Katavi: Wanaume wanaogopa kuwawezesha kiuchumi wake zao wanaamini watakuwa jeuri

Katavi: Wanaume wanaogopa kuwawezesha kiuchumi wake zao wanaamini watakuwa jeuri

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
525
Reaction score
1,257
UMESIKIA ishu ya baadhi ya wanaume wa Kijiji cha Mapili Kata ya Ilela, Halmashauri ya Mlele mkoani Katavi?
d33a986a-e922-417f-bf40-2113c80aef21.jpg
Kama hujasikia ipo hivi, kumbe wanatamani sana kuwawezesha wake zao kiuchumi, lakini wanashindwa kuwawezesha kiuchumi wakihofia wanawake hao kubadilika na kutowasikiliza wakiwa na kipato.

Hayo yamebainika katika mdahalo maalum ulioandaliwa na Shirika lisilo la kiserikali la Marie Stopes Tanzania kwa kushirikiana na wadau mbalimbali uliofanyika jana Julai 12, 2022 katika Kijiji cha Mapili Kata ya Ilela, kwa lengo kutoa elimu ya afya ya uzazi na masuala ya ukatili wa kijinsia.

Akichangia mada kwenye kongamano hilo, Yohanne Samuel alidai wake zao wakipata fedha hujiona wapo juu ya waume zao na ushahidi mzuri ni pale wanapovunja vikundi vyao maarufu kama Vikoba.

“Wakipata fedha za Vikoba huwa wanakuwa wakali kwa kujiona wana fedha nyingi, ndiyo sababu tunaogopa kuwasaidia kiuchumi, watatunyanyasa sana,” alisema Abdul Japhar.

"Sisi wanaume sio wanyanyasaji, isipokuwa wake zetu ndio hutunyanyasa, kwa sababu utakuta mtu unampa mtaji halafu baadaye anakuja kukugeuka," alisema Juma Kapangano kwenye kongamano hilo.

Kwa upande wao walengwa ambao ni wanawake wa kijiji hicho wamedai kuachiwa majukumu ya kifamilia na waume zao, hali inayofanya wao kutaka kujishughulisha na biashara ndogondogo, ili kulea watoto wao.

"Mwanaume anaweza kutoka, akirudi anadai chakula tena anaweza kukupiga wakati hajaacha hata pesa ya chakula, wala mboga, hivyo ili kuhakikisha familia inakula inakubidi wewe mwanamke uhangaike," alisema Rosemary Alex

"Wanawake tunanyanyasika sana hata magonjwa haya ya VVU kwa asilimia 99 Kijiji chetu wanaweza kuwa wamechangia wanaume, kwa sababu mwanamke anaweza kushawishika kutafuta pesa kwa njia zisizo rasmi kama kuchepuka,” amesema Gaudensia Issa.

Naye mshauri wa masuala ya kijinsia, vijana na makundi maalum kutoka shirika la Marie Stopes, Magdalena Thomas amesema wamebaini kwamba wananchi wa kijiji hicho hawana uelewa na masuala ya ukatili wa kijinsia.

"Kuna elimu duni kwenye masuala ya ukatili wa kijinsia pamoja na afya ya uzazi, hivyo tunaendelea kufanyia kazi pamoja na kuhamasisha wadau wengine waweze kufika na kutoa elimu hiyo," alisema.



Source: Habari Leo
 
Kuna wengine mmelelewa na mama zenu na wamewaraise kuwa wanaume bora ilhali shida walizopitia. Wanawake wenye hekima na hofu ya Mungu pamoja na kuheshimu mume katika ndoa wapo. Sawa kuna muda wanaume mnao udikteta lakini ukizidi sana ndo wanawake wanataman kuongea na mnawaita feminist kumbe wanajitetea. Ukiwa mwanaume bora na mkawa as one wenye nia moja kwenye ndoa mwanamke hatakuwa na kiburi kwanza kitokee wapi???

Msiwakandamize na kuwaumiza huku mkijisifia nyie ni vidume....hapo ndo penye shida. Atavumilia akichoka ndo matatizo huanzia hapo. Men should change too period!!!!
 
Kuna wengine mmelelewa na mama zenu na wamewaraise kuwa wanaume bora ilhali shida walizopitia. Wanawake wenye hekima na hofu ya Mungu pamoja na kuheshimu mume katika ndoa wapo. Sawa kuna muda wanaume mnao udikteta lakini ukizidi sana ndo wanawake wanataman kuongea na mnawaita feminist kumbe wanajitetea. Ukiwa mwanaume bora na mkawa as one wenye nia moja kwenye ndoa mwanamke hatakuwa na kiburi kwanza kitokee wapi???

Msiwakandamize na kuwaumiza huku mkijisifia nyie ni vidume....hapo ndo penye shida. Atavumilia akichoka ndo matatizo huanzia hapo. Men should change too period!!!!
Mama wa zamani si sawa na hawa wa sasa wanaogombania haki sawa 50 kwa 50. Akipata hela ndo utamtambua anakufanya house boy kabisaaa!
 
Huwa tunaona hata kwenye maofisi wanawake wanavyokuwa na kiburi na dharau.
Mwanamke anadharau kama siyo mtulivu wa akili unaua kabisa. Bora akae nyumbani tu ukimwezesha akifanikiwa anatafuta mfanyabiashara mwenzake ukute wewe ni boda boda.
Kuna wengine mmelelewa na mama zenu na wamewaraise kuwa wanaume bora ilhali shida walizopitia. Wanawake wenye hekima na hofu ya Mungu pamoja na kuheshimu mume katika ndoa wapo. Sawa kuna muda wanaume mnao udikteta lakini ukizidi sana ndo wanawake wanataman kuongea na mnawaita feminist kumbe wanajitetea. Ukiwa mwanaume bora na mkawa as one wenye nia moja kwenye ndoa mwanamke hatakuwa na kiburi kwanza kitokee wapi???

Msiwakandamize na kuwaumiza huku mkijisifia nyie ni vidume....hapo ndo penye shida. Atavumilia akichoka ndo matatizo huanzia hapo. Men should change too period!!!!
 
Ukitaka ndoa ife jifanye unamsapoti kiuchumi na Mungu ajalie afanikiwe! Ndo utajua wazee wetu walotaka wake zao wakae home waitunze nyumba hawakuwa wajinga
 
Nakubaliana na wewe. Kiasili mwanamke akipata pesa, cheo hushindwa kuhimili utamu wake na hutaka yeye aheshimiwe.
Si anaona humbabaishi kwa chochote, hata kama unatoa fungu flani la matumizi, mwisho wa siku atakwambia anakulea na kukuvisha
 
Kuna jamaa yangu alimsomesha mke wake hadi akaoata degree, alimpeleka kutembea ulaya,alimpaga mtaji wa biashara,akamsaidia kumtafutia ajira

Kukatokea tatizo dogo mke alimkimbia

Ila jamaa nlishawahi muonya, majibu yake kwangu ilikuwa"nyie wahuni walevi mnajua nini [emoji1]

Mke akadai hawana chemistry na mme,kumbe mwanamke alimfanya jamaa ngazi

Ova
 
Kuna wengine mmelelewa na mama zenu na wamewaraise kuwa wanaume bora ilhali shida walizopitia. Wanawake wenye hekima na hofu ya Mungu pamoja na kuheshimu mume katika ndoa wapo. Sawa kuna muda wanaume mnao udikteta lakini ukizidi sana ndo wanawake wanataman kuongea na mnawaita feminist kumbe wanajitetea. Ukiwa mwanaume bora na mkawa as one wenye nia moja kwenye ndoa mwanamke hatakuwa na kiburi kwanza kitokee wapi???

Msiwakandamize na kuwaumiza huku mkijisifia nyie ni vidume....hapo ndo penye shida. Atavumilia akichoka ndo matatizo huanzia hapo. Men should change too period!!!!
Bado hayajakukuta ndugu, mwanamke kiumbe tofauti sana

Sent from my SM-S920L using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom