Mwanongwa
JF-Expert Member
- Feb 15, 2023
- 611
- 567
Licha ya sisi Wananchi kulalamika kila mara lakini ni kama Mamlaka zinazohusika zimeziba masikio, kwa kuwa haitusikii, wanatatuaje kilio chetu.
Kwenye kata yetu ya Kijombe, Wilaya ya Wanging'ombe hapa Njombe uhaba wa maji ni kilio kikubwa kwa baadhi ya Wananchi hali inayosababisha kutumia maji ya kwenye madimbwi.
Mamlaka ya Maji Wanging'ombe (WANGIWASA) wameweka mgao usiyokuwa na maana, kwenye kila Kijiji maji ya Bomba yanatoka mara mbili kwa mwezi.
Hii ni hatari sana kwa Watoto wa Sekondari ya Kijombe ambao wanalazimika kwenda kutafuta maji kwenye maeneo hatarishi.
Hapa wakipatwa na majanga mbalimbali lawama itakuwa kwa nani? Maana Kwa shida hizi wanazozipitia ni balaa, Mamlaka za Maji zitusaidie hali hii siyo nzuri na inaweza kuchangia kuibuka kwa magonjwa ya tumbo.
Pia soma ~ Wakazi wa Kijombe, Wilaya ya Wanging'ombe (Njombe), kwenye huduma ya maji tunaisikia kwenye bomba
Kwenye kata yetu ya Kijombe, Wilaya ya Wanging'ombe hapa Njombe uhaba wa maji ni kilio kikubwa kwa baadhi ya Wananchi hali inayosababisha kutumia maji ya kwenye madimbwi.
Mamlaka ya Maji Wanging'ombe (WANGIWASA) wameweka mgao usiyokuwa na maana, kwenye kila Kijiji maji ya Bomba yanatoka mara mbili kwa mwezi.
Hii ni hatari sana kwa Watoto wa Sekondari ya Kijombe ambao wanalazimika kwenda kutafuta maji kwenye maeneo hatarishi.
Hapa wakipatwa na majanga mbalimbali lawama itakuwa kwa nani? Maana Kwa shida hizi wanazozipitia ni balaa, Mamlaka za Maji zitusaidie hali hii siyo nzuri na inaweza kuchangia kuibuka kwa magonjwa ya tumbo.
Pia soma ~ Wakazi wa Kijombe, Wilaya ya Wanging'ombe (Njombe), kwenye huduma ya maji tunaisikia kwenye bomba