Kasi ya wachezaji wa Yanga uwanjani bado ni kitendawili?

Kasi ya wachezaji wa Yanga uwanjani bado ni kitendawili?

ToniXrated

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2022
Posts
1,134
Reaction score
2,993
Amani iwe nanyi

Sitoi pole kwa Yanga kwa kufungwa na Al hilal licha ya kumiliki sana mpira!! Natoa pole kwa wachezaji wa ligi nzima ya bongo kwa kushindwa kuwa na kasi kiwanjani pindi wanapokuwa na mpira ama wasipokuwa na mpira.

Nitaendelea sana kuongelea kasi/pace/speed ya wachezaji wetu katika hizi klabu kubwa hapa nchini kuwa hairidhishi na wala haiendani na mpira wa kisasa unaochezwa duniani.

Naona makocha wetu wanatumia muda mwingi kufundisha kitandaza mpira kwa maana ya kupiga pasi fupi fupi huku timu ikianza mashambulizi kutoka nyuma. Ni jambo jema ila amini kwamba mpira wa pasi bila ya kuwa na kasi inakuwa sawa na kupoteza muda.

Yanga jana nilikuwa nawashangaa jinsi wanavyosukuma mpira taratibu kana kwamba wao ndio walikuwa wanaongoza katika matokeo. Al hilal sio kwamba walikuwa wakicheza vizuri kuliko yanga, walikuwa wakicheza tu kimkakati na kasi ya wachezaji wao iliwanufaisha sana na kuwawezesha kuondoka na ushindi. Nilikuwa nashangaa sana jinsi mchezaji wa al hilal alivyokuwa akiwazidi mbio wachezaji wa Yanga na kufanikiwa kwenda kuonana na Diara uso kwa uso. Al Hilal silaha yao kubwa ilikuwa ni mbio huku wakijua kuwa wachezaji wengi wa yanga hawakimbii uwanjani ila wana jog tu .Wachezaji angalau wanampira wa kasi ni Tuisila Kisinda,Ambundo ,Shabani Juma na farid Musa. Waliobaki ni mwendo wa kobe.

Kama timu zetu zimeamua kucheza mpira wa pasi basi tuhakikishe kuwa wachezaji wanakimbia uwanjani pindi wawapo na mpira na pale wasipokuwa na mpira. Timu za waarabu hazina mafundi wengi wa soka ila wanajivunia uwezo wao wa kucheza mpira wa kasi .

Nina imani siku tutakapoweza kucheza mpira kwa kasi ndio siku ambayo tutaweza kubeba kombe la klabu bingwa Africa.
 
Hiyo kasi unayoitaka zungumzia yanga yako tu, achana na simba ambaye yupo ndani ya top 15 ya vilabu bora barani Africa.
Wanajua kucheza kikubwa na kimalengo.
Usilinganishe aliye nafasi ya 14 na yule wa 75
 
[emoji856]
IMG-20221016-WA0385.jpg
 
Mpira sio riadha,inategemea na mbinu mnayotumia, alhilal walikua wanakimbia kwa sababu yanga walikua wanaacha nafasi kubwa wanaposhambulia na hivyo kutoa nafasi ya kukimbia kwenye counter.

Huyo kisinda unaesema ana mbio hata sasa bado ana mbio lakini alhilal walikua nyuma muda mwingi na hakukua na hiyo nafasi ya kukimbia.

Kwa kifupi huingii uwanjani kukimbia tu hovyo ila mbinu yenu na dhidi ya timu pinzani ndio itakayoamua mkimbie au mcheze kama timu kwa pasi.
 
Hiyo kasi unayoitaka zungumzia yanga yako tu, achana na simba ambaye yupo ndani ya top 15 ya vilabu bora barani Africa.
Wanajua kucheza kikubwa na kimalengo.
Usilinganishe aliye nafasi ya 14 na yule wa 75
Tumia akili basi acha uparacite mzee daah
 
Hiyo kasi unayoitaka zungumzia yanga yako tu, achana na simba ambaye yupo ndani ya top 15 ya vilabu bora barani Africa.
Wanajua kucheza kikubwa na kimalengo.
Usilinganishe aliye nafasi ya 14 na yule wa 75
Simba ipo nafasi ya 14 afrika? [emoji1787]
 
Kwamba mayele, aziz ki, morison hawana kasi? Nadhan tatzo ni viungo na mabeki aisee walikuwa wanacheza utumbo sn wamerelax as if wameshamtoa al hilal daaah nlitaman ningie kwny tv niwapge kama ngoma. Morison aondolewe haraka kwny timu anakwenda kuigawa timu
 
Amani iwe nanyi

Sitoi pole kwa Yanga kwa kufungwa na Al hilal licha ya kumiliki sana mpira!! Natoa pole kwa wachezaji wa ligi nzima ya bongo kwa kushindwa kuwa na kasi kiwanjani pindi wanapokuwa na mpira ama wasipokuwa na mpira.

Nitaendelea sana kuongelea kasi/pace/speed ya wachezaji wetu katika hizi klabu kubwa hapa nchini kuwa hairidhishi na wala haiendani na mpira wa kisasa unaochezwa duniani.

Naona makocha wetu wanatumia muda mwingi kufundisha kitandaza mpira kwa maana ya kupiga pasi fupi fupi huku timu ikianza mashambulizi kutoka nyuma. Ni jambo jema ila amini kwamba mpira wa pasi bila ya kuwa na kasi inakuwa sawa na kupoteza muda.

Yanga jana nilikuwa nawashangaa jinsi wanavyosukuma mpira taratibu kana kwamba wao ndio walikuwa wanaongoza katika matokeo. Al hilal sio kwamba walikuwa wakicheza vizuri kuliko yanga, walikuwa wakicheza tu kimkakati na kasi ya wachezaji wao iliwanufaisha sana na kuwawezesha kuondoka na ushindi. Nilikuwa nashangaa sana jinsi mchezaji wa al hilal alivyokuwa akiwazidi mbio wachezaji wa Yanga na kufanikiwa kwenda kuonana na Diara uso kwa uso. Al Hilal silaha yao kubwa ilikuwa ni mbio huku wakijua kuwa wachezaji wengi wa yanga hawakimbii uwanjani ila wana jog tu .Wachezaji angalau wanampira wa kasi ni Tuisila Kisinda,Ambundo ,Shabani Juma na farid Musa. Waliobaki ni mwendo wa kobe.

Kama timu zetu zimeamua kucheza mpira wa pasi basi tuhakikishe kuwa wachezaji wanakimbia uwanjani pindi wawapo na mpira na pale wasipokuwa na mpira. Timu za waarabu hazina mafundi wengi wa soka ila wanajivunia uwezo wao wa kucheza mpira wa kasi .

Nina imani siku tutakapoweza kucheza mpira kwa kasi ndio siku ambayo tutaweza kubeba kombe la klabu bingwa Africa.
Bahati mbaya hao uliowataja wana kasinisiyo na faida kwa timu.
 
Back
Top Bottom