unamchukia mtu kwa kosa alilokufanyia. Unamtukana na kutumia maneno makali kuwa hakukupenda ndiyo maana akakufanyia A, B, C. lakini ukikaa kidogo ukafikiria 2012 huko Kidamali, utagundua nawe uliwahi kumfanyia mwingine sawa (au zaidi) ya yale uliyofanyiwa. Ila kwa kuwa sasa kibao kimegeuka kwako, huuoni uovu wako ila wa yule aliyekutenda sasa. BIN ADAMU!
- HISTORIA: Uliyoyafanya kwa kificho, yatadhihirishwa mwangani siku moja. Mara nyingi tunafanya mambo kwa kuamini hayatakuja kutuumbua mbeleni. Kuna nyakati tunafanikiwa. Lakini, amin nakuambia, ipo siku uovu unaoufanya ukijua ni uovu utakuja kuku-haunt.
- NAFASI: Unayo nafasi ya kurekebisha na kuanza upya. Zaidi sana, unayo nafasi sasa ya kutafakari na kuishi sawa. Mfalme Daudi kwenye aya niliyoandika, alijuta na kutubu (kwa bahati mbaya kwake dhambi yake ilisababisha kifo/vifo) lakini alirejeshewa baraka zake. Alirekebisha mwenendo wake na Mungu akamrejeshea ufalme wake. Kwa kiingereza kuna mahali imeandikwa, "God considered him, a man after God's own heart." Inawezekana kurekebisha, inawezekana kuanza upya kwa usahihi na inawezekana kutafakari sasa na kuepuka kufikia kwa Daudi na Mentor.
Wasalaam wapendwa,
Mentor.