Kaseja atua yanga kwa milioni 40

Barthez, Dida , Kaseja, Yondan, na Chuji kweli Yanga ni SIMBA VETERANS siku mkifungwa na Simba msiseme Wamehujumu timu wakati Mnajihujumu wenyewe
 
Napenda kuwapongeza sana viongozi wetu wa yanga kwa kuangalia mbele na hasa ligi ya mabingwa, nadhani kama kuna sehemu imepwaya sana ndani ya kikosi chetu linapokuja suala la ligi ya mabingwa ni golini, pia ninashauri pia tusajili beki wa kati mmoja na nimemwona beki wa Liberty professional ya Ghana ambaye ni kapten wao anavaa jezi no:20, huyu angetufaa sana akicheza na Yondani. Nadhani tuna tatizo la kufungwa magoli ambayo hata huwezi elewa yanapitaje nadhani pia tunahitaji kiungo mkabaji mfano wa Jerry Santo na hapo tutakuwa na kikosi imara ambacho naamini tutafika mbali kwenye ligi ya mabingwa. Mwisho naomba kuuliza hali ya mwenyekiti wetu wa baraza la wadhamini mzee Kifukwe je kweli anaugua? Mwenye kujua tafadhali anijulishe.
 
Barthez, Dida , Kaseja, Yondan, na Chuji kweli Yanga ni SIMBA VETERANS siku mkifungwa na Simba msiseme Wamehujumu timu wakati Mnajihujumu wenyewe

Wachezaji wanasajiliwa kutokana na viwango vyao,hatusajili wachezaji wa kucheza na Simba tu.Chuji,Barthez,Yondani na Dida wameonyesha kiwango cha juu walivyotua Yanga kuliko walivyokuwa Simba.
 

Uko kwenye kimataifa mnaishia round ya kwanza, labda utoe sabubu nyingine
 
Uko kwenye kimataifa mnaishia round ya kwanza, labda utoe sabubu nyingine

Najua hizo ndo sala zenu na kwasasa mtasali sana maana sala ya kuishusha mbeya city nafasi ya tatu haijaisha mpaka january poleni sana wanalunyasi, hata hivyo michezo ipo mingi hata ya kung'oa viti mna vipaji nayo!!
 
Simba wasimpate kivipi! Kwani wanamtaka?

Mara ngapi washabiki tumelalamika juu ya kumtema Kaseja lakini hawajatusikia?

Sasa acha tule jeuri yatu kwa kukiacha kifaa kama Kaseja.

YANGA si walisikia SIMBA wanamtaka tena KASEJA wamemuongezea DAU. hivi unadhani YANGA wanashida ya kipa?
 
bora kushabikia Mbeya City! Yani yanga wanasijiri upuuzi bila kujali mahitaji ya timu! Ni kweli tatizo la yanga Kipa?

Wanachowaza Yanga ni kucheza na Simba, na kuwakomoa Simba tu. Ndio maana huwa hatufiki mbali kwenye michuano ya Kimataifa.
 

demu wake nani na ni mchungaji gani?inaonekana imekuuma sana kaseja kwenda yanga
 
Tatizo la yanga ni kucheza sana na akili ya simba!mi hua nashangaa sana hua hawafanyi vitu kwa mapungufu yao,si watu wakujiangaisha hupenda sana mteremko na huo ni udhaifu mkubwa sana!wana timu imara sana na ndio maana wako kileleni, lakini haikua timu yao akilini,timu kubwa ya yanga ni macho ya simba!kuna tatizo lakufanyia kazi hapo na si kulipotezea!
 

Hapo suala la simba linatoka wapi? Hoja ni kwamba yanga wamemsajili kaseja na ni mchezaji huru sasa ninyi inawasumbua nini?
 
Hapo suala la simba linatoka wapi? Hoja ni kwamba yanga wamemsajili kaseja na ni mchezaji huru sasa ninyi inawasumbua nini?

Nilihisi labda utakua umenielewa kumbe bado ! ni kweli anastahili kuja pale kwakua yuko huru.
 
Je unajuaaaa chimbuko la yanga ni vibaka na wavuta bangi kutoka uswahilini na chimbuko la simba ni vijana waliokuwa wakiishi mitaa ya uzunguni hivyo bado timu hizo zinaadhiliwa na asili hiyo.
 
YANGA si walisikia SIMBA wanamtaka tena KASEJA wamemuongezea DAU. hivi unadhani YANGA wanashida ya kipa?

Mimi ni mshabiki wa Simba, iliniuma Kaseja kuachwa kwa kashfa ya kwamba ameshuka kiwango badala tu ya kusema tumeshindwa kumeet mahitaji yake.

Mi naona Yanga hawamkomoi Simba, kwa sababu tayari Simba tulishajikomoa, na Yanga wamejua udhaifu wa Simba kwa kutokuwa na Kapteni Kaseja.
 
Hawa mameneja, lazima wa yao! haiwezekani kumsajili andunje Kaseja!Kuna deal imechezwa hapo
 
Kaseja amefanya maamuzi mazuri kujiunga na Yanga kwa kitita cha 40 milioni maana ndo uwezo wake ndo unakwenda ukingoni na Simba wangemchukua angekuja kuharibu wale vijana wanaoandaliwa na tabia zake za kuuza mechi amaenda kwa wataalamu wa kununua mechi.
 
Kaseja mchawi sana analoga sana wenzake

Kigogo. Mchawi wa Mtu ni mtu mwenyewe, Kubali usikubali Juma Kaseja ni golikipa mahiri kwa sasa hapa Tanzania. Simba kwa sababu ya Fitna na ujuaji wa Uongozi chini ya RAGE ndo maana walimuacha Juma Kaseja. Naipenda sana Simba ila kwa hili la Kaseja kutemwa sikuwa nao kabisa, hata kiwango kama kilishuka bado hata pale kilipokuwa kimefika hakuna Golikipa hapa Bongo alikuwa nacho. Nitamshabikia Kaseja hukohuko alikoenda ila Tukikutana, halahala Kaseja
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…