Karume hakusaini hati ya muungano

Karume hakusaini hati ya muungano

Mkuu Manyimbo,
Labda nikuulize, jee unajua chochote kuhusu kitu kinachoitwa Kuchafuka kwa hali ya hewa ya kisiasa Zanzibar?!.

Aboud Jumbe ndie rais aliyempokea Karume baada ya kuuwawa, nini kilimtokea?!. alifanya nini?!, na akafanywa nini?!.

Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, enzi hizo ilikuwa ni Wolfgang Dourado!, find out, aliandaa document gani, kuhusu muungano ambayo Jumbe alikuwa aipeleke UN, jee document hiyo ilikuwa na nini, na huyo Dourado nini kilimkuta?!.

Find out wakati wa mchafuko huo, Waziri Kiongozi wa SMZ alikuwa nani na alifanya nini?!.

Pasco

Pasco,

kwa kila hali katika maandiko yako haya umeonekana kuweka ushabiki pembeni na hivyo kufunua vilivyofunikwa ili ukweli na uwongo ufahamike. Ni kutokana na ukweli huo ndo namimi nikakuomba unifafanulie kuhusiana na tuhuma za kuwa Maalim Seif alimtosa Aboud Jumbe ambaye kwa namna ulivyoonesha alikuwa njiani kuquestion muungano katika Jumuiya ya kimataifa. Maali seif ni nikiongozi mwandamizi wa kichama na serekali after all yeye ni katika viongozi wanaoongoza umma wa wazanzibari katika kupigania mamlaka kamili ya nchi yao.

Sasa basi Kwa vile wewe unao ushahidi juu ya jambo hili haina haja ya mimi kuanza kuhangaika na documents ambazo kwa mahali nilipo kamwe siwezi kuwa na access nazo. Naomba ulieleze vizuri hili jambo kwa lengo la kumtendea haki maalim seif pamoja na wale anaowaongoza. Kama utaamua kuwa huwezi kulieleza kwa sababu yeyote iwayo, basi ningekuomba umtake radhi maalim seif pamoja na wafuasi wake kutokana na kumdhalilisha kwa maelezo yako ambayo ni ya kupika, uzushi na unafiki uliopindukia.

Katika post zako hizi, umekuja kwa namna tofauti na ulivyozoeleka, inaonesha umekusudia kuweka mambo hadharani, sasa kama hivyo ndivyo ni kipi kinachokushinda kulieleza jambo hili kwa uwazi na ufasaha mpaka unitake mimi kwenda maktaba kusoma hali ya kuwa wewe unajua kila kitu vilivyo?

Nasubri ufafanuzi juu ya usaliti wa maalim seif OR an apology for your misleading information.
 
Wanabodi,

Wakati sintofahamu kuhusu Hati Halisi za Muungano, ikiendelea, nawaomba Watanzania wenzangu tufike mahali tuambiane ukweli halisi kuwa Hati Halisi za Muungano", hazipo popote!, nakala iliyowasilishwa kwenye Bunge Maalum la Katiba, yenye saini ya Nyerere na Pius Msekwa!, ile sio hati ya muungano (Articles of The Union" bali ile ni Sheria ya Muungano!, "The Act Of Union!" iliyotungwa na Bunge la Tanganyika, ku ratify the "Artcles of Union", ambayo imesainiwa na Nyerere, Speker wa Bunge na Msekwa kama Katibu wa Bunge wa Wakati Huo!.

Msekwa was never a signatory kwenye Artcles of The Union!".

Signatories kwenye "Artcles of The Union" ni
  1. Mwalimu Julius Nyerere-Rais wa Jamhuri ya Tanganyika
  2. Sheikh Abedi Amani Karume- Rais wa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar
  3. Mwanasheria Mkuu wa Tanganyika -Fifthfoot
  4. Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar (Wolfgang Dourado-Alipewa likizo ya lazima nje ya nchi, Akaletwa mwanasheria wa Ghana kuusimamia muungano, ukasainiwa na Mwanasheria Mkuu wa Tanganyika pekee!)
Hati Hizi hazipo Idara ya Nyaraka na kumbukumbu za Taifa Nimezungumza na Mtanzania wa Kwanza kuwa mkuu wa Idara ya Kumbukumbu, Mzee Mongela, hakuwahi kuziona hati hizo wala hata copy yake!.
Nikazungumza na Mkurugenzi wa Nyaraka aliyepita Bwana Mlyansi, pia amekiri kutoziona hati hizi!. Nikazungumza na Mkurugenzi wa Nyaraka aliyeko sasa Bw. Magai!, hati hizo hazipo!.

Ule uongo wa kuwa eti hati ziko UN, nimewahi kuzifuatilia mpaka huko UN hati hizo hazipo!.

Kipindi hiki cha Bunge Maalum sasa ndicho kipindi muafaka tuelezane ukweli bayana kuwa hati hizo are no where to be seen!, tuelezwe vizuri tuu kuwa kwa bahati mbaya zililiwa na mchwa hivyo zimetoweka zote kwa pamoja!.
  1. Nakala halisi ya Serikali ya Tanganyika, imetoweka!
  2. Nakala halisi ya SMZ, imetoweka!
  3. Nakala halisi ya Bunge la Tanganyika-imetoweka!
  4. Nakala halisi ya BLW nayo imetoweka!
  5. Nakala halisi ya Mwanasheria Mkuu -imetoweka!.
  6. Nakala halisi ya Nyerere-imetoweka
  7. Nakala halisi ya Karume -imetoweka!
Hili suala la hati halisi za Muungano nimelizungumza
Hapa-Swali: Hivi Muungano Tanzania Upo Kweli?! au ni Dhana Tuu?!

Na Hapa-Jee Wajua Kuwa Tanzania Hatuna Mkataba wa Muungano?. Kilichopo ni Makubaliano Tuu?!.

Na Hapa-Je, wajua kuwa Zanzibar haikuridhia Muungano? Ina Maana Gani?!.

Na Hapa-Jee Wajua Kuwa Kuna Uwezekano Tanzania Sii Nchi Halali Kisheria?!.



Kwa kuanzia jee Nakala Halisi za Muungano ziko wapi?.

Pasco


Mkuu Pasco

Heko sana Mkuu Pasco kwa jitihada zako hizi za kuweka kumbukumbu mujarabu za hili sakata la Muungano.

Kwa mara ya kwanza, nakuvulia kofia kwa kauli yako thabiti hapo juu [kwenye bluu and bold]

Endelea kuwa nuru Mkuu uwamulike na uwamulikie wengi wanaojitia upofu wa fikra.

Much respect
 
Its a waste of time and resource, I think, to doubt the regitimacy of the Union 50 years of its existance.

Footages are awash showing abeid karume and julius nyerere signing the articles of the union before cameras, and was followed by the formation of the union government.

the best option now is to focus on the ways to improve the state of the union to fit current needs and expectations of the new generation. so Trivial allegations that it was not 'ratified' is both time-barred and un-fruitfull to both parties.

in conclution...the most dangerous enemy of our time are the greeedy and selfish politicians, whose motives are to divide and confuse people to create avenues for self-enrichment! They are of all colours and are found everywhere....BEWARE
 
Its a waste of time and resource, I think, to doubt the regitimacy of the Union 50 years of its existance.

Footages are awash showing abeid karume and julius nyerere signing the articles of the union before cameras, and was followed by the formation of the union government.

the best option now is to focus on the ways to improve the state of the union to fit current needs and expectations of the new generation. so Trivial allegations that it was not 'ratified' is both time-barred and un-fruitfull to both parties.

in conclution...the most dangerous enemy of our time are the greeedy and selfish politicians, whose motives are to divide and confuse people to create avenues for self-enrichment! They are of all colours and are found everywhere....BEWARE

Naunga mkono hii hoja

Hata mimi sioni mantiki ya kuendelea kujadili au kutafuta hati, tufikirie ninikizuri cha kuandika kwenye katiba

Hiyo hati ikipatikana au isipopatikana what next? Nadhani Tanzania tunamatatizo mengine mengi zaidi tunayopaswa kuyajadili kuliko hili
 
Kwa maandishi haya nina hakika Pasco ndio Tundu Artipas Lissu, mbunge wa Singida na mwana sheria wa CHADEMA, kuanzia sasa nitakua nazisoma makala zako kwa ukaribu sana kuliko nilivyokua nikifanya huko nyuma.
 
Wanabodi,

Wakati sintofahamu kuhusu Hati Halisi za Muungano, ikiendelea, nawaomba Watanzania wenzangu tufike mahali tuambiane ukweli halisi kuwa Hati Halisi za Muungano", hazipo popote!, nakala iliyowasilishwa kwenye Bunge Maalum la Katiba, yenye saini ya Nyerere na Pius Msekwa!, ile sio hati ya muungano (Articles of The Union" bali ile ni Sheria ya Muungano!, "The Act Of Union!" iliyotungwa na Bunge la Tanganyika, ku ratify the "Artcles of Union", ambayo imesainiwa na Nyerere, Speker wa Bunge na Msekwa kama Katibu wa Bunge wa Wakati Huo!.

Pasco
Wanabodi,
Leo sikukuu ya Muungano, nafanya mapitio ya baadhi ya mabandiko ya muungano.

Japo waasisi wa muungano wetu huu adhimu ni Nyerere na Karume, muungano ni kama ndoa, kuna mtu ana proposes, mwingine anakubali, ndoa inafungwa. Kwenye muungano wetu huu adhimu, aliye proposes ni Nyerere, Karume akakubali. Nia ya Nyerere ni kwenda kwenye serikali moja. Wito kwa viongozi wetu, kama nia ya kweli ni kudumisha muungano, twende kwenye serikali moja. Tumuenzi Mwalimu Nyerere kwa kuyaishi maono yake!. Nawatakia Muungano Mwema.

Paskali
 
Back
Top Bottom