Karne ya 21 Katibu Mkuu wa CWT alikuwa mwalimu wa Daraja la 3A?

Karne ya 21 Katibu Mkuu wa CWT alikuwa mwalimu wa Daraja la 3A?

Tatizo linaanza na kiongozi wa juu, utakuwaje wewe mzalendo huku boss wako siyo mzalendo? ukionekana mwadilifu utaundiwa zengwe hata kufukuzwa kazi, taasisi za umma zimejaa TISS wanakazi gani kama wanashindwa kuzuia ufisadi? PM 2021 alikuta jamaa(Wizara ya fedha) wamepiga Extra duty 2B kwenye Mei mosi, akaaunda tume mpk leo umepewa mrejesho? kuna Afisa anaweza kutoa pesa nyingi hivyo bila KM na Waziri kujua? chain ya wizi inaanzia juu kushuka chini.
Mkuu umeongea ukweli lakini hao viongozi wanatoka kwenye familia zetu. Familia zenye maadili zitajenga taifa zenye maadili.
 
Mkuu umeongea ukweli lakini hao viongozi wanatoka kwenye familia zetu. Familia zenye maadili zitajenga familia zenye maadili.
Tunatakiwa kujenga mifumo imara, kipindi cha Magu watu wengi walianza kuogopa kuiba maana walikuwa wanapigwa uhujumu uchumi, toka amekufa nani amekamatwa kwa uhujumu uchumi? Leo hii ninaweza kumuona DC anafanya vitendo vya hovyo na sina la kumfanya mpk Rais apende, TAKUKURU ipo ajii ya kukimbizana na VEOs na WEOs. Serikalini kuna wizi mkubwa sn report ya CAG hata robo ya wizi huwa haitaji huwa inawataja tu ambao wamegoma kutoa rushwa, nilifanya kazi ya kujitolea halmshauri Idara ya mipango watu wa CAG ni wala rushwa kupita kiasi.
 
CWT ni laana!!

Walimu wapo darasani wana Masters kiongozi wao mkuu kama Katibu mkuu ni form four grade 3A?

Tena anateuliwa kuwa mkuu wa Wilaya akaringa!!
Kwenye CCM elimu ni sifa ya ziada. Wenye elimu wamewahi kufeli vibaya sana walipokabidhiwa hatamu za kichama. Wajinga CCM wana matokeo makubwa sana ya kazi za chama kuliko werevu. Elimu siyo sifa ya msingi CCM tangu waasisi wake. Kukuthibitishia, wafuatao wamesoma vyuo vikuu vipi duniani hapa? Kama iko tanbihi yao tupe.

1. Sheikh Tabith Kombo Jecha.
2. Sheikh Abeid Amani Karume.
3. Sheikh Aboud Jumbe (mzaliwa wa Juba Sudan Kusini) alikuwa na Diploma tu ya ualimu.
4. Rashid Mfaume Kawawa.
5. Sheikh Ali Hassan Mwinyi.
6. Amani Karume.
7. Idriss Abdul Wakil.
8. Bibi Titi Mohammed.
9. Sophia Kawawa.
10. Nk nk.

Mwalimu alipenda kufanya kazi na under-educated na hii imerithiwa na chama hadi kesho.
 
Hicho chama ni cha kushurutishwa? Kwanini kila mwalimu akatwe ada ya CWT hata kama hapendi kuwa mwanachama?
 
Mwalimu Mwandamizi Daraja la A ni daraja IA na siyo 3A kama huyu mrusha post anavyowadanganya kwa sababu ya umbumbumbu amwake wa kuelewa. Mwalimu Mwandamizi maana yake ni Senior Teacher na mshara wake wa Mwalimu mwandamizi daraja la IA unaanzia 2, 800,000 plus. Kwa hiyo mpuuzeni huyu mtoa post kwani yeye alipoona mwamimu mwandamizi IA akakurupuka haraka akidhani ni 3A ambao ni mshahara anaoanza na mtumishi awe nwalimu au siyo mwalimu.
Mshahara wa mwalimu wa certificate unagotea daraja E hio million mbili umetoa wap??
 
Huyu anaitwa Maganga Japhet very intelligent,mcheshi,hana mengi. Siasa iliingia CWT na ilipoingia yeye akiwa ndo mtendaji Mkuu akawa ananyooka hakati kona kona nyingi tambua ni CPA holder na ndiye afisa masuhuri wa CWT by then hela haitoki bila sahihi yake na Kuna watu kibao wanataka kuchezesha kwa madai wana shida hasa previous leaders wa CWT mshkaji hakutaka ndo wazee wa chama kijani wakaombwa wamshauri apewe udc nafasi ambayo ilipewa kwake pasipo hata upekuzi/vetting yeye na wenzie maana walifuatwa mwezi 1 kabla ili waachie ngazi dili zipigwe. Ila jamaa akachomoa coz ilikuwa mtego kwenda Kyerwa then wamfyatue akazipata za ndani akaona Kama mbwai iwe......
Then wakamnyima kibali na kazi wakamwambia mtoto,CWT wanasema ili aendelee alete kibali Cha mwajiri wakati TAMISEMI wamekula kichwa, FITNA NYINGI SANA
 
Kuna diwani darasa la saba, amechaguliwa kuwa mwenyekiti wa madiwani ngazi ya Wilaya. Wasomi wapo ila nani amfunge paka kengele shingoni aliwe? Panya wanabishana kuhusu kumfunga paka kengele shingoni ili akipita sauti ya kengele isikike.
 
Back
Top Bottom